Chochea Moto Huu Ili Uendelee Kuwaka

Unapaswa kuchochea moto wa hamasa uliopo ndani yako. Hamasa ni kama moto, usipouchochea huwa unazima. Ili moto uendelee kuwaka ,lazima uchochewe, kuwepo na nishati na hewa ya oksijeni. Vile vile kwenye hamasa, unaweza kuhamasika mara moja, lakini kadiri muda unavyokwenda hamasa hiyo inapungua. Unapaswa kuchochea hamasa yakko kila siku. Unapaswa kujikumbusha kule unakoenda na jinsi …

Usimpe Mtu Ahadi Ya Kuendelea Kutegemea Wakati Huna Uhakika Wa Kumpatia

Kwenye jamii zetu watu wamekuwa ni mabingwa wa kutoa ahadi na inafikia mahali ahadi zinawafunga watu na hata kukosa raha kwa sababu kila akiangalia amezungukwa na ahadi nyingi alizoamua kuahidi kwa hisia. Maisha ni yako na una uamuzi wa kutoa pale unapojisikia kutoa na siyo lazima. Usijifunge na ahadi, kama kitu huna uwezo nacho kutoa …

Usiwe Kopo Linaloelea Juu Ya Maji Likiwa Limefungwa

Ukichukua kopo la maji au chupa ya maji halafu ukaifunga na kuitupia kwenye mto, bahari, au ukaiweka bombani ikiwa imefungwa kamwe maji hayawezi kuingia ndani. Hii ina maana gani katika maisha yetu ya kawaida? Watu wengi huenda wanafanya kile wanachopaswa kufanya lakini hawapati matokeo mazuri yanayofanana na juhudi wanazoweka. Yaani wako kwenye maji lakini hawayafaidi …

Kama Unataka Kuuza Chochote Kile, Tafuta Kundi Hili

Kama unavyojua, maisha ni mauzo, lazima uuze kitu fulani ili upate fedha. Bila kuuza, ni wazi hakuna kipato utakachoingiza. Ili uweze kuuza chochote kile, unapaswa kutafuta kundi lenye njaa kali, kisha unawauzia kundi hilo chakula au kile wanachotaka ili kushibisha njaa yao. Nadhani unapata picha, mtu akiwa na njaa hasa, atanunua chakula kwa namna yoyote …

Njia Yenye Ushawishi Kwenye Kila Eneo La Maisha

Siyo njia nyingine bali ni nkia ya kuuliza maswali. Njia ya kuuliza maswali ina ushawishi kwenye biashara, kazi, huduma nk. Ukitaka kuwashawishi watu na kukubaliana na wewe, tumia njia ya maswali na siyo maelezo. Mara nyingi binadamu hapendi kuamuliwa, bali anapenda kuamua kupitia kuuliza maswali, yanamjengea fikra sahihi na kufanya maamuzi sahihi. Ukiwa katika mauzo …

Hiki Ndiyo Kinaweza Kukutofautisha Na Wengine Kwenye Biashara, Kazi Au Kile Unachofanya

Kinachoweza kukutofautisha na wengine wote ambao mnafanya biashara zinazofanana, kazi au huduma zinazoendana ni utoaji wa huduma bora sana kwa wateja. Kumbuka yoyote yule unayempatia huduma ni mteja wako. Jihoji tu, kuanzia kwenye biashara, kazi, mahusiano je, huduma ninayotoa hii kwa mteja wangu anaweza kuipata sehemu nyingine? Kama anaweza kuipata je, mimi natoaje huduma bora …

Usiwe Na Wasiwasi Na Kitu Hiki Hapa

Kabla hatujafanya kitu chochote kile, ndani ya nafsi zetu huwa kuna sauti tunazisikia. Wakati mwingine nafsi zetu zinatuambia hapa tunaweza au hatuwezi. Kinachowazuia wengi kufanikiwa ni kuwa na wasiwasi juu ya nafsi zao wenyewe.Mtu anataka ushindi wa kitu fulani, lakini hajiamini kabisa kama atashinda, kimdomo anasema anataka kitu fulani lakini nafsi haimaanishi. Kwa sababu walijaribu …

Usitawanye Nguvu Zako

Rafiki, jihusishe na kitu kimoja pekee na komaa na kitu hicho mpaka utakapofanikiwa au pale uzoefu wako unapokuonesha kwamba ni wakati wa kuachana nacho. Kwa mfano, kugonga nyundo kwenye msumari mmoja kwa kurudia rudia kunafanya msumari huo uingie ndani. Pale ambapo umakini wa mtu unawekwa kwenye kitu kimoja, akili yake inakuwa inamletea njia za kuboresha …

Kitu Pekee Kitakachokuwezesha Kuendelea Mbele

Kuna wakati unachoka na unaona ni sahihi kwako kuishia hapo ulipofika. Safari  ya  kupata  kile  unachotaka  kwenye  maisha  yako  haitakuwa  rahisi,  dunia haitakuachia  kirahisi ufanye  kila  unachotaka.  Utakutana  na  vikwazo,  changamoto  na magumu mbalimbali.  Kuna  wakati utajiona  kama  umekosea  kila  ulichokuwa  unafanya. Utafikia  hatua  ya  kukata  tamaa  na  kuona  haina  haja  ya  kuendelea  tena. Kitu  …

Mpe Mteja Uhakika Huu Hapa

Kwenye biashara au huduma yoyote ile unayotoa, unatakiwa kumpatia mteja  uhakika  wa  kile  unachomuuzia. Mfanye  ajisikie  kwamba  amepata suluhisho  na  siyo  kupoteza  fedha  zake. Siku  zote kutoa  fedha  kunauma,  kwa sababu  unapotoa  fedha  na  kulipia  kitu,  maana  yake  huna  tena  fedha  hizo  kwa matumizi  mengine.  Jua  mteja  wako  ana  matumizi  mengine  ya  fedha  zake, hivyo  …

Design a site like this with WordPress.com
Get started