Watu wengi wamekuwa hawayafurahii maisha yao kwa sababu wamekuwa wanaahirisha kuishi. Kwa mfano, mpaka nikiwa na nyumba au nikiwa na gari ndiyo nitaanza kuishi na kuwa na maisha ya furaha. Wanasubiri mpaka kila kitu kiwe sawa ndiyo wafanye yale wanayotaka kufanya. Unapaswa kujua maisha hayakusubiri wewe uwe tayari, bali yanaendelea kwenda. Hivyo wajibu wako ni …
Category Archives: MAKALA ZA MAISHA
Ni Kipi Kikubwa Kinachoweza Kukushinda?
Kuna hadithi moja mwandishi Robin Sharma anasimulia katika kitabu chake cha The everyday Hero Manifesto. Robin Sharma anatushirikisha mgonjwa aliyeandika kitabu kwa njia ya kukonyeza. Unaweza kushangaa imewezekanaje, lakini tayari imeshawezekana na rekodi imeshawezekana. Robin Sharma anatushirikisha hadithi ya Jean -Dominique Bauby ambaye alikuwa na maisha mazuri na ya mafanikio. Siku moja akapatwa na kiharusi …
Kama Mtu Akiwa Anataka Kitu
Huwa anafanya na anakipata. Ikiwa mtu hataki kitu, hawezi kukuambia ukweli bali atakuonesha sababu ambazo ukizichunguza vizuri unakuta siyo za kweli ila anakupa sababu kwa sababu anaogopa kukuambia ukweli na akikuambia ukweli utajisikia vibaya. Mtu ambaye anataka kitu utaona nia yake ya kweli hata kama amewekewa vipingamizi. kwa mfano, watu watano waliitwa katika usaili, watatu …
Nyumba Usiyolala Hujui Hila Yake
Ukiwa nyumbani kwako ukiziangalia nyasi za jirani yako kwa mbali unaona za kijani kweli, unavutiwa nazo na kuziona za kwako siyo za kijani kama za jirani yako, ila ukizisogelea karibu unaona siyo za kijani kama ulivyoziona na ukiziangalia za kwako wakati uko kwa jirani unaona tena nyasi zako ni nzuri. Hapa tunapata somo gani? Tunapata …
Una Maoni Kila Mahali Lakini Huna Maoni Juu Yako
Unatoa maoni kwenye michezo mbalimbali inayoendelea duniani. Unatoa maoni kwenye maisha ya watu wanavyoishi. Unatoa maoni kwenye siasa na nchi kwa ujumla inavyoenda. Kifupi unatoa maoni kila mahali lakini hutoi maoni kwenye maisha yako binafsi. Ukiacha kutoa maoni kwenye kila kitu na kutunza muda huo kwenye kufanya kazi, na kujitathimini binafsi, kwa nini uko hivyo …
Continue reading “Una Maoni Kila Mahali Lakini Huna Maoni Juu Yako”
Sababu Mbili Za Mafanikio
Kuna sababu mbili za kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yako. Ukiweza kuzifuata lazima utafanikiwa ni suala la muda tu. Sababu ya kwanza, jua gharama ya mafanikio unayotaka.Kama unataka kufanikiwa kitu jua ni gharama kiasi gani unayopaswa kulipa. Sababu ya pili, kuwa tayari kulipia gharama. Baada ya kujua gharama sasa kuwa tayari kulipia gharama hizo. Kila …
Unatakiwa Kufanya Hivi Kama Kitu Hakipo Sawa
Wakati mzuri wa kubadili mambo yaliyoharibika ni kabla hayajaharibika, na unaweza kufanya hivyo kwa kuchukua hatua kwenye mambo madogo ambayo hayana madhara na yanaweza kupuuzwa, lakini baadaye yanatengeneza madhara makubwa. Kwa mfano, huwa tunadharau yale mambo madogo madogo kwenye maisha yetu, lakini baadaye yanakuja kutugharimu. Kama kitu hakipo sahihi, kirekebishe kabla mambo hayajaharibika. Muda mzuri …
Continue reading “Unatakiwa Kufanya Hivi Kama Kitu Hakipo Sawa”
Mafanikio Siyo Kushinda Mara Zote
Somo kubwa ambalo unapaswa kulielewa wakati wote kwenye maisha ni kwamba, mafanikio Siyo kushinda mara zote. Bali matokeo ya USHINDI mkubwa kwenye mambo machache. Unapokuwa unakabiliana na changamoto kwenye kazi, biashara, uwekezaji nk na kushindwa vibaya, siyo kwamba hutafanikiwa bali utafanikiwa. Unachotakiwa kufanya ni wewe kushinda kwenye maeneo machache ambayo uko vizuri na kufidia kwingine. …
Unachopaswa Kujua Ni Hiki
Mtu mmoja aliwahi kunukuliwa akisema, nataka kujua ni wapi nikienda nitakufa, niepuke kwenda sehemu hiyo. Hii ina maana gani kwetu? Hii ina maana kwamba, unatakiwa kujua ni vitu gani ukivifanya vitakupa hasara na uviepuke kuvifanya vitu hivyo. Unatakiwa kujua ni uwekezaji gani ukifanya utakupa faida na uwekezaji gani ukifanya utakupa hasara na uepuke hasara hiyo. …
Maana Ya Kutosheka
Kutosheka haimaanishi kidogo kama wengi wanavyofikiri. Kutosheka ni kufikia hatua ambayo unajua hata ukienda zaidi hakuna mabadiliko makubwa utakayoleta na kwa kuwa kila hatua unayochukua ina hatari hivyo hakuna hatari itakayoweza kukulipa. Kwa mfano, mtu ukishiba maana yake umetosheka na hata ukisema ule zaidi inakuwa ni hatari na sumu. Wengi wakisikia kutosheka wanaona ni kama …