Mambo Mawili Ya Kuzingatia Katika eneo La Fedha

Moja, USICHEZE NA HELA. Kuwa makini na hela zako, zisimamie vizuri na wekeza sehemu salama unayoweza kuifuatilia kwa umakini. Mbili, USIENDE MAHALI NA FEDHA UNAYOTAKA KUTUMIA TU. Kwa kifupi kwenye maisha usiwe na kiasi cha fedha unachohitaji kwa matumizi tu, unahitaji kuwa na kiasi cha fedha kwa ajili ya dharura. Hatua ya kuchukua leo; USICHEZE …

Unakuwa Wa Maana Pale Unapofanya Hiki

Rafiki yangu nikupendaye, Kwenye maisha unakuwa wa maana pale unapotimiza wajibu wako. Kwenye biashara unakuwa wa maana pale unapotekeleza wajibu wako kwenye biashara. Na ustaarabu wa kwanza kwenye biashara ni kuuza na kama huuzi kwenye biashara basi unapoteza maana. Unapoteza maana kama uko kwenye kazi fulani halafu huifanyii kazi hiyo kazi. Unapoteza maana kwenye mahusiano …

Zifahamu Tabia Mbili Za Watu

Sina uhakika kama itakufaa lakini watu wana tabia kuu mbili nazo ni; Kwanza  watu  ni viumbe  wa  kijamii  kwa  sababu wanawapenda  na  kuwajali  watu  ambao  wapo  ndani ya  kundi moja. Nafikiri hili halina ubishi, binadamu ni watu wa ambao tunajali wale ambao tupo kundi moja. Kwa mfano, shabiki wa timu x atamjali shabiki timu x …

Usimwambie Mtu, Nimekuambia Wewe Tu

Ni maneno ambayo watu huyatumia kujihakikishia usalama pale wanapotoa jambo lao kwa watu wengine. Usijidanganye kwamba ukimwambia mtu hivyo ndiyo mambo yatakuwa safi bali ndiyo kama vile umemwambia fanya. Kama una jambo lako na unataka watu wasijue ni bora usiseme kabisa kuliko kusema halafu unamwambia nimekuambia wewe tu lakini usimwambie mtu mwingine.Wimbo unakuwa ni mmoja …

Huenda Hujafanya Jukumu Lako Vizuri

Dunia itakuwa sehemu salama kwa kila mmoja wetu endapo kila mmoja wetu atatimiza wajibu wake. Matatizo mengi yanayotokea ni watu kushindwa kutimiza majukumu ipasavyo. Ukishindwa kutimiza wajibu wako jua kwamba unawaumiza wengine. Kila mmoja wetu anamtegemea mtu mwingine ili maisha yake yaende. Endapo unasitisha kile unachofanya basi unakuwa siyo tu kufanya dhambi lakini unaifanya dunia …

Mbinu Nzuri Ya Kutumia Pale Unapoona Umetingwa Na Mambo Mengi

Ukiona umebanwa na una mambo mengi ya kufanya huku muda wako ukiwa mchache unapaswa kufanya yafuatayo; Moja, futa yale yote yasiyo na tija kwako. Watu wengi wanasema wako bize lakini kwenye mambo ambayo hayana tija kwao. Jiulize, hicho kinachokufanya uwe bize kinaleta fedha mfukoni? Kama jibu ni ndiyo, endelea kukifanya lakini kama jibu ni hapana, …

Kitu Cha Kwanza Kuangalia Kabla Hujamsaidia Mtu

Pata picha unatoka nje ya nyumba yako unaona moshi unatoka mahali na ukakimbilia kuondoa moshi huo, kawaida hutazuia moshi kuendelea kutoka kwa sababu kwa akili za kawaida kabisa penye moshi, chini pana moto. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye watu, unapomwona mtu yupo kwenye matatizo, jua kuna kitu kimesababisha. Sasa ukikimbilia kumsaidia kumsaidia mtu kuondokana na …

Licha Ya Madhaifu Yako, Bado Wewe Ni Mtu Muhimu Sana

Rafiki yangu nikupendaye, Pamoja na madhaifu yako, bado wewe ni muhimu. Moja ya mambo yanayopelekea tusijijali sana ni kwa sababu tunajijua sisi wenyewe kuliko mtu mwingine anavyotujua, kuliko tunavyowajua watu wengine. Sasa inapotokea pale tunapojikumbusha madhaifu yetu, mabaya ambayo tumewahi kufanya huko nyumaz tunajiona tunastahili mateso na hivyo kutokujijali kama tunavyowajali wengine. Tunakuwa tunajiona sisi …

Jinsi Mabadiliko Yanavyokuua

Ray Norda anasema ukisababisha mabadiliko, unakuwa kiongozi wa mabadiliko, unakuwa kwenye nafasi kubwa ya kufanikiwa. Na pale unapokabiliana na mabadiliko, unapona kwenye Mabadiliko hayo. Lakini pia mabadiliko hayatakupoteza. Ila ukiyapinga mabadiliko, mabadiliko yanakuua na yanakupoteza kabisa. Hatua ya kuchukua leo; popote pale ulipo, kuwa chanzo cha mabadiliko na mara zote utakua mbele na kufanikiwa. Kitu …

Maisha Gani Haya?

Kwako rafiki yangu, Usikubali kuishi maisha ambayo hayana maana hapa duniani. Usikubali kuishi bila kujifunza, unapojifunza unapata hekima ya kukuwezesha kufanya maamuzi. Usikubali kufanya kazi pasipo kuwekeza wala kuweka akiba. Uwekezaji unakuza utajiri wako na akiba inakulinda wakati unauhitaji wa fedha. Usikubali mtu akupite kwenye kazi, kubali watu wakupite maeneo yote lakini usikubali upitwe katika …

Design a site like this with WordPress.com
Get started