Ni kweli kabisa kazi ndiyo rafiki wa kweli. Na ninasisitiza watu wafanye kazi kwa sababu kupitia kazi watapata kile wanachotaka.
Hata Mungu katika uumbaji wa dunia, aliweza kufanya kazi na kupumzika. Jitahidi sana uweze kupumzika baada ya kufanya kazi wiki nzima.
Usipopumzika unatafuta kupata uchoshi ambao utakulazimisha uumwe kwa lazima.
Mwili nao unahitaji kupumzika ili uweze kupata nguvu za kuendelea kujisukuma kufanya kazi.
Mapumziko ni muhimu sana, kwa sababu bila ya afya imara huwezi kufurahia utajiri au mafanikio yoyote yale.
Unapofanya kazi, fanya kazi kweli hata ukichoka unapumzika kwa sababu ulifanya kazi.
Hatua ya kuchukua leo; Fanya kazi lakini kumbuka kupumzika.
Kila wiki tenga muda wa kujifanyia tathmini lakini pia tenga muda wa kupumzika ili uweze kupata nguvu za kuendelea kufanya kazi.
MUHIMU;
Kama bado hujajiunga na kundi la wasapu la Mimi ni Mshindi jiunge leo kwani kuna maarifa mengi unayakosa ambayo sikushirikishi hapa.
Kujua ni maarifa gani hayo na jinsi ya kujiunga nitumie ujumbe wasapu kwa namba 0717101505. Kupata vitabu vizuri vya kujisomea kwa lugha ya kiswahili wasiliana kwamba namba 0717101505.
Rafiki Na Mwalimu Wako, Afisa Mhamasishaji Mkuu (CIO)Chief Inspiration Officer.
Mwl. Deogratius Kessy
0717101505 au 0767101504
https://kessydeo.home.blog