Hiki Ndiyo Cheti Kikuu Kuliko Vyote Duniani

Mpendwa rafiki yangu, Huwa sisi binadamu tunapenda pale tunaposoma, kuwekeza, kufunga ndoa, kufanya kitu fulani tupewe cheti kama cha uthibitisho fulani. Ndiyo maana ukiwa na soma mafunzo yoyote unatamani sana umalize na upewe cheti chako mapema na hata ukienda kuomba kazi unaonesha cheti cha kuthibitisha kuwa wewe umehitimu mafunzo fulani. Tumekuwa ni watu wa kutafuta …

Kama Unataka Kiasi Kikubwa Cha Fedha, Badili Kwanza Kitu Hiki

Rafiki, Mara nyingi huwa tunapata kiasi kile kile cha fedha kwa sababu kuu moja. Hatujaziandaa akili zetu kupata kiwango kikubwa cha fedha ndiyo maana unaweza kumuona mtu akipata kiwango kikubwa cha fedha kuliko akili yake ilivyozoea atafuta namna ya kukiondoa abaki katika hali yake. Unatakiwa kuseti kiwango kikubwa cha fedha kwenye akili yako hata kama …

Hawa Ndiyo Misukule Ya Kiteknolojia

Rafiki yangu, Kadiri dunia inavyokuwa kwa kasi, ndivyo teknolojia inaongezeka na misukule wa mitandao wanaongezeka. Watu katika zama hizi wamekuwa bize a simu kutembelea mitandao ya kijamii, hawa tunawaita misukule wa kiteknolojia yaani cyber zombies. Wameshikwa na mitandao ya kijamii kiasi kwamba wamekuwa misukule yaani badala wao ndiyo waiendeshe mitandao imekuwa kinyume sasa, mitandao ndiyo …

Jinsi Ya Kufanikiwa Kwenye Kile Unachotaka

Je unataka kufanikiwa kwenye kile unachotaka? Tunashindwa kufanikiwa kwenye kile tunachotaka kwa sababu kuu moja hatufikirii kile tunachotaka muda wote. Tumepewa akili za aina mbili, ya kwanza ni yenye utambuzi yaani conscious mind hii ni ile inayohusika na kufikiri kwa kina. Na nyingine ni ile akili ambayo haina utambuzi, yaani subconscious mind hii huwa inakusanya …

Punguza Matumizi Haya Ya Kifedha Ili Uweze Kufanikiwa Kiuchumi

Mpendwa rafiki yangu, Bado suala la nidhamu ya fedha imekuwa ni tatizo miongoni mwa watu wengi. Hata uwe mtu unayepata kipato kikubwa kiasi gani na ukawa unatumia zaidi ya kile unachopata bado wewe ni masikini mkubwa. Watu wamekuwa ni watu wa kutumia kile walichopata mpaka kiishe kwanza. Hakuna falsafa mbaya kwenye matumizi ya fedha kama …

Hii Ndiyo Sehemu Ya Kuanzia Kama Hujui Wapi Kwa Kuanzia

Rafiki, Huwa tunataka kufanya jambo tunajiuliza tuanzie wapi? Tuna kuwa na maswali mengi sana juu yetu tukitaka kuanza kitu fulani. Wengine huwa wanakabiliwa na hofu ya kuogopa kuanza kitu fulani na kuona je watu watanichukuliaje? Neno kubwa ambalo napenda kukuambia kama ni mtu unayejishauri ni wapi utaanzia mimi nakuambia anzia hapo hapo ulipo. Hicho ulichonacho …

Kwanini Hupaswi Kufanya Kama Watu Wanavyotaka Wao

Kila siku unatakiwa kuishi maisha ya vile unavyotaka wewe kwa sababu wewe ndiyo mkurugenzi wa maisha yako. Tumekuwa watumwa wa kuishi maisha ya watu wengine na siyo vile tunavyotaka sisi. Na hii imetuletea maisha ya maigizo sana. Chochote unachotaka kufanya fanya kwa ajili yako na siyo kumfurahisha mtu yeyote yule. Maish ni mafupi sana kama …

Kazi Unayopaswa Kufanya Kila Siku Ili Kukuletea Mafanikio Makubwa

Mpendwa rafiki, Wote tunajua umuhimu wa kazi, ila sharti la kazi iwe halali na siyo vinginevyo. Usijisifie unafanya kazi kumbe kazi yenyewe siyo halali. Kuna kazi ambayo watu wengi sana hawaifanyi, kazi ambayo kila mmoja wetu akiifanya inamletea mafanikio makubwa kwenye maisha yake. Kazi unayopaswa kufanya kila siku ili ikuletee mafanikio makubwa siyo kazi nyingine …

Jambo Muhimu La Kulijua Katika Maisha Yako

Rafiki, Kila mmoja wetu anapaswa kujua kuwa jukumu la maisha yake ni lake mwenyewe na siyo la mtu mwingine. Hutakiwi kuwa laumu watu wengine kwa kile kinachotokea katika maisha yako. Maisha ni kama mwili wako, hivyo mwili wako unapokuwa na kitu fulani huwezi kumuachia mtu bali uwe mzima au unaumwa utaambatana na mwili wako. Utayabeba …

Njia Bora Ya Kujiandaa Kifedha Ili Kukabiliana Na Matukio Na Sikukuu Za Mwisho Wa Mwaka

Mpendwa rafiki yangu, Dunia huwa inatupa kalenda ya matukio ya karibu mwaka mzima. Hapo ulipo tayari umeshakuwa na kalenda yako na unajua tukio fulani ni lini au siku gani. Hivyo, kama umeshakuwa na utambuzi huo unatakiwa sasa uchukua hatua ya kujiandaa kukabiliana na hayo. Mwezi unaongozwa kwa matumizi makubwa huwa ni mwezi wa mwisho wa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started