Vitu Viwili Vitakavyokufikisha Kwenye Utajiri

Natumaini kama unasoma hapa, huna lengo la kuwa masikini. Bali lengo lako kuu ni kuwa tajiri. Tunapaswa kuungana wote duniani kupambana na adui ambaye anatesa watu ambaye ni umasikini. Umasikini ni laana, tupambane usiku na mchana kumtokomeza adui huyu ambaye kwa sasa ameshaota mizizi. Na umasikini wa watu wengi hauko mfukoni bali uko kwenye akili. …

Kwenye Kila Mauzo Angalia Hiki

Angalia faida. Kwenye mauzo yoyote yale unayofanya angalia faida. Faida ndiyo kila kitu kwenye biashara, usifanye biashara kwa hasara kwa sababu hasara haitakusaidia kulipa bili wala kuendesha biashara yako. Unapofanya mauzo, kitu cha kwanza kufanya ni kuchukua mauzo kutoa gharama za mauzo. Kile kinachobakia sasa ndiyo faida yako halisi. Na ili upate faida nzuri, hakikisha …

Kero Unayoipata Kwenye Biashara Ya Wengine

Itumie kero hiyo kuboresha biashara yako na kuwa bora. Huwa tunajifunza vitu vingi sana kwenye biashara za wenzetu pale tunapoenda kupata huduma fulani. Kuna wakati unakutana na vitu vizuri na unajiambia kabisa hiki nitaenda kukitumia kwenye kazi au biashara yangu. Na kuna wakati unaenda kupata huduma kwenye biashara nyingine unakutana na huduma mbovu kiasi kwamba …

Kitu Kinachomfanya Mtu Achukue Hatua Haraka

Huwa tunalalamika kwanini watu wengine tukiwaambia wafanye kitu fulani hawachukui hatua.Siyo tu watu wengine, wakati mwingine hata sisi wenyewe tunakuwa ni wagumu kuchukua hatua. Unafikiri ni kwanini watu wanakuwa wagumu kuchukua hatua? Kwa sababu hujagusa maslahi yao binafsi. Kitu kinachomsukuma mtu kuchukua hatua haraka ni maslahi. Mtu anakuwa ana hamasika kuchukua hatua pale anapokuwa anaona …

Usisome Kumaliza, Soma Kujifunza

Watu wengi huwa wanasoma kama kasuku, wanakimbilia kusoma ili wamalize vitabu vingi. Wengine watajitamba kwamba, wamesoma vitabu kadhaa ndani ya muda fulani. Kujitamba bila matokeo hakuna maana yoyote ya kusoma vitabu. Unapokuwa mtu wa kusoma, tunataka kuona matokeo mazuri na siyo kumuona mtu yule yule kila siku. Maisha ya kusoma vitabu yakubadilishe kweli, uishi yale …

Kwanini Ni Muhimu Kila Mfanyabiashara Kuijua Biashara Yake Kwa Undani?

Ni muhimu sana kila mfanyabiashara kuijua biashara kwa undani, Kwanini? Ili kuweza kumsaidia kufanya maamuzi sahihi kila wakati. Kuendesha biashara ni sayansi na sanaa. Na kwenye sayansi kuna vitu vina kanuni na kwenye sanaa hakuna kanuni ni kufanya maamuzi kulingana na hali jinsi inavyokwenda. Usipoijua vizuri biashara yako, ni rahisi sana kuipoteza. Ijue biashara yako …

Jinsi Ya Kutengeneza Deni Ili Ulipwe

Kwenye maisha lazima utengeneze madeni mengi kwa watu wengine ili ulipwe. Unatengenezaje sasa madeni hayo? Ni kwa njia ya utoaji. Utoaji huwa unatengeneza deni ambapo upande uliopokea huwa unasukumwa kulilipa kwa namna yoyote ile. Kwa mfano, mtu akikusaidia kitu, utatafuta namna yoyote ile ya kurudisha fadhila kwa sababu amekusaidia. Ndivyo binadamu walivyo, ukimpa kitu anatafuta …

Kitu Pekee Ambacho Huwezi Kukopa Hapa Duniani

Tumeshazoea kukopa, wengine kukopa imeshakuwa ni tabia, mtu asipokopa anakuwa anajiona kama vile hajakamilika. Pale mtu anapokuwa hana fedha anaweza kukosa kwa mtu wake wa karibu na akamsaidia lakini kuna kitu ambacho wote hapa duniani hatuwezi kukopa. Kitu chenyewe ambacho hatuwezi kukopa ni muda.Huwezi kukopa masaa 24 yajayo uyatumie kwa mambo yako leo na utakuja …

Ukishakuwa Na Sababu Hii, Hakuna Kitakachokushinda

Mwanafalsafa Friedrich Nietzsche aliwahi kunukuliwa akisema,Yeyote mwenye sababu ya kuishi, anaweza kupambana na chochote. Kumbe basi, ukishakuwa na sababu ya kuishi, hakuna kinachoweza kukushinda. Ukishajua kile unachotaka na ukiwa na kwanini kubwa ndani yako utaweza kupambana na chochote kile. Wakati mwingine unakutana na mateso kwenye safari ya mafanikio, ukiangalia mapito unayopitia kama huna kwanini kubwa …

Ng’ombe Anapokuwa Muhimu Kuliko Wewe

Watu wengi hujitoa sana pale wanapowasaidia wengine, lakini inapokuja kwao binafsi wanapuuza. Kwa mfano, mifugo ambayo mtu anaifuga ikiumwa haraka hutafutiwa matibabu na kuhakikisha inapata matibabu, lakini wewe mwenyewe ukiumwa huhangaiki sana na hata ukipewa dawa hutumii kwa ukamini kama unavyoelekezwa lakini kama ni mtu mwingine au mifugo unahakikisha inamaliza dozi. Watu wanapoumwa wakiandikiwa dawa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started