Unamdanganya Nani?

Maisha kiuhalisia hayadanganyi ila wewe mwenyewe ndiyo unajidanganya. Maisha ni maigizo lakini kuigiza kitu ambacho siyo sahihi siyo sawa. Kuwa na maisha yenye uadilifu, chochote unachofanya fanya kwa uaminifu na uadilifu. Maisha yako yasiwe na makando makando mengi maana yanakuchosha kuigiza. Nilishawahi kuandika kwamba, maisha ya kuigiza una hela halafu huna hela yana gharama sana. …

Sifa Inayolipa Sana Duniani

Mwandishi mmoja wa kitabu cha How I Raised Myself From Failures to Success in Selling alikuwa ni mchezaji wa kikapu, alikuwa anachezea timu moja huko Marekani. Siku moja kocha wake wa timu ya kikapu akamwita, akamwambia tumeamua kukufukuza katika timu yetu ya kikapu. Frank akauliza, ni kwa sababu gani mmeamua kunifukuza kazi? Kocha wake akamjibu …

Mambo Yasiyokuwa Na Tija Yananasa Umakini Wako

Kwenye maisha kuna drama nyingi sana, unaweza kupanga mipango yako lakini usiitimize lakini mambo ya kijinga ambayo hujayapangia ratiba yanachukua umakini wako. Mambo yasiyokuwa na tija, yananasa umakini wako kuliko maelezo. Utaweza kusema huna muda wa kufanya mambo muhimu lakini mambo yasiyokuwa na tija yakanasa umakini wako. Tumezungukwa na mambo mengi yasiyokuwa na tija, ambayo …

Ifahamu Siri Muhimu Kuliko Zote Kwenye Mauzo

Biashara zote ambazo hazifanyi vizuri tatizo lake moja linakuwa kwenye mauzo. Kama biashara haina mauzo mazuri maana yake haina maisha. Mauzo ndiyo kila kitu kwenye biashara, yaani pumzi kwenye biashara. Mauzo yanapokuwa vizuri, biashara inakuwa vizuri maana itapata fedha ya kujiendesha. Kwenye kitabu cha How I Raised Myself From Failures to Success in Selling, mwandishi …

Wako Watu Wa Aina Mbili, Je wewe Upo Aina Gani Kati Ya Hawa

Kuna watu aina mbili hapa duniani. Wapo watu ambao wanayakubali majukumu yao na kuchukua hatua. Na wapo watu ambao wanayakataa kabisa majukumu yao na kutafuta sababu kwa nini hawawezi kuchukua hatua. Kifupi rafiki yangu, mafanikio hayajawahi kwenda kwa mtu yeyote ambaye siyo wa kukubali majukumu. Mafanikio yanawapenda wale wanaokubali majukumu na kuchukua hatua na siyo …

Njia Pekee Ya Kufanikiwa Kwenye Maisha

Ni mtu kutumia kile ambacho kipo ndani yake, kukifanyia kazi na kuweza kutoa matokeo mazuri. Kila mtu ana kitu ambacho kipo ndani yake, kitu ambacho ni tofauti kabisa na watu wengine. Lakini, wengi wamekuwa hawafanyii kazi kilichopo ndani, ila wanakimbizana na vitu vya nje. Huwezi kufanikiwa kwenye kitu chochote kile kama umeshindwa kutumia vizuri kile …

Sababu Mbili Zinazowapelekea Watu Kununua

Kwanza unapaswa kujua kwamba watu hawanunui kwa sababu ya bei. Watu wananunua kwa sababu ya thamani na mapenzi. Usijidanganye kwamba watu wananunua kwa sababu ya bei kuwa chini. Kwenye mauzo watu wamekuwa wanajidanganya kwamba sababu za watu kutokununua ni kwa sababu hawana fedha au kitu ni bei ghali. Hivyo wengi hukimbilia kupunguza bei wakiamini ndiyo …

Watu ni Wazuri Sana Kwenye Kitu Hiki

Watu ni wazuri sana kwenye sababu. Waulize watu kwanini hawajafanya au kwanini maisha yao yako hivyo walivyo watakupa sababu. Ukiwapa watu majukumu fulani usipowapa namba ya kuifikia lazima watakupa sababu. Na nimekuja kugundua sababu hizi tunazojipa ni sababu za uvivu na uzembe. Yaani sababu ndiyo imekuwa kificho cha watu wengi ambao hawataki kuchukua hatua kwenye …

Dhambi Kuu Tatu Zinazowakwamisha Watu Wengi Kwenye Mafanikio Yoyote Yale

Hakuna ambaye hajui anatakiwa kufanya nini kwenye maisha yake. Kama kila mtu anajua kile anachotakiwa kufanya unafikiri kitu gani ambacho kinawakwamisha watu? Utajisikiaje leo unakwenda kuvijua vitu hivyo na kuchukua hatua? Watu wanakwamisha na dhambi hizi ambazo nakusihi sana rafiki yangu uzikatae kwa kila namna. Moja ni uzembe. Uzembe ni kufanya mambo kimazoea.Kufanya vitu kwa …

Ukitaka Kuuza Sana Gusa Hisia Hizi Za Mteja Wako

Watu huwa wanaongozwa na hisia kuu mbili.Moja hisia ya kupata na mbili ni hisia ya kupoteza. Ukitaka kuuza, hakikisha unagusa hisia za wateja wako. Hisia kama za maumivu, kupoteza, matumaini, hofu nk. Unapaswa kujua kwamba, watu hawafanyi manunuzi kwa njia ya fikra bali hisia. Unagusa hisia za wateja wako pale biashara yako inapokuwa halisi na …

Design a site like this with WordPress.com
Get started