Kataa Rushwa Hizi Kama Unataka Kufanikiwa

"Mwandishi mmoja amewahi kuandika makampuni makubwa huwa yanawalipa vizuri sana vijana pale wanapoanza kazi ili kuzima ndoto zao, wakishakaa muda mrefu hawawalipi tena vizuri kwa sababu wanajua hawana tena ndoto kubwa au ujasiri wa kwenda kupambana wenyewe." Viko vitu ambavyo vimekuwa kama rushwa ambavyo vimewafanya watu wengi kutoziishi ndoto zao. Mshahara na marupurupu mbalimbali ni …

Tatizo Lako Ni Hili Hapa

Kama una tatizo lolote lile ambalo linaweza kutatuliwa na fedha basi hapo tatizo lako siyo tatizo ulilo nalo bali; tatizo lako ni fedha. Ukiona una tatizo na tatizo lenyewe ukiwa na fedha linaisha basi tatizo lako wewe ni huna fedha hivyo unatakiwa kutafuta fedha ili utatue tatizo ulilokuwa nalo. Ukishakuwa na fedha tatizo ulilokuwa nalo …

Wape Watu Kitu Hiki Utajua Kile Wanachopitia

Wape watu muda na utajua kile wanachopitia. Watu wanaweza kupitia mengi lakini huwezi kujua kile wanachopitia mpaka pale utakapowapa muda. Muda ni rasilimali muhimu sana ambayo huwa inatibu mengi kwenye maisha yetu. Ukimpa mtu muda atafurahia na atahisi una mthamini na atakua tayari kukuambia kile anachopitia. Watu wanaweza kuwa na mengi ya kukuambia lakini hawawezi …

Njia Ya Pekee Ya Kushinda Mabishano Yoyote Yale

Rafiki,Hata uwe na hoja nzuri kiasi gani ukishaingia kwenye mabishano tayari umeshakubali kushindwa. Ulishawahi kuona wapi watu wanabishana na baada ya hapo wanabadilisha misimamo yao? Watu huwa wanaamini kile wanachoamini hivyo hata mkibishana ni sawa na kazi bure. Pata picha watu wanabishana juu ya dini, siasa, michezo lakini baada ya hapo wanabadilisha misimamo yao? Kuna …

Kama Unataka Watu Wakukwepe Na Kukudharau Usiwe Hivi

Sisi binadamu ni viumbe vya hisia. Ukiwa ni mtu wa kujijali sana wewe mwenyewe bila kujali wengine watu watakuona wewe ni mbinafsi na itakuwa ngumu wewe kufanya jambo lako halafu wakubaliane na wewe. Kama unataka watu wakukwepe na kukudharau usiwe msikilizaji mzuri. Njia rahisi ya kuwashawishi watu wakubaliane na wewe ni kuwa msikilizaji mzuri na …

Ili Mapenzi Yake Yatimie

Siyo kila mtu anayeteseka ametenda dhambi. Ni akili za binadamu kuona mtu akiteseka basi anajua ametenda dhambi au amepatwa na laana. Wakati mwingine mtu anateseka na hana makosa aliyofanya lakini kiasili Mungu huwa anaruhusu mtu ateseke ili mapenzi yake yatimie. Huenda hata wewe kuna maumivu unayopitia, jua unapitia maumivu hayo ili uweze kuimarishwa kwa kitu …

Chochote Unachofanya Kifanye Kwa Namna Hii

Iwe ni kazi yako au ya mtu mwingine, kazi yoyote ile inayopita mikononi mwako ifanye kwa moyo na kwa ubora wa hali ya juu. Tunapimwa uwezo wetu kwenye kazi au kile tunachofanya. Ni bora ukafanye kwa ubora au usifanye kabisa. Kwa sababu kufanya kitu kwa namna ambayo ni ya hovyo ni kujidharirisha wewe mwenyewe. Waachie …

Epuka Kitu Hiki Kwenye Malezi Ya Watoto

Watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu. Watoto ni matunda ya ndoa. Watoto wenye maadili mazuri huwa wanatokea familia zenye maadili mazuri. Watoto wanakua bora pale ambapo wazazi wanakuwa bora. Shabaha yetu kubwa ya leo ni mzazi au mlezi kuepuka kuwalinganisha watoto. Usiwalinganishe watoto wako kwa sababu utakosa kujua upekee wao. Watoto huwa hawafanani hata siku …

Njia Ya Kushawishi Watu Kukubaliana Na Wewe

Ukitaka watu wakubaliane na wewe usiwakosoe. Kisaikolojia mtu akiona umeshamkosoa huwa anatafuta namna ya kujilinda. Watu wanataka wafanye ambacho wao wanaona wameamua wao kufanya maamuzi na siyo kulazimishwa. Kwa mfano, mtu mmoja alikuwa ni kiongozi wa kiwanda fulani alikuwa anawalazimisha wafanyakazi wa kiwanda hicho kuvaa kofia.Alikuwa anatumia mamlaka yake kila anapokutana na mtu ambaye hajavaa …

Vita Viwili Unavyopambana Navyo Kwenye Jamii Yako

Mafanikio ni kazi kweli. Kwenye jamii yetu yule mtu ambaye ameaua kubadilika na kuishi misingi yake na kuachana na maisha ya mkumbo huwa anachukiwa sana. Jamii yetu huwa haipendi kumuona mtu anayekwenda hatua ya ziada. Waambie watu unataka kuajiriwa na kulipwa mshahara wa kawaida hawatakua na shida na wewe. Waambie watu unataka kuwa tajiri na …

Design a site like this with WordPress.com
Get started