Hiki Ndiyo Kitu Ambacho Wanandoa Wengi Wanaoga Kuambiana

Mpendwa rafiki yangu, Kwa asili hakuna kitu kibaya au kizuri. Ubaya au uzuri wa jambo unaletwa na tafsiri zetu juu ya kile kitu. hivyo basi, wako ambao wanaona ndoa ni kitu kizuri na wengine wanafikiria kinyume na hivyo. Kila mtu ana mtazamo wake na kila mtu yuko sahihi kadiri ya kile anachokiamini yeye. Ukikaa na …

Usiingie Katika Biashara Kama Una Roho Hii

Mpendwa rafiki, Ni rahisi watu kuongelea biashara kwa njia ya mdomo, miaka nenda rudi, na ziko sababu nyingi zinazowafanya wasichukue hatua lakini ukizichunguza ni za uwongo, wako ambao watakuambia mtaji ndiyo shida na sababu nyingine nyingi ambazo hazina mashiko. Katika zama hizi, kutegemea kipato kimoja ni hatari sana na lolote linaweza kutokea hata katika hicho …

Hii ndiyo Mbinu Ya Kumfanya Mtoto Wako Kuwa Bora

Watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu. Hakuna aliyeandika barua kuwa anataka kuzaliwa au alichagua azaliwe na wazazi fulani. Wote tumejikuta tumezaliwa na wazazi ambao tunao sasa. Kuzaa siyo kazi, kazi kulea mwana. Hakuna kazi ngumu kama malezi , hiki ni kipindi cha kumuunda mtoto vile unavyotaka wewe, tukikosea katika malezi, tumekubali kuwaharibu watoto wetu sisi …

Kitu Ambacho Kipo Nje Ya Uwezo Wako

Muda mwingine ukitaka mambo yaende kama ulivyopanga wewe utashindwa. Huwezi kuzuia dunia iende kama vile unavyotaka wewe. Huwezi kuzuia matukio ya dunia bali unachotakiwa yaruhusu yatokee kama yalivyopangwa kutokea. Kutaka watu wafanye kama unavyotaka wewe,waende kama vile unavyotaka wewe ni kitu ambacho kipo nje ya uwezo wako. Watu wanaishi vile wanavyotaka wao ila ukienda kinyume …

Jinsi Ya Kuishi Katika Nyumba Yako Mpya na Kuwa na Gari Lako Jipya

Rafiki yangu, Naanza kwa kusema mchezo mzima wa mafanikio unaanzia akili kwako. Akili yako ndiyo inaunda kile unachotaka katika maisha yako. Akili yako ni sumaku huwa ina tabia ya kuvuta kile unachowaza mara nyingi. Je namna gani unaweza kuwa na nyumba yako mpya na gari lako jipya? Ni rahisi tu, weka nyumba au gari unalotaka …

Katika Nafasi Yoyote Ya Uongozi Uliyonayo Hakikisha Una Kuwa Na Kitu Hiki

Mpendwa rafiki, Katika uongozi wowote ule unahitaji utu, siyo kwamba wewe ukiwa kiongozi ndiyo unatakiwa kutumia matakwa yako kama vile unavyotaka wewe. Yaani wewe uko juu ya sheria, yaani rule of law. Tunatakiwa kutumia matakwa yetu vizuri, ili tuwe na uongozi bora ndani yetu tunaalikwa kuwa na kitu hiki; Unyenyekevu, tunaalikwa kuwa na unyenyekevu katika …

Uko Kundi Gani Kati Ya Haya Mawili

Rafiki, Maisha yetu yanaathiri watu wengine kwa kiasi kikubwa sana, kama tutakuwa tunaishi maisha yenye mchango chanya kwa wengine basi tutatukuwa tunawaathiri sana wengine na kufanikiwa kwa vile tunavyofanya na tunavyoishi. Leo hii nakupa kazi moja rafiki yangu, nenda kajitafakari je wewe unasemwa kwa mazuri au mabaya? Dunia huwa inatupa kile tunachokitoa nje, usitegemee unatoa …

Usiishi Bila Kuwa Na Kitu Hiki Katika Maisha Yako

Sisi binadamu ni viumbe wa hisia na kila binadamu yuko katika mahusiano ni mpango wa Mungu kila bindamu kuwepo katika mahusiano. Una mahusiano ya familia yako, wazazi, ndugu, nakadhalika. Mahusiano ndiyo yanafanya maisha yetu kuwa mazuri au mabaya. Kama tukiwa na fedha na mahusiano yako vizuri basi maisha yanakuwa mazuri na ya kitajiri, kwani maisha …

Siku Hii Ya Leo Nenda Katawale Kitu Hiki Moja Na Utakuwa Na Siku Bora

Rafiki, Kila mtu anataka kuwa na siku bora, hivyo huwezi kuwa na siku bora kama hujui jinsi ya kuwa na siku bora katika maisha yako. Ukitaka kuwa na siku bora, tawala kwanza mawazo yako. usikubali uendeshwe na hisia yoyote bali kubali kuingozwa na akili kwanza. Chochote unachotaka kufanya rudi kwanza kwenye kufikiri kwanza kabla ya …

Jijengee Tabia Hii Muhimu Katika Mambo Ya Fedha

Rafiki, Kila kitu katika maisha yetu ni tabia. Tabia tulizonazo leo tulizianzisha sisi wenyewe hivyo katika kila jambo huwa tuna vuna kile tulichopanda. Matokeo unayopata sasa hivi ni kutokana na kile ulichopanda. Hata katika mambo ya fedha tabia ulizonazo leo ni kutokana na tabia ulizojijengea huko nyuma. Unachotakiwa sasa ni kuvunja tabia zote hasi ambazo …

Design a site like this with WordPress.com
Get started