Kitu Pekee Duniani Ambacho Hakuna Anayeweza Kukihodhi Au Kukimiliki Hata Awe Nani

Ni kawaida yetu sisi binadamu kupenda kuhodhi au kumiliki vitu mbalimbali, wapo ambao wanamiliki ardhi, nyumba na mali nyingine. Tunayo nguvu ya kumiliki vitu vyote lakini kuna kitu kimoja ambacho sisi binadamu hatuwezi kukimiliki. Aliyekuwa mwanafalsafa wa ustoa Seneca aliwahi kunukuliwa akisema, ‘’ ukweli hauwezi kuhodhiwa, yeyote anayetafuta ukweli ataupata.’’ Rafiki, kitu pekee ambacho hakuna …

Jinsi Ya Kukabiliana Na Mtu Asiyejielewa

Rafiki, Siyo kila mtu unayekutana naye anajielewa na kujitambua. Tunakutana na watu wa aina mbalimbali kuna wengine wana hekima na kuna wengine hawana kabisa hekima wala busara. Kuishi na watu ni kazi sana kwa sababu kila mtu ana mitazamo yake. Ukitaka kuishi vile watu wanavyotaka hapo utakua unaishi maisha ya kuwafurahisha watu ambayo ni kazi …

Jinsi Ya Kuwa Na Utulivu Wa Akili

Mpendwa rafiki yangu, Akili zetu zinapokuwa na amani na utulivu basi zinaweza kufanya kazi vizuri sana. Kama ukiishi bila kuwa na utulivu wa akili itakupelekea kufanya mambo ya ajabu usiyoyategemea. Tukiwa na utulivu wa ndani tutaweza kufanya kazi zetu kwa viwango vya juu sana, hivyo basi ni namna gani unaweza kuwa na utulivu wa akili? …

Haya Ndiyo Maandilizi Muhimu Unayopaswa Kuwa Kwenye Maisha Yako

Maisha ni maandalizi. Hivyo unatakiwa kujiandaa na maandalizi kwenye kila eneo la maisha yako. Isifikie mahali sasa ukaridhika na kile ulichonacho. Dunia siyo mti au jiwe kwamba halikui wala halisogei bali dunia inakuwa na kubadilika kila siku. Mambo yanabadilika kila kukicha, kama matumizi ya kifedha yanapanda na wewe unatakiwa kubadilika kuongeza kipato. Hutakiwi kukaa chini …

Huu Ndiyo Uhai Wa Kila Biashara

Rafiki, Kama unafanya biashara basi kuna eneo moja ambalo unatakiwa kulifanyia kazi kila siku ya maisha yako. Kila mtu ni mfanyabiashara kiasili kwa sababu biashara ni mfumo wa kubadilishana thamani, kama umeajiriwa kuna kitu una uza ambacho ndicho ujuzi wako. Kwa namna yoyote ile sisi wote ni wauzaji wa kitu fulani. Uhai wa biashara uko …

Huu Ndiyo Mfumo Mzuri Wa Mafanikio Wa Kuishi Kila Siku

Tumekuwa ni kama wakulima ambao wanapanda leo na kesho wanafukua hata kabla mbegu haijaota. Hebu chukulia mfano, mkulima anapanda leo mbegu ya mahindi kesho anaifukua na kutaka tena kwenda kupanda kitu kingine. Je kwa mtindo huu, unafikiri ataweza kufanikiwa kweli? Ataweza kuona hata mbegu ikichipua? Hawezi kuiona, unapopanda unatakiwa uwe na subira mbegu ikae chini …

Hii Ndiyo Sehemu Pekee Ambayo Upendo Huwa Unapenda Kukaa

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna falsafa kubwa duniani kama upendo, ukiweza kuishi kwa upendo utaweza kushika amri zote. Karibu dini zote duniani zinashikilia falsafa ya upendo. Katika upendo tunapata kila kitu, upendo ndiyo asili ya dunia na tunapokwenda kinyume na upendo huwa tunapata shida. Kila mtu anajua ni kwa jinsi gani upendo ulivyokuwa na nguvu, kama …

Mbinu Bora Itakayokusaidia Kutoka Hapo Ulipo

Vita vikubwa ambavyo tunapaswa kuvitangaza ni vita dhidi ya miili yetu, hakuna upinzani mkubwa tunaopata katika maisha yetu kama upinzani wa miili yetu. Tusipokuwa makini na miili yetu basi tutaishia mahali pabaya sana. Miili yetu inapenda rah asana, inataka kile inachotaka bila sababu yoyote ile. Tukianza kuisikiliza miili yetu hakika hatutoweza kutoboa, hatutoweza kutoka hapa …

Jinsi Ya Kuwa Na Hekima Kwa Njia Rahisi

  Watu wengi wanaweza kujiuliza je nina wezaje kuwa na hekima? Hili ndiyo swali ambalo linaulizwa na watu wengi. Iko njia rahisi ya kuweza kuwa na hekima katika maisha yetu nayo ni kutumia akili. Kwa kuwa sisi ni binadamu tulioumbwa kwa jinsi ya ajabu tumepewa akili kubwa ya kuweza kujua zuri na baya. Kwa kutumia …

Huna Haja Ya Kuelezea Falsafa Yako

Mpendwa rafiki, Hatutakiwi kuyaanika maisha yetu hadharani, kila mtu ajue vile tulivyo. Unapoanika mambo yako na watu wakishakujua inakuwa si salama kwako tena. Huna haja ya kuelezea falsafa yako kwamba wewe ni mwanafalsafa wa ustoa au la. Unapochagua kuwa mwanafalsafa hutakiwi kuelezea na kusema kuwa wewe ni mwanafalsafa bali unatakiwa; Unatakiwa kuishi misingi ya kifalsafa, …

Design a site like this with WordPress.com
Get started