Kuna watu wanataka mteja anunue leo, kabla hata hajawaamini. Lakini ukweli ni huu: Mteja hanunui bidhaa tu. Ananunua pia imani kwamba atapata kile unachomuahidi. Ndiyo maana usikimbilie kumwambia: βNunua sasa!β Kwanza msaidie kuelewa. Mweleze ukweli hata kama si faida yako kubwa.Timiza ulichoahidi.Usifiche taarifa muhimu.Usiahidi kitu usichoweza kutimiza. Kwa sababu unaweza kupata mauzo leo kwa kumshawishi …
π₯ FOLLOW-UP SI USUMBUFU β NI SEHEMU YA MAUZO
Mteja akisema: βNitaangalia kwanza.β Usichukulie moja kwa moja kwamba amekukataa. Wakati mwingine hajakataa.Bado hajawa tayari kuamua. Tatizo ni kwamba wauzaji wengi wakikosa jibu la haraka, wanamwacha mteja na kuendelea kutafuta wengine. Kumbuka: Mteja anaweza kuwa na nia leo, lakini akawa tayari kununua kesho. Ndiyo maana follow-up ni sehemu ya kazi ya mauzo. Lakini follow-up si …
Continue reading "π₯ FOLLOW-UP SI USUMBUFU β NI SEHEMU YA MAUZO"
π° FEDHA YAKO INAPASWA KUFANYA KAZI PIA
Kuna watu wanafanya kazi maisha yao yote kutafuta fedha. Lakini kuna tofauti kubwa kati ya kutafuta fedha na kujenga mfumo ambao fedha nayo inakutafutia fedha. Ukipata fedha na zote zikaishia kwenye matumizi, kila mwezi itabidi uanze tena kutafuta. Lakini ukiweza kutenga sehemu ya fedha yako na kuipeleka kwenye kitu kinachoweza kuongeza thamani au kuzalisha kipato, …
Continue reading "π° FEDHA YAKO INAPASWA KUFANYA KAZI PIA"
UKITAKA KUPATA KUTOKA KWA WENGINE, JIFUNZE KUTOA KWANZA
Kwa nini watu hawakupi kile unachotaka? Huenda si kwa sababu hawakupendi.Huenda si kwa sababu hawana uwezo wa kukusaidia.Huenda ni kwa sababu hujawahi kujiuliza wewe una thamani gani kwenye maisha yao. Ukweli ni huu: Kila mtu ana maumivu anayopitia, hitaji analotafuta na tatizo analotamani kulitatua. Na kama unataka kuwa muhimu kwenye maisha ya mtu, jifunze kwanza …
Continue reading "UKITAKA KUPATA KUTOKA KWA WENGINE, JIFUNZE KUTOA KWANZA"
π° JILIPE KWANZA KABLA HUJAANZA KUTUMIA
Watu wengi hufanya hivi: Wanapata fedha, wanalipa kila kitu, wanatumia, wakibakiwa na kitu ndipo wanaweka akiba. Tatizo? Mara nyingi hakibaki kitu. Badili mfumo. Unapopata fedha, tenga sehemu kwa ajili ya kesho kabla hujaanza kutumia kwa leo. Si lazima iwe kubwa. Hata 5% au 10% ya kipato chako inaweza kuwa mwanzo. π― Siri si kiasi pekee. …
Continue reading "π° JILIPE KWANZA KABLA HUJAANZA KUTUMIA"
TATIZO SI KUPATA FEDHA TU β JIFUNZE KUZISIMAMIA
Watu wengi wanaposema, βNahitaji fedha zaidi,β mara nyingi wanamaanisha wanahitaji maisha bora. Lakini kuna swali muhimu zaidi: Ukiongeza kipato chako leo, utazisimamiaje hizo fedha? Kwa sababu unaweza kupata milioni 1 na ikaisha. Unaweza kupata milioni 5 na ikaisha. Unaweza hata kupata milioni 10 na bado ukabaki ukisema, βSijui fedha zangu zinaishia wapi.β Tatizo si kipato …
Continue reading "TATIZO SI KUPATA FEDHA TU β JIFUNZE KUZISIMAMIA"
PIMA MAENDELEO YAKO KABLA HUJAHUKUMU MAISHA YAKO
Wakati mwingine tunahisi hatujaendelea kwa sababu tunaangalia sana kile ambacho bado hatujapata. Lakini jiulize: Mwezi uliopita nilikuwa wapi, na leo niko wapi? Huenda bado hujafika unapotaka kufika, lakini: Umejifunza kitu kipya. Umeongeza wateja. Umeanza kuweka akiba. Umeacha tabia fulani. Umeongeza nidhamu. Umeanza kuchukua hatua. Hayo ni maendeleo. Usijipime kwa maisha ya wengine. Jipime dhidi ya …
Continue reading "PIMA MAENDELEO YAKO KABLA HUJAHUKUMU MAISHA YAKO"
Kwa Nini Isiwe leo?
Kama kuna kitu kinapaswa kufanyika basi kifanye mara moja. Huna haja ya kukichelewesha kusubiria baadaye, kesho, mwakani au mwezi ujao. Leo ni kesho ya jana, kama umepanga kufanya kitu leo , kifanye tu leo. Kama kitu ni muhimu kifanye tu, ipangilie siku yako na fanya yale yote uliyopanga kufanya. Usiahirishe mambo, muda pekee ulionao ni …
Hii Ndiyo Roho Unayopaswa Kuwa Nayo
Rafiki, Kwenye safari ya mafanikio, kuna changamoto nyingi ndani yake.Kama mtu hujajitoa hasa na hujui kile unachotaka ni rahisi mno kuishia njiani. Unatakiwa kuwa na nia ya dhati kabisa ya kutaka kufanikiwa.Mtu yeyote, mwenye nia ya dhati kabisa kwenye kile anachotaka lazima atajitoa na kukipata kile anachotaka. Huwa tunajitoa kweli kama kitu tunakitaka kweli. Roho …
Kanuni Ya Thelathini Ya Kujenga Mafanikio ya Kudumu: JIFUNZE KUWA NA SHUKRANI BILA KUACHA KUTAMANI ZAIDI
π₯ AUGUST 30 Kuna watu wanaishi wakisubiri siku ambayo watakuwa na kila kitu ndipo waanze kufurahia maisha. "Nikifanikiwa zaidi nitakuwa na furaha." "Nikijenga nyumba nitakuwa na amani." "Nikifikisha kiwango fulani cha fedha ndipo nitashukuru." Lakini kuna tatizo: π Ukimzoesha moyo wako kwamba furaha ipo kwenye kitu ambacho bado hujakipata, utatumia maisha yako yote ukisubiri. Ndiyo …