Kama Unataka Kwenda Mbinguni Epuka Kufanya Dhambi Hizi Hapa Mbili

Siko hapa kukuhubiria injili bali niko kukuambia vitu viwili tu ambavyo vinawakwamisha watu wengi kufanikiwa kwenye maisha yao. Hata kwenda mbinguni ni mafanikio pia lakini siyo kila mtu ataenda mbinguni kwa sababu ya yale anayofanya. Tabia ulizonazo na yale unayofanya unafikiri yatakufikisha kule unakotaka kufika? Acha utani, weka kazi hakuna kitu kirahisi. Ingekuwa rahisi kila …

Naweza Kuajiri Watu Kunisaidia Kufanya Kila Kitu, Isipokuwa Vitu Hivi Viwili

Frank Bettger katika kitabu cha How I Raised Myself From Failure to Success in Selling aliweza kumnukuu na kujifunza kauli moja kutoka kwa aliyekuwa mmiliki wa viwanda alisema hivi, naweza kuajiri watu kunisaidia kufanya kila kitu isipokuwa vitu viwili tu, kufikiri na kufanya vitu kwa mpangilio wa umuhimu wake. Rafiki yangu, huwa nakushirikisha hapa vitu …

Vitu Viwili Muhimu Vya Kuzingatia Kwa Kila Muuzaji

Ni imani yangu kwamba kama uko hai, basi kuna kitu unaendelea kuuza hapa duniani. Kwa sababu hakuna mtu ambaye anaweza kuendesha maisha yake pasipo mauzo. Tunapouza maana yake tunatoa, na katika maisha asiyetoa maana yake hapokei, hivyo basi, kila anayetoa huwa anapokea kadiri ya sheria ya asili. Ukiwa kama muuzaji bora kuwahi kutokea kwenye eneo …

Kitu Ambacho Huwezi Kukibadilisha Kwenye Mahusiano

Kuna wakati huwa tunaumia kwenye mahusiano yetu kwa sababu ya kujitakia wenyewe. Kwenye mahusiano, watu wengi wanapenda kuwa viranja wa kuwatawala wengine, yaani wanataka watu wengine waishi kama vile wanavyotaka wao. Kitu ambacho huwezi kukibadilisha kwenye mahusiano ni kumbadilisha mtu kuwa kama vile unavyotaka wewe. Ni kazi kubwa sana, pata picha mtu amekulia malezi tofauti, …

Kitu Ambacho Kimezungumziwa Kwenye Kila Kitabu Unachokijua Wewe

Huwezi kusoma kitabu chochote kile ukakosa kukutana na sentensi usikate tamaa. Kila mtu ambaye amesoma kitabu basi anao ushahidi huo kwamba, amekutana na sentensi inayosema usikate tamaa. Hata wewe rafiki yangu napenda kukuambia tena usikate tamaa. Kukata tamaa kwenye maisha ni kujinyima mafanikio makubwa ambayo yapo mlango wa pili. Endelea kukazana mpaka ufikie mlango wa …

Swali Muhimu Sana La Kujiuliza Pale Tu Unapokutana Na Kitu Usichotegemea

Mwandishi Deepak Chopra anasema hakuna ajali, ila kuna kusudi ambalo bado hatujalijua. Mara nyingi mambo yanapotokea kwenye maisha yako bila ya wewe kutegemea kutokea huwa yanapotokea unasema ni ajali. Lakini Chopra anatuambia hakuna ajali, badala yake kuna kusudi ambalo bado hatujalijua. Kila kinachotokea kwenye maisha yako, iwe ni kizuri au kibaya jua kimekuja na kusudi …

Ukitaka Watu WasikupuuzeKuwa Hivi

Kuwa bora kiasi kwamba hakuna anayeweza kukupuuza kwenye kile unachofanya. Hakuna mtu ambaye anafanya vitu vyake kwa ubora halafu watu wakampuuza. Ukishakuwa bora watu watakuheshimu wao wenyewe yaani kifupi, ubora wako utakuheshimisha. Chochote kinachopita mkononi mwako kifanye kwa ubora wa hali ya juu. Kama unafanya kazi, ifanye kazi yako kwa ubora kiasi kwamba hakuna atakayekupuuza …

Hiki Ndicho Kinachokufanya Usifanikiwe

Kama unaweka mipango na hufanikiwi ulishawahi kujiuliza nini kinakuzuia usifanikiwe? Huwezi kufika kule unakotaka kufika kama huna mikakati ya kufika huko. Unaweza kuwa na mikakati lakini kitu kimoja tu kikakukwamisha ambacho ndiyo kitu kinachowasumbua watu wengi. Kitu hicho ni ukosefu wa nidhamu ya UTEKELEZAJI. Kama kila mtu akiwa na nidhamu ya UTEKELEZAJI basi hakuna kitu …

Haya Ndiyo Majibu Unayopaswa Kumpatia Mteja Wako Pale Anapokuuliza Kuhusu Washindani Wako

Wafanyabiashara wengi huwa wanajua njia pekee ya kukubalika na mteja ni kumsema vibaya mshindani wake. Baadhi ya wafanyabiashara huwa wanachukiana na hata kujenga uadui kabisa hasa zaidi pale anapoona mteja wake ameenda kupata huduma sehemu nyingine au mshindani wake anauza zaidi au anapata wateja zaidi. Kumekuwa hakuna habari njema dhidi ya washindani tunaofanya nao biashara …

Mbinu Bora Ya Kujiamini Na Kuaminika Na Wengine Kwenye Kile Unachofanya

Kama unataka kujiamini na kuaminika na wengine kwenye kile unachofanya, basi jua vizuri kile unachofanya na kuendelea kujifunza. Kwa mfano, Ijue biashara yako na endelea kujifunza kuhusu biashara yako. Ijue kazi yako na endelea kujifunza kuhusu kazi yako. Na kitu muhimu zaidi ni kwamba kujifunza hakuna mwisho. Hivyo basi endelea kujifunza kuhusu kile unachofanya na …

Design a site like this with WordPress.com
Get started