Usiendeshwe Na Mkumbo Kwenye Chochote Kile

Watu wengi kwenye jamii yetu huwa wanafanya maamuzi kwa kuendeshwa na silaha ya kufuata mkumbo yaani social proof. Watu hawana muda wa kufikiria na kuja na kitu cha ubunifu.Badala yake wanaangalia mwenzao wamefanya nini ili na wao wafanye. Na asilimia 5 ya watu duniani ndiyo wabunifu. Asilimia 95 ya watu duniani wanaiga tu nini ambacho …

Ushauri Wa Ndoa Kutoka Kwa Bilionea Charlie Munger

Charlie Munger ni Bilionea ambaye amefariki Novemba 28 mwaka 2023. Ni mtu ambaye ana hekima sana, alikuwa ni mzee aliyeishi miaka 99 alibakisha siku kadhaa tu kutimiza miaka yake 100. Huyu Munger ana madini kweli na ni mtu mwenye HEKIMA sana alikuwa anaitwa kitabu kinachotembea. Alikuwa ni mzee lakini bado alikuwa na ndoto kubwa ya …

Ni Wajibu Wako, Usiwalaumu Watoto

Kwa jamii zetu, wazazi wengi wanawasomesha watoto au kuwa na watoto ili waje wawasaidie baadaye.Ni kitu kizuri na matamanio ya wazazi wengi. Wazazi wanakuwa na matarajio mengi ambayo yanakuja kuwatesa hapo baadaye.Rafiki, hutakiwi kuweka mategemeo kwa watoto na usifanye kitu kwa sababu unataka urudishiwe. Mzazi ni wajibu wako kumsomesha mtoto shule nzuri na kumpa mahitaji …

Epuka Kuanza Siku Yako Na Vitu Hivi

Muda wa asubuhi ni muda ambao unapaswa kuulinda sana. Wakati mwingine, unaweza kujiharibia siku kwa sababu ya kuanza na vitu ambavyo havikupi ushindi. Epuka sana kuanza siku yako na vitu ambavyo vinakuharibia utulivu wako. Ukianza kujivuruga na vitu hasi asubuhi, utakua na siku ya hovyo sana. Epuka kuangalia au kusikiliza vitu hasi asubuhi. Hakikisha unailinda …

Ukiwa Na Kitu Hiki Shukuru Mungu

Huwa ninawashangaa watu ambao wanakuwa wanalalamika pale wanapokuwa na kazi nyingi.Mtu anaweza akawa anaomba kazi lakini akipata kazi anaanza kulalamika kwa sababu ya kazi kuwa nyingi. Ni kawaida ya binadamu, akiwa na kazi anaona haina maana na akikosa kazi anaona ina maana kwake. Huwa hatuoni thamani ya kitu pale tunapokuwa nacho ,ni mpaka pale kitakapoondoka …

Kazi Moja Ya Kiongozi

Sehemu yoyote inayoenda vizuri nyuma yake kuna kiongozi mzuri.Huwezi kuendelea kwenye eneo lolote lile kama sehemu hiyo hakuna uongozi mzuri. Uongozi mzuri unaanzia na kujiongoza wewe mwenyewe kwanza. Huwezi kuwaongoza wengine kama wewe mwenyewe maisha yako yamekushinda.Ukiweza kujiongoza wewe mwenyewe vizuri, hata wale unaowaongoza watakuchukulia wewe kama mtu wa mfano kwako. Kwenye kuwaongoza wengine, unapaswa …

Siri Moja Ya Mafanikio Kutoka Kwa Bilionea Charlie Munger

Mpendwa rafiki yangu nikupendaye, Hivi karibuni novemba 28, 2023 nilipokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Bilionea Charlie Munger ambaye alikuwa ni mtu ambaye najifunza mengi kutoka kwake. Ni Bilionea ambaye alikuwa anapendwa na watu wengi, alikuwa hana upinzani na watu wengine. Kwa sababu alikuwa ni mtu ambaye ana hekima sana na rafiki yake …

Fanya Kazi Na Watu Hawa Utafanikiwa Sana

Kwenye maisha ukifanya kazi na mtu ambaye tayari anaona ameridhika ni ngumu sana kukufanyia kile ambacho unataka tena kwa wakati. Watu walioridhika na mafanikio kidogo ni sumu kubwa kwenye safari yako ya mafanikio.Unapaswa kufanya kazi na mtu ambaye ana njaa ya mafanikio na siyo mtu ambaye ameshiba. Waswahili walishasema, mwenye shibe hamjui mwenye njaa.Fanya kazi …

Hii Ndiyo Maana Ya Mafanikio Kwako

Mafanikio yana maana tofauti kwa watu tofauti. Kwenye maisha usishindane na mtu kwa sababu kila mmoja ana maana yake kwenye. Unaweza ukahangaika kuwa kama wengine lakini baadaye unajikuta mtupu kwa sababu unaishi maana ya wengine na siyo yako.Ukijua nini maana ya mafanikio kwako, utakua unacheza mchezo wako mwenyewe.Na raha ya maisha ni pale unapokuwa unajua …

Hata Siku Moja Usiingiwe Na Hii Hali Kwenye Maisha Yako

Kwenye jambo lolote lile kwenye maisha watu huwa wanataka matokeo ya haraka. Watu wasipopata matokeo ya haraka, wanakuwa hawana subira hivyo wanajikuta wanakata tamaa. Hutakiwi kususa pale unapopata matokeo ya tofauti. Bali endelea kujisukuma zaidi kwenye kile unachofanya mpaka upate matokeo ya tofauti. Kushindwa ni kulipa ada. Hata kama hujapata matokeo mazuri kwenye kile unachofanya. …

Design a site like this with WordPress.com
Get started