Kama Unataka Kuwa Muuzaji Mzuri, Kuwa Na Tabia Hizi Mbili

Kiasili, kila mtu ni muuzaji.Kila mtu anauza kila wakati, haijalishi wewe ni nani, kila unapokutana na mtu mwingine, unapoelezea wazo lako, unapotoa maoni yako, unauza kitu muhimu sana, ambacho ni wewe mwenyewe. Kitendo tu cha kuweza kumshawishi mtu na akubaliana na wewe hapo unakuwa muuzaji. Kwa sababu umeuza mawazo yako kwa wengine. Kama unatafuta kazi …

Adhabu Zinawasaidia Watoto Kuelewa Uhalisia Wa Dunia

Wazazi wa siku hizi wanawalea watoto utafikiri wamepata mkataba wa kuishi nao milele. Wazazi hawataki kuwafundisha watoto kukosa. Mtoto akitaka kile anachotaka anapewa mara moja. Hii inamfanya mtoto kuja kuteseka baadaye anapokuja kuingia kwenye uhalisia wa mambo. Watoto wanaharibiwa kwa kukosa adhabu kuliko kuharibiwa na adhabu. Kumekuwa na harakati nyingi za kufuta adhabu kwa watoto …

Usiende Mahali Ukiwa Fedha Hii Tu

Kwenye maisha lolote linaweza kutokea. Na maisha ni safari huwezi kujua nini kitatokea katika ya safari. Hivyo basi, unapoishi lazima uishi kwa tahadhari kwamba ujiandae kukabiliana na lolote lile litakalojitokeza. Kwenye fedha, ninao ushauri mzuri ambao napenda kukuambia leo rafiki yangu. Ushauri huu nilijifunza kutoka kwa mwandishi Grant Cardone ambaye ni mwandishi wa mambo ya …

Vitu Viwili Vitakavyokufikisha Kwenye Utajiri

Natumaini kama unasoma hapa, huna lengo la kuwa masikini. Bali lengo lako kuu ni kuwa tajiri. Tunapaswa kuungana wote duniani kupambana na adui ambaye anatesa watu ambaye ni umasikini. Umasikini ni laana, tupambane usiku na mchana kumtokomeza adui huyu ambaye kwa sasa ameshaota mizizi. Na umasikini wa watu wengi hauko mfukoni bali uko kwenye akili. …

Kwenye Kila Mauzo Angalia Hiki

Angalia faida. Kwenye mauzo yoyote yale unayofanya angalia faida. Faida ndiyo kila kitu kwenye biashara, usifanye biashara kwa hasara kwa sababu hasara haitakusaidia kulipa bili wala kuendesha biashara yako. Unapofanya mauzo, kitu cha kwanza kufanya ni kuchukua mauzo kutoa gharama za mauzo. Kile kinachobakia sasa ndiyo faida yako halisi. Na ili upate faida nzuri, hakikisha …

Kero Unayoipata Kwenye Biashara Ya Wengine

Itumie kero hiyo kuboresha biashara yako na kuwa bora. Huwa tunajifunza vitu vingi sana kwenye biashara za wenzetu pale tunapoenda kupata huduma fulani. Kuna wakati unakutana na vitu vizuri na unajiambia kabisa hiki nitaenda kukitumia kwenye kazi au biashara yangu. Na kuna wakati unaenda kupata huduma kwenye biashara nyingine unakutana na huduma mbovu kiasi kwamba …

Kitu Kinachomfanya Mtu Achukue Hatua Haraka

Huwa tunalalamika kwanini watu wengine tukiwaambia wafanye kitu fulani hawachukui hatua.Siyo tu watu wengine, wakati mwingine hata sisi wenyewe tunakuwa ni wagumu kuchukua hatua. Unafikiri ni kwanini watu wanakuwa wagumu kuchukua hatua? Kwa sababu hujagusa maslahi yao binafsi. Kitu kinachomsukuma mtu kuchukua hatua haraka ni maslahi. Mtu anakuwa ana hamasika kuchukua hatua pale anapokuwa anaona …

Usisome Kumaliza, Soma Kujifunza

Watu wengi huwa wanasoma kama kasuku, wanakimbilia kusoma ili wamalize vitabu vingi. Wengine watajitamba kwamba, wamesoma vitabu kadhaa ndani ya muda fulani. Kujitamba bila matokeo hakuna maana yoyote ya kusoma vitabu. Unapokuwa mtu wa kusoma, tunataka kuona matokeo mazuri na siyo kumuona mtu yule yule kila siku. Maisha ya kusoma vitabu yakubadilishe kweli, uishi yale …

Kwanini Ni Muhimu Kila Mfanyabiashara Kuijua Biashara Yake Kwa Undani?

Ni muhimu sana kila mfanyabiashara kuijua biashara kwa undani, Kwanini? Ili kuweza kumsaidia kufanya maamuzi sahihi kila wakati. Kuendesha biashara ni sayansi na sanaa. Na kwenye sayansi kuna vitu vina kanuni na kwenye sanaa hakuna kanuni ni kufanya maamuzi kulingana na hali jinsi inavyokwenda. Usipoijua vizuri biashara yako, ni rahisi sana kuipoteza. Ijue biashara yako …

Jinsi Ya Kutengeneza Deni Ili Ulipwe

Kwenye maisha lazima utengeneze madeni mengi kwa watu wengine ili ulipwe. Unatengenezaje sasa madeni hayo? Ni kwa njia ya utoaji. Utoaji huwa unatengeneza deni ambapo upande uliopokea huwa unasukumwa kulilipa kwa namna yoyote ile. Kwa mfano, mtu akikusaidia kitu, utatafuta namna yoyote ile ya kurudisha fadhila kwa sababu amekusaidia. Ndivyo binadamu walivyo, ukimpa kitu anatafuta …

Design a site like this with WordPress.com
Get started