Ni kauli ya Mungu kwa watu wake wote wanaotafuta kile wanachotaka. Mungu amesema ombeni nanyi mtapewa lakini cha kushangaza watu hao wanakwenda kinyume na kauli ya Mungu. Watu hawaombi, kama ukiomba lazima dunia itakupa. Kama huombi usitegemee kama dunia itakupa kile unachotaka kwenye maisha yako. Kama wewe ni muuzaji wa kitu, waombe watu wanunue, waombe …
Usiweke Malengo Haya Kamwe
Malengo ambayo unajua unaweza kuyafikia. Usiwe na malengo ya kimasikini, kuwa na malengo ya kitajiri. Masikini anaweka malengo ambayo anaweza kuyafikia na tajiri anaweka malengo ambayo hawezi kuyafikia. Kwa mfano, tajiri anaweka malengo makubwa ambayo yatamsukuma zaidi kufika mbali hata asipoyafikia malengo yake makubwa basi hata akifikia nusu yake inakuwa ni faida. Usiweka malengo ambayo …
Fanya Kazi Na Upumzike
Ni kweli kabisa kazi ndiyo rafiki wa kweli. Na ninasisitiza watu wafanye kazi kwa sababu kupitia kazi watapata kile wanachotaka. Hata Mungu katika uumbaji wa dunia, aliweza kufanya kazi na kupumzika. Jitahidi sana uweze kupumzika baada ya kufanya kazi wiki nzima.Usipopumzika unatafuta kupata uchoshi ambao utakulazimisha uumwe kwa lazima. Mwili nao unahitaji kupumzika ili uweze …
Ujumbe Muhimu Kwako Kutoka Kwa Elbert Hubbard
Juzi nilipokea zawadi kutoka kwa rafiki yangu Kocha Dr Makirita Amani, ni zawadi ya kijitabu kidogo ambacho amechambua ujumbe wa insha kutoka Garcia, ujumbe kwenda kwa Garcia yaani A message to Garcia. Naomba ninukuu kama ilivyo kutoka kwa Elbert Hubbard. Kama unamfanyia mtu kazi, mfanyie kazi kweli. Kama anakulipa mshahara unaoweza kukupatia mkate na siagi …
Continue reading "Ujumbe Muhimu Kwako Kutoka Kwa Elbert Hubbard"
Usiahirishe Kuishi Bali Ishi Sasa
Watu wengi wamekuwa hawayafurahii maisha yao kwa sababu wamekuwa wanaahirisha kuishi. Kwa mfano, mpaka nikiwa na nyumba au nikiwa na gari ndiyo nitaanza kuishi na kuwa na maisha ya furaha. Wanasubiri mpaka kila kitu kiwe sawa ndiyo wafanye yale wanayotaka kufanya. Unapaswa kujua maisha hayakusubiri wewe uwe tayari, bali yanaendelea kwenda. Hivyo wajibu wako ni …
Ni Kipi Kikubwa Kinachoweza Kukushinda?
Kuna hadithi moja mwandishi Robin Sharma anasimulia katika kitabu chake cha The everyday Hero Manifesto. Robin Sharma anatushirikisha mgonjwa aliyeandika kitabu kwa njia ya kukonyeza. Unaweza kushangaa imewezekanaje, lakini tayari imeshawezekana na rekodi imeshawezekana. Robin Sharma anatushirikisha hadithi ya Jean -Dominique Bauby ambaye alikuwa na maisha mazuri na ya mafanikio. Siku moja akapatwa na kiharusi …
Unakosa Kitu Hiki Muhimu
Hakuna kitu kipya mpaka sasa,mara nyingi mambo ni yaleyale lakini kwa nini inakuwa vigumu watu kuchukua hatua au kufanikiwa kwenye jambo fulani? Unafikiri ni kwa nini watu wanakuwa vilevile kila mara? Ni kwa sababu watu wanakosa uwajibikaji. Ni rahisi mwasibu aliyeajiriwa kufanya kazi vizuri alipoajiriwa ila ukija kwenye maisha yake binafsi hata mipango binafsi wala …
Hii Ndiyo Sehemu Pekee Ambayo Mafanikio Yanakuja Kabla Ya Kazi
Ni kwenye kamusi hakuna sehemu nyingine. Kamusi ndiyo sehemu pekee ambayo mafanikio yanakuja kabla ya kazi. Kufanya kazi kwa juhudi ndiyo gharama tunayolipa ili kufanikiwa. Vince Lombardi — Sina uhakika kama itakufaa lakini kazi ndiye rafiki wa kweli. Fanya kazi na achana na biashara nyingine ambazo hazina mchango wa kukufikisha kule unakotaka kufika. Linda muda …
Continue reading "Hii Ndiyo Sehemu Pekee Ambayo Mafanikio Yanakuja Kabla Ya Kazi"
Mambo Mawili Ya Kuzingatia Katika Fedha
USICHEZE NA HELA, kuwa makini na hela zako, zisimamie vizuri na wekeza sehemu salama unayoweza kuifuatilia kwa umakini.USIENDE MAHALI NA FEDHA UNAYOTAKA KUTUMIA TU. Kwa kifupi kwenye maisha usiwe na kiasi cha fedha unachohitaji kwa matumizi tu, unahitaji kuwa na kiasi cha fedha kwa ajili ya dharura. Kila mara yanatokea mambo ambayo hatukutegemea yatokee, kama …
Kama Mtu Akiwa Anataka Kitu
Huwa anafanya na anakipata. Ikiwa mtu hataki kitu, hawezi kukuambia ukweli bali atakuonesha sababu ambazo ukizichunguza vizuri unakuta siyo za kweli ila anakupa sababu kwa sababu anaogopa kukuambia ukweli na akikuambia ukweli utajisikia vibaya. Mtu ambaye anataka kitu utaona nia yake ya kweli hata kama amewekewa vipingamizi. kwa mfano, watu watano waliitwa katika usaili, watatu …