Hivi Ndivyo Vitu Ambavyo Hupaswi Kushukuru Kwenye Maisha Yako

Rafiki, Tunaalikwa kushukuru kwa kila jambo, lakini siyo kila jambo tunapaswa tu kushukuru nitakuambia baadaye kivipi. Kushukuru ni utamaduni wa kila mwanadamu, tukikosa kushukuru basi tutakuwa hatuna fadhila. Tunaposhukuru ndiyo tunatengeneza nafasi ya kupata zaidi. Kitu ambacho kipo ndani ya uwezo wako halafu umeshindwa kukifanya hupaswi kukaa chini na kusema nashukuru kwa kila jambo. Unashindwa …

Hiki Ndiyo Kipimo Cha Kuonesha Kama Umeelewa Kitu

Mara nyingi unapokuwa unafundisha unatakiwa kuwaelezea wanafunzi kwa lugha rahisi ili waweze kukuelewa. Kumfundisha mtu kwa lugha ngumu ambayo haielewei huo ni ujinga. Aliyekuwa mwanafizikia Einstein aliwahi kusema, kama huwezi kuelezea kitu kwa lugha rahisi basi hujakielewa. Kwahiyo, kipimo cha kuonesha kama wewe umeelewa kitu ni kuwaelezea wengine kwa lugha rahisi. Ukiona huwezi kuelezea kwa …

Ukienda Sokoni Nunua Mahitaji Usinunue Maradhi

Ukienda sokoni jitahidi sana kununua mahitaji muhimu sana na siyo maradhi. Wengi huwa tunaenda sokoni lakini hatuendi kununua mahitaji bali tunaenda na mengi ambayo yanatusababishia kuyapata ambayo siyo muhimu. Ukiwa na fedha mkononi unatakiwa kuwa makini sana, maana fedha uliyonayo inaweza kukusaidia kununua maradhi au uhai. ‘’ nimewapeni uchaguzi kati ya uhai na kifo, kati …

Kwanini Umasikini Siyo Mpango Wa Mungu

Rafiki, Umasikini siyo haki yako ya kuzaliwa bali utajiri ndiyo haki yako ya kuzaliwa. Ni haki ya kila mmoja wetu kufanikiwa, kuwa tajiri. Kila mtu ana uwezo wa kuwa vile anavyotaka kuwa kadiri apendavyo yeye. Umasikini ni adui mkubwa sana wa binadamu, tunaalikwa kumpiga vita vikali, siyo rafiki mzuri kwani hatupatii kile tunachotaka. Lakini utajiri …

Kama Unataka Usipoteze Siku Yako Fanya Kitu Hiki

Rafiki, Kwa zama hizi za taarifa watu wamekuwa ni mabingwa wa kupoteza siku zao. Watu wako bize lakini hakuna kikubwa wanachoingiza wazungu wanasema busy for nothing. Changamoto ya zama hizi ni kwamba mitandao ya kijamii inawachangia sana kuwavuta watu kuvunja siku zao. Siku moja nilikuwa na mwadhiri wa chuo kikuu fulani, akaniambia yaani nikiamka nikishika …

Jinsi Watu Wanavyojidanganya Kwenye Suala La Kuweka Akiba

Hatuwezi kuendelea kama hatuwezi kuweka akiba. Kupata fedha na kutumia yote bila kuweka akiba ni umasikini mkubwa sana. Kila mmoja wetu anaalikwa kuweka akiba ambayo itamsaidia katika dharura. Watu wengi ambao wanakuwa wanakimbilia kukopa ni wale ambao hawana akiba. Kama una akiba na umepatwa na dharura kwanini uende ukakope? Unakopa kwa changamoto za fedha kidogo …

Mambo Muhimu Ya Kuondoa katika Akili Ya Watoto

Watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu. Wazazi nao ni zawadi kutoka kwa Mungu, hakuna aliyewahi kuandika barua ya kuomba kuzaliwa na mzazi fulani. Bali wote tumejikuta tumezaliwa na wazazi ambao tunao sasa. Waswahili wanasema, kuzaa siyo kazi bali kazi ni kulea mwana. Kuna kazi kubwa sana ya malezi kwa sasa. Kumlea mtoto katika mtazamo chanya …

Hiki Ndiyo Kiunganishi Cha Ushindi Wowote Ule Unaotaka

Mpendwa rafiki, Kila mtu ni bosi wa maisha yake mwenyewe. Kila mtu ni bosi katika kazi yake. Hakuna mtu anayeweza kufanya kazi ya mwenzake. Kazi ya mtu ni kazi ukipewa hutoiweza hata kidogo. Tunatakiwa kuheshimu kazi za mwenzetu kwani kila mmoja ana kazi yake. Unaweza kuiona kazi ya mtu ni rahisi ila ukiingia kuifanya utaona …

Hiki Ndiyo Chanzo Kikuu Cha Maamuzi Mabovu

Mpendwa rafiki yangu, Kama kuna eneo ambalo wengi wetu tunaongoza kufanya maamuzi basi hayo maamuzi mengi ni mabovu. Wengi tumekuwa tu tunafanya maamuzi kwa sababu ya kuongozwa na hisia. Asilimia kubwa ya maamuzi tunayofanya mengi ni hisia na siyo akili. Tunakuwa na matatizo mengi sana kwa sababu ya kufanya maamuzi mabovu. Maamuzi ndiyo maisha, utakapoamua …

Eneo Muhimu Unalopaswa Kulidhibiti Katika Fedha

Fedha ni muhimu sana katika maisha yetu hilo halina ubishi. Watu wengi wamekuwa ni masikini wa fedha katika eneo la matumizi. Ukiangalia matumizi ya watu wengi unakuta matumizi yako juu ukilinganisha na kipato. Hii ni alama ya hatari sana. Kama mtu kipato chake ni 10 halafu matumizi yake ni 15 basi huyo yuko hatarini sana. …

Design a site like this with WordPress.com
Get started