Kazi yenye nguvu hugusa pande mbili kubwa. Pale unapofanya kazi yoyote yenye nguvu, inayoleta mapinduzi makubwa, utagusa pande kuu mbili.
Upande wa kwanza ni wale watakaokupenda sana kwa sababu umekuwa mkombozi wao kupitia kazi yako.
Na upande wa pili ni wale watakaokuchukia sana kwa sababu umevuruga mazoea waliyokuwa nayo. Ili upendwe na baadhi, lazima pia uchukiwe na baadhi ya watu.
Kama unataka usichukiwe na mtu yeyote, jua pia hutaweza kupendwa na yeyote. Kama hakuna anayekuchukia maana yake hakuna kazi kubwa na ya kimapinduzi unayofanya, unafanya vitu vya kawaida tu na ambavyo vimezoeleka na kil mtu.
Hatua ya kuchukua leo; fanya kile unachopenda na usiangalie wale ambao wanakuchukia wanasema nini.
Kumbuka, huwezi kumfurahisha kila mtu ni kazi ngumu ambaye hakuna aliyeweza kuifanya.
MUHIMU;
Kama bado hujajiunga na kundi la wasapu la Mimi ni Mshindi jiunge leo kwani kuna maarifa mengi unayakosa ambayo sikushirikishi hapa.
Kujua ni maarifa gani hayo na jinsi ya kujiunga nitumie ujumbe wasapu kwa namba 0717101505. Kupata vitabu vizuri vya kujisomea kwa lugha ya kiswahili wasiliana kwamba namba 0717101505.
Rafiki Na Mwalimu Wako, Afisa Mhamasishaji Mkuu (CIO)Chief Inspiration Officer.
Mwl. Deogratius Kessy
0717101505 au 0767101504
https://kessydeo.home.blog