Maeneo Mawili Ambayo Kazi Yenye Nguvu Hugusa

Kazi yenye nguvu hugusa pande mbili kubwa. Pale unapofanya kazi yoyote yenye nguvu, inayoleta mapinduzi makubwa, utagusa pande kuu mbili.Upande wa kwanza ni wale watakaokupenda sana kwa sababu umekuwa mkombozi wao kupitia kazi yako. Na upande wa pili ni wale watakaokuchukia sana kwa sababu umevuruga mazoea waliyokuwa nayo. Ili upendwe na baadhi, lazima pia uchukiwe …

Chochote Ambacho Hakipimwi

Huwa hakikui. Watoto wadogo huwa wana kliniki wanapima uzito na maendeleo mengine ya ukuaji. Wanafanya hivyo ili kujua maendeleo ya watoto kwa sababu bila KUPIMA huwezi kujua kama kitu kinakua au hakikui. Hii ina maana gani kwetu? Unatakiwa kujifanyia tathmini kila siku, kila wiki na mwezi ili ujue maendeleo yako. Kila unachofanya hakikisha unakipima, usiendelee …

Huwezi Kumzuia Mtu Anayetaka Kujiua Njia rahisi ya kuishi muda mrefu ni kuwa mwangalifu kwenye kila eneo la maisha yako. Lakini, kuna watu wanachagua kujiua wao wenyewe. Unaweza kupambana kuwasaidia lakini wao hawasikii, hivyo unamwacha afe. Iko hivi, kwenye maisha unajua kabisa kuna vitu ukifanya vinakupelekea kifo, na iko wazi kabisa lakini watu wengine hata …

Kabla Hujaendelea Na Safari

Pata picha umeenda stendi na kupanda gari halafu unamuuliza swali dereva, hii gari inaenda wapi?Dereva anakujibu sijui hata inaenda wapi. Hatua ya kwanza utakayochukua kabla ya mengine ni kushuka kwanza ili usije ukapotea zaidi. Hii ina maana gani? Kama bado hujajua kule unakokwenda ni bora usiendelee na safari. Kwa sababu utaendelea kupotea zaidi. Usiongeze mwendo …

Njia Ya Kivivu Kupata Wateja

Biashara yoyote ambayo haina wateja ina hatari ya kuanguka.Kwa sababu wateja ndiyo wanaoleta fedha kwenye biashara na fedha ndiyo damu ya biashara, pata picha wewe kama binadamu mwili wako hauna damu moyo unaweza kufanya kazi? Unapata majibu kwamba mauzo ndiyo moyo wa biashara. Hivyo, kwa chochote unachofanya kwenye biashara jiulize kinachangiaje kuongeza MAUZO?Ziko nyingi za …

Mchukulie Kila Mtu Kwa Heshima

Mchukulie kila mtu kwa heshima kwa sababu huwezi kujua ni wakati gani utamwitaji sana kwenye maisha yako. Huna haja ya kumdharau au kumchukulia mtu yeyote yule vibaya, kwa kufanya hivyo ni kujiwekea vikwazo visivyokuwa na umuhimu. Mchukulie kila mtu unayekutana naye kwa adabu, heshima na uaminifu. Siyo tu ni kitu sahihi kufanya hivyo, bali ndiyo …

Ombeni Nanyi Mtapewa

Ni kauli ya Mungu kwa watu wake wote wanaotafuta kile wanachotaka. Mungu amesema ombeni nanyi mtapewa lakini cha kushangaza watu hao wanakwenda kinyume na kauli ya Mungu. Watu hawaombi, kama ukiomba lazima dunia itakupa. Kama huombi usitegemee kama dunia itakupa kile unachotaka kwenye maisha yako. Kama wewe ni muuzaji wa kitu, waombe watu wanunue, waombe …

Usiweke Malengo Haya Kamwe

Malengo ambayo unajua unaweza kuyafikia. Usiwe na malengo ya kimasikini, kuwa na malengo ya kitajiri. Masikini anaweka malengo ambayo anaweza kuyafikia na tajiri anaweka malengo ambayo hawezi kuyafikia. Kwa mfano, tajiri anaweka malengo makubwa ambayo yatamsukuma zaidi kufika mbali hata asipoyafikia malengo yake makubwa basi hata akifikia nusu yake inakuwa ni faida. Usiweka malengo ambayo …

Fanya Kazi Na Upumzike

Ni kweli kabisa kazi ndiyo rafiki wa kweli. Na ninasisitiza watu wafanye kazi kwa sababu kupitia kazi watapata kile wanachotaka. Hata Mungu katika uumbaji wa dunia, aliweza kufanya kazi na kupumzika. Jitahidi sana uweze kupumzika baada ya kufanya kazi wiki nzima.Usipopumzika unatafuta kupata uchoshi ambao utakulazimisha uumwe kwa lazima. Mwili nao unahitaji kupumzika ili uweze …

Ujumbe Muhimu Kwako Kutoka Kwa Elbert Hubbard

Juzi nilipokea zawadi kutoka kwa rafiki yangu Kocha Dr Makirita Amani, ni zawadi ya kijitabu kidogo ambacho amechambua ujumbe wa insha kutoka Garcia, ujumbe kwenda kwa Garcia yaani A message to Garcia. Naomba ninukuu kama ilivyo kutoka kwa Elbert Hubbard. Kama unamfanyia mtu kazi, mfanyie kazi kweli. Kama anakulipa mshahara unaoweza kukupatia mkate na siagi …

Design a site like this with WordPress.com
Get started