Kama Bado Unamtafuta Mtu Wa Kubadilisha Maisha Yako Soma Hapa

Mpendwa rafiki, Hakuna mtu anayekosa usingizi kwa sababu ya maisha yako, kila mmoja wetu yuko bize na mambo ambayo yanamchanganya kwenye maisha yake. Wako ambao wanasubiria serikali ibadilishe maisha yao, wako ambao wanasubiria wazazi wao wabadilishe maisha yao. Kusubiria watu wengine waje kubadili maisha yako ni kujiandaa kushindwa katika maisha yako. Maana watu wengi wamepoteza …

Jinsi Ya Kuishinda Hofu Ya Kuongea Mbele Ya Watu

Kila mmoja wetu ni muuzaji. Hivyo katika kuuza lazima ujifunze sana namna ya kuongea na watu vizuri ili waweze kukuelewa kile unachouza. Watu wengi wanafikiria kuuza ni mpaka uwe na bidhaa hapana, hata kuwa tu na wazo lako na ukaweza kushawishi wengine hapo tayari umefanikiwa kumuuziwa mawazo yako. Kuuza ni kumshawishi mtu aweze kukubaliana na …

Hizi Ndiyo Hisia Mbili Zinazowatawala Watu Wengi

Mpendwa rafiki yangu, Sisi binadamu ni viumbe wa hisia, na karibu maisha yetu ya kila siku yanaendeshwa na hisia, huwa tunafanya maamuzi kwa hisia mara nyingi sana lakini tunakuja kuhalalisha kwa kufikiri, ukitaka kuamini hilo angalia ni vitu vingapi unavyo ndani ulinunua tu kwa hisia na kwa sasa wala hata huvitumii. Vitu vingi tunavyofanya tunakua …

Hiki Ndiyo Kitu Chenye Nguvu Sana Katika Karne Ya 21

Mpendwa rafiki yangu, Tukiachana na pumzi hii tunayovuta kila siku basi kipo kitu ambacho ni muhimu sana baada ya pumzi. Na kitu hicho siyo kingine bali ni fedha. Fedha  ina ngumu sana katika maisha yetu. Licha tu ya kuwa na nguvu bali fedha ni muhimu sana katika maisha yetu. Fedha inakubalika kwenye kila eneo la …

Maswali Matatu(03) Ya Kujiuliza Kila Siku Ya Maisha Yako

Mpendwa rafiki yangu, Mmoja kati ya waasisi wa taifa la marekani Benjamin Franklin  aliwahi kusema kulala mapema na kuamka mapema inaleta afya,hekima na utajiri. Kumbe katika maisha tunapopangilia muda wetu vizuri tunapata faida sana. wengine watakuambia mpaka wanakosa muda kumpumzika hii yote siyo kwa sababu ya muda bali kukosa vipaumbele. Kama kitu ni muhimu kwako …

Huu Ndiyo Muda Sahihi Wa Kuomba Msamaha

Kila binadamu ana asili ya mahusiano  kadiri ya vinasaba. Kama kila mtu yuko katika mahusiano basi anatakiwa kujua somo la msamaha. Kama wewe uko hai basi unapaswa kujifunza juu ya msamaha, kwanini? Kwa sababu msamaha ni somo ambalo limegusa maisha yetu sisi binadamu kwa ujumla. Kila siku kuna watu ambao wanakwenda kinyume na sisi, wako …

Jinsi Ya Kujijua Kama Umeelewa Jambo Vizuri

Dunia kwa sasa imerahisishwa, kila kukicha watu wanafikiria ni namna gani wanaweza kufanya mambo kuwa marahisi na siyo magumu. Watu waliotutangulia duniani kabla ya kizazi chetu huenda maisha yao yalikuwa ni magumu kuliko sasa. Kwa sasa maisha yamerahisishwa sana, hatupo tena kwenye zama za mawe, bali tupo kwenye zama za taarifa. Dunia iko mikononi mwako, …

Jinsi Ya Kuishi Muda Mrefu

Mpendwa rafiki yangu, Kila mmoja wetu anapenda kuishi muda mrefu hapa duniani. Licha ya kuwa tunapenda kuishi muda mrefu hapa duniani tukae tukijua kuwa iko siku tutakufa. Iko mbinu ya kuishi muda mrefu ambayo ukiitumia kwenye maisha yako kuanzia sasa utakapojifunza hapa utafanikiwa sana. Aliyekuwa mwanafalsafa wa falsafa ya ustoa Seneca  enzi za uhai wake …

Jinsi Ya Kujenga Tabia Yoyote Ile

Mtu mmoja alishawahi kusema, tunatengeneza tabia na kisha tabia zinatutengeneza sisi. Jinsi ulivyo ni matokeo ya tabia ambazo umejitengenezea wewe mwenyewe. Tabia yoyote ile haijengwi kwa siku moja. Bali yale mazoea tunayoanzisha ya kupendelea kufanya mara kwa mara unajikuta tayari imeshakuwa tabia. Kwa mfano, huna tabia ya kuweka akiba, unachukua hata shilingi mia mbili unakuwa …

Hiki Ndicho Kinachokufanya Ujiumize Kwenye Jambo Fulani

Huwa tunajiumiza sisi wenyewe kwa kujua au kutokujua. Tunatengeneza picha ya vitu ambavyo siyo vya uhalisia kisha zile picha zinakuja kututengeneza. Hakuna tofauti na vile mtu anapotengeneza tabia yeye mwenyewe kisha tabia zile zile alizozitengeneza zinakuja kumtengeneza na yeye. Huwa tunajipa maumivu sisi wenyewe, pale ambapo tunapoona tukio fulani limetokea basi tunaanza kujihukumu sisi wenyewe …

Design a site like this with WordPress.com
Get started