Hawa Ndiyo Wahanga Wakubwa Katika Familia

Wanapopigana tembo nyasi huumia kama wasemavyo waswahili. Vivyo hivyo katika familia zetu, panapo tokea changamoto katika familia zetu watu wa kwanza kuumia ni watoto. Watoto ndiyo wanakuwa wahanga wakubwa katika familia zao. Changamoto katika familia kama vile baba na mama kugombana, kutengana ni moja ya adhabu kubwa wanayoipata watoto. Wazazi ndiyo walinzi wa watoto. Hivyo …

Jinsi Ubinafsi Unavyovunja Ndoa

Mpendwa rafiki, Hakuna mtu ambaye anaweza kusema kuwa yeye yuko salama kwa kila kitu kwenye mahusiano yake. Mahusiano yetu ya ndoa yanakabiliwa na changamoto mbalimbali, kama tunavyoona changamoto maeneo mengine ya kwenye biashara, kazi na hata ndoa ndivyo ilivyo. Kama unataka ndoa yako iwe bora basi acha kuambatana na watu hasi wanaokwenda kinyume na misingi] …

Sehemu Pekee Ambayo Hutakiwi Kuwekeza Fedha Zako

Rafiki yangu, Katika uwekezaji unatakiwa kwanza kujifunza eneo unalotaka kuwekeza fedha zako. Watu wengi huwa hawawekezi fedha zao sahihi. Wengi wanaangalia wengine wanafanya nini nao wanafanya bila hata ya kujifunza kwa undani nini watakiwa kufanya. Unatakiwa upende fedha zako, pale ambako fedha zako umeziwekeza hakikisha macho yako pale. Ukiwekeza fedha zako bila kuzifuatilia utakuwa umeamua …

Huu Ndiyo Muda Wa Kujitesa

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna kitu chochote unachoweza kupata kwenye hii dunia bila kutoa jasho. Kila kitu kina mateso yake ili uweze kukipata. Mambo hayawezi kutokea kama ajali bali yanahitaji nguvu ili yaweze kutokea. Wote tunajua kuwa itafikia kipindi hatutaweza tena kufanya kazi tena, licha ya kuwa na muda. Kila kitu kina ukomo wake hapa duniani. …

Kama Unajali Wengine Wanasema Nini Kwenye Maisha Yako

Rafiki, Kila mtu ni kiongozi wa maisha yake. Hakuna mtu mwingine anayejua zaidi kuhusu wewe kama wewe. Wewe ndiyo bosi wa maisha yako lakini cha kushangaza wako watu hawajali maisha yao bali wanajali kile wanachosema wengine. Utakua ni mtu wa ajabu pale unapoacha kujali yako na kujali mambo ambayo hayakuhusu. Kama wewe ndiyo mkurugenzi wa …

Jinsi Ya Kuandika Upya Hadithi Ya Maisha Yako

Kila mtu ana uwezo mkubwa sana ndani yake lakini watu wengi hawatumii vizuri uwezo mkubwa walionao. Ni kama vile watu wanavyoenda kununua kompyuta yenye uwezo mkubwa kusikiliza mziki. Hapa tunakuwa tunaua uwezo wa kompyuta kwa sababu ina uwezo mkubwa wa kufanya mambo lakini wewe unaitumia kwa kusikiliza mziki pekee. Ndivyo ilivyo hata sisi katika maisha …

Ifahamu Pumzi Ya Biashara Yako

Rafiki, Biashara ni kama binadamu, inatungwa mimba ( mawazo)inazaliwa ,inakua na hatimaye inakufa. Biashara ina uhai kama vile binadamu alivyo, kitu chochote kikikosa uhai kitakufa. Katika biashara nyingi unazoziona zinakufa ujue zimekosa pumzi. Kitu kikikosa pumzi huwa kinakuwa kinakufa. Leo tutajifunza pumzi ya muhimu katika biashara yako. Pumzi muhimu ya biashara yako ni mzunguko wa …

Sababu Mbili Zitakazokufanya Ushindwe au Ushinde Kwenye Jambo Lolote

Mpendwa Rafiki yangu, Sisi wenyewe huwa tunachangia sana maisha yetu au sisi binafsi kuwa kama tulivyo leo. Kama ni mafanikio makubwa au hali ngumu kwenye maisha yetu sisi ndiyo tumekuwa chanzo namba moja. Hadithi ni nyingi sana kwenye maisha yetu. Kila mtu ana hadithi yake ambaye akikuelezea unaweza kujifunza kitu fulani. Tumepewa uwezo mkubwa na …

Jinsi Ya Kuepuka Kufanya Maamuzi Ya Kuongozwa Na Hisia

Karibu maamuzi mengi wanayofanya watu duniani yanaongozwa na hisia. Watu wengi hawapendi kufikiri kwani kufikiri ni moja ya kazi ngumu duniani. Kama ingekuwa tunafikiri kabla tusingekuwa tunafanya maamuzi ya hisia. Wengi wetu tunaendeshwa na hisia kuliko kuongozwa na akili. Tunanunua kwa hisia na siyo kwamba kwa uhitaji, bali ule msukumo wa hisia unavyofanya mambo ndani …

Jinsi Ya Kumwamasisha Mtoto Wako Ili Aweze Kufaulu Sana Darasani

Rafiki yangu mpendwa, Sisi binadamu huwa tuna vitu viwili ambavyo vinatuhamasisha kuchukua hatua, kitu cha kwanza ambacho kinatuhamasisha kuchukua haraka ni kwa ya kupata furaha au raha na kingine kinachotuhamaisha kuchukua hatua ni kuepuka maumivu. Ziko hamasa za aina mbili zinazofanya kazi vizuri ambazo ukizitumia utaweza kumwamasisha mtoto wako na kufanya vizuri shuleni. Kila mzazi …

Design a site like this with WordPress.com
Get started