Iko hivi rafiki yangu, Mahusiano mazuri ni maisha mazuri na mahusiano mabaya ni maisha mabaya. Hakuna mafanikio yanayopatikana katika mahusiano mabaya, ukitaka kuwa na mafanikio unapaswa kuwa na mahusiano mazuri na wale unaojijusisha nao.Mahusiano mabaya yanaumiza, yanakufanya ushindwe kufokasi katika kazi. Muda mwingi utautumia katika kusuluhisha migogoro badala ya kufanya kazi. Weka juhudi kwenye kujenga …
Huwa Inatokea Lakini Usifanye Kila Siku
Huwezi ukapanga mambo yako na yakaenda vizuri kila wakati. Kuna wakati mambo yanaenda vizuri na kuna wakati mambo yanaenda ndivyo sivyo. Kuna wakati unaanguka kama binadamu lakini katika msimamo wako ulioamua kufanya usiuvunje mara pili. Dharura huwa zinatokea lakini usikubali iwe kila siku kwa mfano, kuchelewa kufika eneo la kazi, biashara au miadi yoyote ile. …
Ung’ang’anizi Wa Muda Mrefu
Watu wengi wamekuwa hawana subira kwenye maisha yao. Wanaanzisha kitu leo na wakiona hakina matokeo ndani ya muda mfupi wanaamua kuachana nacho.Kitu chochote ukitaka kujua kama kitakunufaisha au la unatakiwa ukifanyanye ndani ya miaka 10. Ndiyo, jitoe ndani ya miaka 10 kupitia kile ulichoamua kukifanya na utaona matokeo. Kazi uliyoamua kuifanya jipime ndani ya miaka …
Leo Hakuna Taarifa Ya Habari
Pata picha umejiandaa kusikiliza au kuangalia taarifa ya habari ukiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua dunia inaendaje au nini kimetokea, halafu anakuja mtangazaji wa taarifa ya habari anakuambia zima TV au radio yako nenda kalale leo hakuna habari, je utajisikiaje?Watu wanapenda habari na hata ukiwaambia hakuna habari hawawezi kukuelewa. Na hata habari nyingi unazozisikia …
Utakuja Kumwitaji Tena Baadaye
Milima huwa haikutani ila binadamu tunakutana, wahenga walisema hivyo. Jamii yetu imekuwa na mtazamo wa hovyo na wa tofauti sana. Mtu anapokuwa anahusiana na mtu mambo yanakuwa mazuri lakini wakishindwa kuelewana kwenye kitu kidogo tu, basi kisirani kinaanzia hapo. Sina uhakika kama itakufaa lakini kama umeachana na msaidizi wako kwenye biashara, nyumbani, mpenzi au mchumba …
Hakuna Unachojenga
Biashara yoyote ambayo haina mfumo ni sawa na kujenga nyumba bila msingi, itaanguka muda wowote ule. Mahusiano bila misingi inayoendesha mahusiano hayo ni rahisi kuanguka.Kazi yoyote isiyokuwa na misingi huwa ni rahisi kupoteza mwelekeo. Kitu chochote kile ambacho hakina mwelekeo, huwa mwelekeo wowote ule unauchukua. Kuwa na mfumo wa kuendesha kila kitu kwenye maisha yako. …
Namba Hazidanganyi
Ukiwauliza maswali watu kwamba wanaendeleaje? Watakujibu wanaendeleaje vizuri tu, wengine watasema Mungu anasaidia kwa kweli. Ukija katika upande wa namba majibu wanayotoa watu na namba haziendani kabisa kwa mfano, kwenye biashara, muulize mtu biashara yako inaendaje? Atakujibu inaendelea vizuri tu, Sasa ukitaka kumuuliza namba kwa mfano,mauzo yako yakoje?una wateja wangapi, wangapi ni wapya na wangapi …
Kama Unauchukia Umasikini Huwezi Kuwa Hivi
Umasikini siyo utakatifu wala utajiri siyo dhambi. Kama umasikini unakuumiza na unapenda kweli kubadilika kwenye maisha yako, huwezi kuwa na mjadala kwenye kazi. Kama unataka kufika mbali, huwezi kuwa na mjadala kwenye mambo yako muhimu kama vile uamke asubuhi na mapema ukafanye kazi au ulale. Huwezi kuwa na mjadala kwenye mambo muhimu, yaani ukipanga umepanga, …
Continue reading "Kama Unauchukia Umasikini Huwezi Kuwa Hivi"
Watu Wanakuchukuliaje?
Ni rahisi sana, watu wanakuchukulia kwa namna unavyojichukulia wewe. Ukijichukulia mwaminifu na watu watakuchukulia mwaminifu. Na mara nyingi binadamu huwa tunatoa kile ambacho tunacho. Hatuwezi kutoa kile ambacho hatuna. Hata kama kuna mtu anaigiza hali fulani kwenye maisha hawezi kudumu naye hata siku moja. Watu wanakuchukulia jinsi unavyojichukulia wewe mwenyewe. Tuwe makini, sisi ni kioo, …
Penye Nia Pana Njia
Ukiwa unataka kufanikiwa kitu, utafanikiwa kama kweli umejitoa na kuwa king'ang'anizi bila kujali ukinzani wowote ule. Fuata nia yako ya ndani na hakuna kitakachokuzuia. Dunia itakupisha kama kweli na wewe umejitoa. Hujawahi kuona unawaza kitu fulani halafu unashangaa unakutanishwa na mazingira ya kitu hicho? Au unamfikiria mtu halafu unashangaa anakupigia simu au anakutembelea. Ndani yetu …