Mchukulie kila mtu kwa heshima kwa sababu huwezi kujua ni wakati gani utamwitaji sana kwenye maisha yako.
Huna haja ya kumdharau au kumchukulia mtu yeyote yule vibaya, kwa kufanya hivyo ni kujiwekea vikwazo visivyokuwa na umuhimu.
Mchukulie kila mtu unayekutana naye kwa adabu, heshima na uaminifu.
Siyo tu ni kitu sahihi kufanya hivyo, bali ndiyo kitu hekima kufanya hivyo.
Kwa mfano, huwezi kujua nani atakuja kukusaidia, unaweza kumdharau mtu kumbe ndiyo mtu muhimu unayemwitaji akusaidie kwenye kitu jambo fulani.
Hatua ya kuchukua leo; popote unapokuwa na ukakutana na mtu, mchukulie kila mtu kama mtu muhimu sana na unayemwitaji ili kupata unachotaka kutoka kwake.
Kumbuka, mafanikio yoyote yale unayotaka, utayapata kutoka kwa wengine.
MUHIMU;
Kama bado hujajiunga na kundi la wasapu la Mimi ni Mshindi jiunge leo kwani kuna maarifa mengi unayakosa ambayo sikushirikishi hapa.
Kujua ni maarifa gani hayo na jinsi ya kujiunga nitumie ujumbe wasapu kwa namba 0717101505. Kupata vitabu vizuri vya kujisomea kwa lugha ya kiswahili wasiliana kwamba namba 0717101505.
Rafiki Na Mwalimu Wako, Afisa Mhamasishaji Mkuu (CIO)Chief Inspiration Officer.
Mwl. Deogratius Kessy
0717101505 au 0767101504
https://kessydeo.home.blog