Kabla mteja hajanunua kitu kwako anachotaka ni kupata uhakika juu ya kile unachouza kwanza. Sasa wauzaji wengi huwa hawawapi wateja uhakika. Hata mgonjwa akiwa anaumwa akimuuliza daktari je, nitapona na daktari akimpa matumaini ndiyo utapona mgonjwa anakuwa na matumaini lakini akimwambia huponi atampoteza. Na unaweza kumpoteza mteja kama hujampa uhakika wa kile unachouza. Ukimwambia hakifanyi …
Haya Ndiyo Maisha Ambayo Hayana Maana Kuishi
Ni maisha ambayo hayatathiminiwi. Mwanafalsafa Socrates aliwahi kunukuliwa akisema, maisha ambayo hayatathiminiwi, hayana maana kuishi. Watu wengi hawajifanyii tathimini kwenye kile wanachofanya ndiyo maana hawaoni matokeo mazuri, hawajui kama wanaenda mbele au wanarudi nyuma. Fanyia tathmini kazi yako. Jiulize kazi unayofanya inakulipa? Na itakufikisha kweli kule unakotaka kufika?Kazi unayofanya inasaidia jamii au ina haribu maisha …
Continue reading "Haya Ndiyo Maisha Ambayo Hayana Maana Kuishi"
Jinsi Ya Kula Mema Ya Nchi
Kila mtu amepewa kibali cha kula mema ya nchi. Kila mtu amebarikiwa kwenye maisha yake. Unachopaswa kujua ni kwamba, baraka huwa haziji tu kwako bila kufanya kitu. Baraka huwa zinakuja kwako kwa kufanya kitu. Ukifanya kitu na utaona baraka zinakuja. Baraka haziji kwa kuweka mikono mifukoni, bali baraka zinakuja kwa kufanya kitu. Ili uweze kuchota …
Biashara Mpya Ambayo Haijawahi Kufanywa Na Mtu Yeyote Yule Na Ina Fursa Nyingi Kweli
Kifupi tu rafiki yangu, hakuna biashara mpya ambayo haijawahi kufanywa. Biashara ni zile zile lakini tatizo liko kwenye utoaji wa huduma. Unaweza ukafanya biashara yako kuwa mpya kwa kuifanya ya kipekee sana kuliko nyingine zote ambazo tayari zilikuwepo. Usipate shida kutafuta wazo la biashara, unachotakiwa kufanya angalia biashara ambazo ziko mtaani kwako au changamoto ambayo …
Kadiri Unavyoweka Juhudi Za Kuongeza Kipato, Kuwa Makini Na Matumizi Yako
Fedha ikiwepo huwa haikosi matumizi. Unapokuwa na fedha mara nyingi inatafuta matumizi na sasa usipokuwa makini utajikuta huna unachofanya. Lazima uwe mjanja, kwani kuna kawaida ya matumizi kuongezeka pale kipato chako kinapoongezeka. Ukitaka uione hela, ongeza kipato chako na punguza matumizi yasiyokuwa na ulazima. Usipokuwa makini na matumizi, utashangaa mwanzoni ulikuwa na kipato kidogo na …
Continue reading "Kadiri Unavyoweka Juhudi Za Kuongeza Kipato, Kuwa Makini Na Matumizi Yako"
Bila Ya Kuwa Na Kitu Hiki Huwezi Kufanikiwa Kwenye Maisha
Katika safari ya mafanikio ya kuyafikia mafanikio makubwa inahitaji mtu mwenye sifa kuu mbili, kwanza mtu ambaye anajituma na kujiongoza. Bila ya kuwa mtu wa kujituma wewe mwenyewe, ni vigumu kufanikiwa kwenye maisha. Wapo watu ambao wanasubiri kuambiwa cha kufanya, bila kuambiwa hawajisumbui kabisa kifupi wanakosa nidhamu binafsi. Lakini wale wanaofanikiwa sana huwa hawasubiri kuambiwa …
Continue reading "Bila Ya Kuwa Na Kitu Hiki Huwezi Kufanikiwa Kwenye Maisha"
Tengeneza Maoni Yatakayokupa Hamasa Binafsi
Yapo maoni mengi ambayo huwa tunajitengenezea kwenye fikra zetu. Yapo maoni ambayo tunajipa sisi wenyewe na yapo maoni ambayo yanajitengenezea kwenye fikra zetu. Wako ambao wanajipa maoni chanya na wako ambao wanajipa maoni hasi. Maoni yanayotengenezwa kwenye fikra zetu yana mchango mkubwa sana kwenye mafanikio yetu kimaisha. Kujitengenezea maoni ni hamasa binafsi. Vile unavyofikiri upo …
Continue reading "Tengeneza Maoni Yatakayokupa Hamasa Binafsi"
Kama Unataka Kuwa Muuzaji Mzuri, Kuwa Na Tabia Hizi Mbili
Kiasili, kila mtu ni muuzaji.Kila mtu anauza kila wakati, haijalishi wewe ni nani, kila unapokutana na mtu mwingine, unapoelezea wazo lako, unapotoa maoni yako, unauza kitu muhimu sana, ambacho ni wewe mwenyewe. Kitendo tu cha kuweza kumshawishi mtu na akubaliana na wewe hapo unakuwa muuzaji. Kwa sababu umeuza mawazo yako kwa wengine. Kama unatafuta kazi …
Continue reading "Kama Unataka Kuwa Muuzaji Mzuri, Kuwa Na Tabia Hizi Mbili"
Adhabu Zinawasaidia Watoto Kuelewa Uhalisia Wa Dunia
Wazazi wa siku hizi wanawalea watoto utafikiri wamepata mkataba wa kuishi nao milele. Wazazi hawataki kuwafundisha watoto kukosa. Mtoto akitaka kile anachotaka anapewa mara moja. Hii inamfanya mtoto kuja kuteseka baadaye anapokuja kuingia kwenye uhalisia wa mambo. Watoto wanaharibiwa kwa kukosa adhabu kuliko kuharibiwa na adhabu. Kumekuwa na harakati nyingi za kufuta adhabu kwa watoto …
Continue reading "Adhabu Zinawasaidia Watoto Kuelewa Uhalisia Wa Dunia"
Usiende Mahali Ukiwa Fedha Hii Tu
Kwenye maisha lolote linaweza kutokea. Na maisha ni safari huwezi kujua nini kitatokea katika ya safari. Hivyo basi, unapoishi lazima uishi kwa tahadhari kwamba ujiandae kukabiliana na lolote lile litakalojitokeza. Kwenye fedha, ninao ushauri mzuri ambao napenda kukuambia leo rafiki yangu. Ushauri huu nilijifunza kutoka kwa mwandishi Grant Cardone ambaye ni mwandishi wa mambo ya …