Pata Kitabu Cha Ijue Njaa Ya Wanandoa Na Zawadi Inayodumu Mpaka Kesho

Habari rafiki yangu nikupendae,  Leo ninayo habari njema kwa wakazi wa Dar Es salaam, kuanzia leo kitabu cha Ijue Njaa Ya Wanandoa kinapatikana jijini Dar Es salaam huna haja tena ya kutuma na nauli wewe ni kutoa tu oda nahitaji kitabu na kuletewa kitabu hapo ulipo.  Tumekusogezea huduma karibu na kazi hii itakuwa inafanywa na …

Sehemu Ambayo Hupaswi Kukaa Kwenye Foleni

Tokea tunazaliwa mpaka tumekua, tumekaririshwa kukaa kwenye foleni na siyo kuruka foleni. Leo nakwenda kukushirikisha sehemu ambayo hupaswi kukaa kwenye foleni. Badala yake ruka foleni au chepuka. Usibaki kwenye njia kuu maana utachelewa kufika. Eneo ambalo hupaswi kukaa kwenye foleni ni eneo la kipato. Yaani kama kila mwisho wa mwezi kipato chako ni kile kile …

Hiki Ndiyo Kitu Ambacho Watu Wengi Wanapenda Kupata

Ni uhakika.Watu wakipata uhakika huwa wanapata utulivu wa ndani. Hata mteja yeyote yule akishahakikishiwa uhakika na muuzaji na kumpa ushuhuda anakuwa hana shaka tena. Anapata utulivu wa ndani na kuendelea kufanya yake. Watu wengine wanaogopa au kuchelewa kufanya maamuzi kwa sababu ya hofu ya kushindwa kupata uhakika.Mtu anakuwa anajiuliza hivi nikilipia nitapata kile nachotaka au …

Jinsi Ya Kupata Utulivu Wa Akili

Tunaishi katika zama za kuvurugwa na mitandao ya kijamii. Watu wanakosa utulivu wa akili kwa sababu ya kutingwa na mambo mengi ya kidunia. Yaani kila siku mikimiki, mtu hatulii akatulia kwa sababu ya mambo ambayo hata hayana faida kwake. Siyo kila mtu ambaye yuko bize anazalisha faida. Wengine wako bize kweli lakini hawana wanachozalisha zaidi …

Kila Siku Unapaswa Kuitumia Kanuni Hii

Kifupi rafiki yangu, kila siku unatakiwa uwe bora zaidi ya jana. Yaani siku zako mbili zisifanane. Kama unataka siku zako mbili zisifanane unatakiwa kutumia au kuishi kanuni moja inayojulikana kama kanuni ya Kaizen Rule. Kanuni hii ikoje kwani? Hii kanuni inasema hivi, never ending improvement, yaani uwe na maboresho kila siku. Isifikie mahali ukasema sasa …

Jinsi Ya Kukabiliana Na Changamoto Ya Wategemezi Wengi Uliokuwa Nao

Katika jamii zetu ni ngumu watu kukosa utegemezi. Kama hutegemewi na wazazi, utategemewa na watoto, ndugu nk. Hata kama unawapenda sana wazazi na ndugu zako kiasi gani unapaswa kuwa na kiwango katika usaidizi wako. Utajikuta huendi mbele kwa sababu na wewe pia unahitaji kutengeneza maisha yako. Lakini hupaswi kulalamika kuwa huendelei kwa sababu nimekuwa na …

Njia Bora Ya Kupata Msaidizi Kwenye Biashara Yako

Kazi ya kushughulika na watu ni kazi ngumu duniani. Dunia kwa sasa inapambana kutengeneza maroboti ili yaweze kufanya zile kazi ambazo watu wanazifanya. Kwa sababu watu wanasumbua na ni pasua kichwa kweli. Mtu atakuambia sina kazi mpe kazi halafu utaona namna anavyofanya kazi zake kimazoea. Watu wanapenda kupata fedha lakini hawako tayari kuzalisha thamani ya …

Maisha Yako Yanatakiwa Yawe Hivi Kwa Wengine

Unaweza kuwa na maarifa lakini ukakosa hekima. Hekima ni matumizi ya maarifa ambayo unayo. Kwa mfano, wewe ni daktari unawashauri wagonjwa wasivute sigara wakati na wewe mwenyewe unavuta sigara. Kwenye haya maisha kujitambua ni kazi sana. Huwa napenda kusema kujitambua ni zawadi kutoka kwa Mungu. Na huwezi kuipata zawadi hii mpaka wewe mwenyewe uamue kuipata. …

Hii Ndiyo Fedha Unayopaswa Kuithamini Kuliko Fedha Zingine Zote

Ni FEDHA unayojilipa wewe mwenyewe. Hii ndiyo fedha ya utajiri wako maana inakuwa inafanya kazi kwa ajili yako. Fedha zingine zote siyo za kwako kwa sababu unawalipa wengine bili mbalimbali. Lakini hii unayojilipa ndiyo unatakiwa kuwa nayo makini sana maana hii ndiyo chanzo chako cha wewe kuwa tajiri au masikini. Fedha unayojilipa hakikisha unaiwekeza sehemu …

Hili Ndilo Eneo Unalopaswa Kuongeza Thamani

Katika kuongeza thamani tafuta eneo ambalo upatikanaji wa wanaoweza kikifanya ni wachache na uhitaji ni mkubwa mno. Angalia tatizo ambalo linawasumbua wengi lakini hakuna wengi wanaolifanyia kazi. Au angalia watu wanavyofanya kazi zao kimazoea halafu wewe njoo uzifanye kwa ubora na ubunifu. Yaani weka utii, ubunifu na kujituma. Jitofautishe na wale ambao wanatoa huduma za …

Design a site like this with WordPress.com
Get started