Kinachokufanya Usiende Mbele Ni Hiki Hapa

Hakuna kitu kingine zaidi ya kutochukua hatua. Hakuna mtu asiyejua ili afanikiwe anapaswa kufanya nini. Hakuna asiyejua ili afanikiwe kiroho, kiakili au kimwili anatakiwa kufanya nini. Watu wanajua kile wanachopaswa kufanya lakini shida iko kwenye kutokuchukua hatua. Wako watu wana kiri kabisa baada ya kuanza kuchukua hatua kwa nidhamu sasa wanaona mabadiliko chanya kwenye maisha …

Hakuna Mtu Anayependa Kukuona Wewe Ukipata Fedha

Iko wazi na siyo siri. Ukitaka ugomvi na watu ni pale wanapojua wewe unapata hela zaidi kuliko wao. Hakuna mtu anayependa kukuona wewe ukipata hela. Wako wachache sana watafurahia kukuona wewe ukipata hela nyingi lakini wengine utawakera na watakuchukia. Hakuna mtu anayependa kukuona wewe ukipata hela kwa mfano, ukiwa umeajiriwa na ukawa na miradi yako …

Tulia Kwenye Eneo Hili

Kama unataka kufikia kitu fulani kwenye maisha yako, iwe ni ndoto au lengo kubwa au kitu chochote kile unapaswa kutulia kwenye eneo la mchakato. Tulia kwenye mchakato na mafanikio yatakuja yenyewe. Kumbuka kuwa mchakato ndiyo zawadi. Ndiyo lengo la kufanya. Unafanya ili ufike kule unakotaka kufika. Mchakato ni kama mwendesha baiskeli, ili afike anapaswa kuendelea …

Huu Ndiyo Uhakika Wa Kufikia Ndoto Yako

Uhakika wa kufikia ndoto au lengo lolote ulilo nalo unakuja pale ambapo unakuwa unaifanyia kazi ndoto yako kila siku. Licha ya kuwa sisi binadamu hatuwezi kudhibiti matokeo yoyote yale, lakini tunaweza kupata matumaini ya uhakika kupitia mchakato au kazi tunayofanya kila siku. Kila siku ukijitahidi kuchukua hatua hata kama ni ndogo kiasi gani ni alama …

Mambo Ya Kuepuka Kukumbushiana Na Mwenza Wako Wa Ndoa

Hakuna mtu aliyekamilika kwenye kila eneo la maisha yake. Binadamu tuna asili ya udhaifu. Na kila mmoja wetu anakua kadiri ya mtazamo anaokutana nao kwenye jamii yake aliyokulia. Kawaida wanandoa wengi huwa wanaingia kwenye ndoa tayari wakiwa wakubwa hivyo kila mtu anakuwa na tabia zake. Na kazi inaanza pale wawili hao wanapoanza kuishi pamoja. Kwa …

Kauli Ya Kishujaa Unayopaswa Kujiambia Kila Siku

Kila siku unapoamka salama jiambie kila kitu kinawezekana.Mwanzoni ulikuwa unajiuliza utawezaje kuwa hivyo ulivyo leo lakini mbona leo umekuwa hivyo ulivyo leo? Kumbe kila kitu kinawezekana. Endelea kuwa na ndoto kubwa halafu kila siku jiambie inawezekana kuwa mtu fulani. Kwa mfano, jiambie inawezekana kuwa tajiri, yaani weka uwezekano kwenye kile unachotaka kufanya. Maisha yanakupa kile …

Haya Ndiyo Maisha Unayopaswa Kuishi

Ukiwa unatembea njiani ukikutana na ng'ombe mwenye rangi nyeupe, nyeusi hutoweza kushtuka kwa sababu unajua ni kitu cha kawaida tu ng'ombe kuwa na rangi tajwa hapo juu. Lakini;Ukikutana na ng'ombe mwenye rangi ya zambarau yaani purple cow lazima utashangaa kwa sababu siyo kitu cha kawaida ng'ombe kuwa na rangi ya zambarau. Lazima utaacha kile unachofanya …

Yaonee Huruma Maisha Yako

Maisha tayari ni magumu lakini watu wanayafanya kuwa magumu zaidi. Tafadhali, naomba uyaonee huruma maisha yako. Acha kuyafanya kuwa magumu zaidi. Kwenye kitabu cha Follow Your Heart mwandishi anasema kuwa, maisha yakiwa rahisi, huwa tunatafuta njia ya kuyafanya kuwa magumu zaidi. Na ukiliangalia hilo liko wazi. Mtu akiwa hana kipato kikubwa ataishi kwa nidhamu kubwa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started