Huwezi ukapanga mambo yako na yakaenda vizuri kila wakati. Kuna wakati mambo yanaenda vizuri na kuna wakati mambo yanaenda ndivyo sivyo. Kuna wakati unaanguka kama binadamu lakini katika msimamo wako ulioamua kufanya usiuvunje mara pili. Dharura huwa zinatokea lakini usikubali iwe kila siku kwa mfano, kuchelewa kufika eneo la kazi, biashara au miadi yoyote ile. …
Category Archives: MAKALA ZA MAISHA
Leo Hakuna Taarifa Ya Habari
Pata picha umejiandaa kusikiliza au kuangalia taarifa ya habari ukiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua dunia inaendaje au nini kimetokea, halafu anakuja mtangazaji wa taarifa ya habari anakuambia zima TV au radio yako nenda kalale leo hakuna habari, je utajisikiaje?Watu wanapenda habari na hata ukiwaambia hakuna habari hawawezi kukuelewa. Na hata habari nyingi unazozisikia …
Watu Wanakuchukuliaje?
Ni rahisi sana, watu wanakuchukulia kwa namna unavyojichukulia wewe. Ukijichukulia mwaminifu na watu watakuchukulia mwaminifu. Na mara nyingi binadamu huwa tunatoa kile ambacho tunacho. Hatuwezi kutoa kile ambacho hatuna. Hata kama kuna mtu anaigiza hali fulani kwenye maisha hawezi kudumu naye hata siku moja. Watu wanakuchukulia jinsi unavyojichukulia wewe mwenyewe. Tuwe makini, sisi ni kioo, …
Kama Ameshindwa Kujihurumia Je, Wewe Utaweza?
Siku zote upendo huwa unaanza na mtu kujipenda kwanza yeye mwenyewe. Kama mtu yeye mwenyewe hajipendi unafikiri wewe ndiyo utaweza kufanya hivyo? Kama mtu hajihurumii yeye mwenyewe, je, wewe utaweza kumhurumia? Kwenye maisha huwezi kumzuia mtu anayetaka kujiua, mtu kama ameamua kujiua atajiua hata ufanye nini. Hii ina maana kwamba, nguvu ya ndani ya mtu …
Continue reading “Kama Ameshindwa Kujihurumia Je, Wewe Utaweza?”
Usiwe Na Wasiwasi
Akili huwa haifanyi kazi pale hisia zinapokuwa juu na fikra zinapokuwa chini. Fikra zinapokuwa chini, mtu anakuwa anafanya maamuzi ya ajabu na baadaye kuja kujutia. Ndiyo maana, haishauriwi kabisa kufanya maamuzi ukiwa na hisia. Jicheleweshe kufanya maamuzi mpaka pale hisia zinapokuwa chini au zimeisha. Ukiwa na changamoto yoyote ile wala usiwe na wasiwasi, tulia kwani …
Ondoka Kwenye Vikundi Hasi
Ni kawaida yetu sisi binadamu kupenda kuonekana kuwa ndani ya kundi fulani. Tunapokuwa ndani ya kundi huwa tunajisikia vizuri, pale tusipokuwa ndani ya kundi huwa tunaona kama vile tumepotea. Swali muhimu la kujiuliza uko kwenye kundi gani? Kama uko kwenye kundi lolote ambalo halina manufaa kwako, ni kundi hasi badala ya kujadili mambo chanya yanayojenga, …
Changamoto Moja Kwenye Kujifunza
Aliyekuwa baba wa falsafa Mwanafalsafa Socrates aliwahi kunukuliwa akisema hekima pekee ambayo ninayo, ni kwamba sijui kitu. Wakati huo Mwanafalsafa Socrates ndiyo mtu ambaye alikuwa anaonekana anajua sana lakini watu wakimuuliza anasema anachojua ni kwamba hajui kitu. Hii ina maana gani kwetu? Ni kujishusha na kuwa mnyenyekevu na kuwa tayari kutaka kujifunza tena. Sina uhakika …
Kwa Sababu Ya Tabia
Vitu vyote watu ambavyo huwa unaona watu wakifanya jua ni tabia. Hakuna mtu ambaye anaweza kufanya kitu ambacho ni nje ya tabia yake. Huwezi kumkuta mtu anaamka asubuhi na mapema kama siyo tabia yake, na hata akiamka mapema anaenda kufanya nini huo muda kama hana malengo makubwa? Kama mtu siyo tabia yake hawezi kufanya, kwa …
Usiweke Matumaini Kwenye Kitu Hiki
Usiweke matumaini yako kwenye kitu hewa. Usiweke matumaini kwa kitu chochote ambacho hujakifanyia kazi kwani hayo ni matumaini hewa tu. Mtu akishakuonesha dalilli nyekundu kwenye kitu chochote kile, usiweke matumaini yako kwake badala yake msaidie kufanya maamuzi kupitia kile anachotaka kutokana na dalilli nyekundu alizokuonesha.Watu wengine wanakuonesha kabisa dalilli nyekundu kwamba hataki kitu fulani lakini …
Kuwa Na Chujio
Kwa dunia unayoishi sasa, mambo ambayo yanateka umakini yako ni mengi sana ukilinganisha na faida unazopata. Unatekwa umakini wako, tokea unaamka mpaka unaenda kulala. Lazima uchuje watu unaojijusisha nao kila siku, siyo kila mtu ni wa kumpa muda wako. Siyo kila mtandao wa kijamii unapaswa kuwepo. Siyo kila habari inayotoka unapaswa kuijua, ukitaka kuwa mtu …