Jinsi Ya Kuwasha Moto Wa Hamasa Ndani Yako

Watu wengi wanaamua kufanya kitu fulani kwa sababu ya hamasa. Hamasa iliyoko ndani yetu ndiyo inatusukuma kuthubutu jambo fulani. Mara nyingi pale tunapokuwa na hamasa ya kazi fulani tunakuwa kama vile tuna moto ndani yetu unaowaka na hatuwezi kuuzima kwa kuongea bali kwenda kufanya kile ambacho kipo ndani yetu. Na muda mzuri wa kufanikiwa jambo …

Kama Unataka Kuona Maisha Yako Ni Bora Fanya Kitu Hiki Kimoja

Rafiki, Kila mtu maisha yake ni bora kuliko ya mwingine kama kila mmoja wetu akiishi maisha yake. Maisha ya kujilinganisha na mwingine ni maisha ambayo hayana maana kuishi. Kujilinganisha na mwingine ni mwizi wa furaha yako. Ukitaka tu kujiona wewe uko tofauti na wengine anza kujilinganisha utatamani kuyakimbia maisha yako. Hakuna anayejilinganisha na mwingine halafu …

Jiandae Kuwa Mbahili Katika Msimu Huu Wa Sikukuu

Rafiki yangu, Katika msimu wa sikukuu watu ndiyo wanaongoza sana kutumia hela, wako wanaoingiza sana na wako wanaotumia sana fedha. Huwa wengi wanaongozwa sana na hisia katika matumizi ya fedha. Usikubali kutumia hisia katika matumizi ya pesa katika msimu wa sikukuu. Ukiruhusu hisia zikutawale, utajikuta unanunua vitu ambavyo huna hata uhitaji nao, sijakuambia usinunue kitu …

Haya Ndiyo Maisha Ambayo Hayana Msingi Wa Kuishi

Rafiki, Usiishi tu kama mbuzi, bali ishi kama binadamu mwenye uwezo mkubwa wa akili.  Ishi kwa malengo, unatakiwa kuwa na malengo ya siku, wiki, mwezi na hata mwaka.  Usipokuwa na malengo ya kitu chochote utapoteza siku, muda bila kujua hata muda na siku zimeishaje. Wengi hawajiongozi kwa ratiba tokea wanapoamka asubuhi na mapema bali wanaongozwa …

Hiki Ndiyo Kitu Ambacho Hakifichiki Katika  Utendaji Wa Kazi

Rafiki yangu mpendwa, Kazi ni asili ya kila mwanadamu hapa duniani. Ukikataa kufanya kazi maana yake umechagua kuwa mtu wa hovyo. Mtu asiyetaka kufanya kazi ni wa hovyo maana hatapendwa na yeyote, kila mtu atamkwepa maana ni mzigo. Amka asubuhi na nenda kafanye kazi, ipende kazi na jua kabisa kazi ndiyo rafiki yako kwa sababu …

Hivi Ndivyo Vitu Ambavyo Hupaswi Kushukuru Kwenye Maisha Yako

Rafiki, Tunaalikwa kushukuru kwa kila jambo, lakini siyo kila jambo tunapaswa tu kushukuru nitakuambia baadaye kivipi. Kushukuru ni utamaduni wa kila mwanadamu, tukikosa kushukuru basi tutakuwa hatuna fadhila. Tunaposhukuru ndiyo tunatengeneza nafasi ya kupata zaidi. Kitu ambacho kipo ndani ya uwezo wako halafu umeshindwa kukifanya hupaswi kukaa chini na kusema nashukuru kwa kila jambo. Unashindwa …

Hiki Ndiyo Kipimo Cha Kuonesha Kama Umeelewa Kitu

Mara nyingi unapokuwa unafundisha unatakiwa kuwaelezea wanafunzi kwa lugha rahisi ili waweze kukuelewa. Kumfundisha mtu kwa lugha ngumu ambayo haielewei huo ni ujinga. Aliyekuwa mwanafizikia Einstein aliwahi kusema, kama huwezi kuelezea kitu kwa lugha rahisi basi hujakielewa. Kwahiyo, kipimo cha kuonesha kama wewe umeelewa kitu ni kuwaelezea wengine kwa lugha rahisi. Ukiona huwezi kuelezea kwa …

Ukienda Sokoni Nunua Mahitaji Usinunue Maradhi

Ukienda sokoni jitahidi sana kununua mahitaji muhimu sana na siyo maradhi. Wengi huwa tunaenda sokoni lakini hatuendi kununua mahitaji bali tunaenda na mengi ambayo yanatusababishia kuyapata ambayo siyo muhimu. Ukiwa na fedha mkononi unatakiwa kuwa makini sana, maana fedha uliyonayo inaweza kukusaidia kununua maradhi au uhai. ‘’ nimewapeni uchaguzi kati ya uhai na kifo, kati …

Kwanini Umasikini Siyo Mpango Wa Mungu

Rafiki, Umasikini siyo haki yako ya kuzaliwa bali utajiri ndiyo haki yako ya kuzaliwa. Ni haki ya kila mmoja wetu kufanikiwa, kuwa tajiri. Kila mtu ana uwezo wa kuwa vile anavyotaka kuwa kadiri apendavyo yeye. Umasikini ni adui mkubwa sana wa binadamu, tunaalikwa kumpiga vita vikali, siyo rafiki mzuri kwani hatupatii kile tunachotaka. Lakini utajiri …

Kama Unataka Usipoteze Siku Yako Fanya Kitu Hiki

Rafiki, Kwa zama hizi za taarifa watu wamekuwa ni mabingwa wa kupoteza siku zao. Watu wako bize lakini hakuna kikubwa wanachoingiza wazungu wanasema busy for nothing. Changamoto ya zama hizi ni kwamba mitandao ya kijamii inawachangia sana kuwavuta watu kuvunja siku zao. Siku moja nilikuwa na mwadhiri wa chuo kikuu fulani, akaniambia yaani nikiamka nikishika …

Design a site like this with WordPress.com
Get started