Usihofie Kifo,Hofia Kuchelewa Kuishi Maisha

MEMENTO MORI..#03It is not death that a man should fear, but he should fear never beginning to live. - Marcus Aurelius Sio kifo ambacho mtu anapaswa kuogopa. Unapaswa kuogopa kwa ninihujaanza kuishi Maisha yako. Watu wanapoteza muda mwingi katika kufikiria kifo badala ya kuishi maisha. Usihofie kifo kwa sababu kifo kitakuja kwa namna yoyote ile …

Hakuna Siku Niliyofurahi Duniani Kama Hii

"Jana nilifurahi sana kwa sababu nimerudi nyumbani nimekuta mume wangu  amenisaidia kupika na kuogesha watoto. Ni kitu ambacho sijawahi kutegemea kufanyiwa na mume wangu. " PATA KITABU CHAKO CHA IJUE NJAA YA WANANDOA KWA SHILINGI 15000/= BADALA YA 20000/= Hayo ni maneno ya ushuhuda kutoka kwa msomaji wa kitabu cha Ijue Njaa Ya Wanandoa. Msomaji …

Hiki Ndiyo Chombo Cha Mfanyabiashara Yoyote Yule

Asili ya maisha yetu yanaendeshwa katika msingi wa biashara. Huwezi kupata kitu mpaka utoe kitu. Ni ngumu pale unapotaka kumsaidia mtu kitu halafu huna cha kumsaidia. Maisha yetu ni masoko na mauzo. Lazima tutengeneze mazingira ya kile tulichonacho ili kiweze kupokelewa na wengine. Chombo kikubwa cha mfanyabiashara ni thamani. Kama unataka kufanya biashara na huna …

Hakuna Kifo Kibaya Kama Hiki

Memento Mori#2Death is not the greatest loss in life. The greatest loss is what dies inside us while we live. - Norman Cousins Kifo kibaya na kikubwa ni kile ambacho watu huwa wanakufa na utajiri ndani yao wakati wakiwa hai.Kifo siyo kitu kikubwa kama kufa ukiwa hujatimiza ndoto yako ambayo iko ndani yako. Fikiria vitu …

Njia Sahihi Huleta Kitu Hiki Hapa

Mwalimu wa somo la hisabati alikuwa anatuambia kuwa ukitumia njia sahihi katika kufanya hesabu lazima itakuletea jawabu sahihi. Kumbe basi, njia sahihi sahihi lazima ilete jibu sahihi. Kwa chochote kile unachofanya, kama unafanya kwa njia sahihi lazima ilete jibu sahihi. Hakuna miujiza, bali ni kutumia njia sahihi ili upate kitu sahihi. Kitu ukikifanya kwa usahihi …

Hii Ndiyo Siku Utakayopaswa Kufunga Biashara Yako

Maisha yetu ni biashara. Kila kitu ni biashara hapa duniani. Kumbe basi, biashara haikwepi kama maisha yetu ni biashara. Malezi ya watoto ni biashara, watoto wanakuwa wateja kwa wazazi. Wazazi wakishindwa kupafanya nyumbani kuwa sehemu ya kutulia watoto hawatakaa nyumbani. Wazazi wakiwa ni wachokozi kwa watoto, biashara ya malezi kwa wazazi itakua ngumu. Mke au …

Ubongo Wetu Hauridhiki Mpaka Upate Kitu Hiki

Binadamu ni watu wa kuhusishanisha vitu. Kitu chochote kikitokea lazima binadamu watahusishanisha matukio. Kwa mfano, ajali ikitokea watu walikuwa sita na wakafariki watu wa 5 na kupona mmoja lazima huyo mmoja ataandamwa na watu kwamba yeye ndiyo aliwatoa kafara watu wenzake. Tukiachana na hilo, katika sehemu yoyote ambayo watu wanatoa fedha zao na wakitegemea kupata …

Hili Ndiyo Eneo Zuri La Kuwa Mbishi

Kwenye ubishi hakuna mtu ambaye anakubali kushindwa. Mtabishana lakini kila mtu atabaki kuwa katika kile anachoamini. Mabishano yako mengi, wako ambao wanabishania siasa, mpira wa miguu, na mengine ambayo sijayaorodhesha hapa. Unapobishana unakua unapoteza nguvu kubwa ambazo ungezielekeza kwenye uzalishaji ungekuwa mbali. Leo ninataka nikupe kazi ya kwenda kuwa mbishi kwenye eneo moja muhimu sana …

Tengeneza Mifumo Hii Ili Watoto Wako Waje Kufaidi

Kama wewe ulianzia sifuri yaani zero. Ulikuwa huna kitu, ukapambana na kufikia mafanikio ya juu, hakikisha unalinda kile ulichopata ili kizazi chako kisije kupata shida. Nguvu zako zisiende bure, fanya kazi mara moja na achia urithi kizazi chako. Na njia nzuri ya kuachia kizazi chako urithi ni kutengeneza mfumo imara. Usiwaachie watoto wako mzigo wakuja …

Design a site like this with WordPress.com
Get started