Usiwe Mtu Wa Namna Hii Katika Maisha Yako

Mpendwa rafiki yangu, Mtu mmoja aliwahi kusema ni rahisi kuwaswaga kondoo na wakaenda katika mstari mmoja lakini ni ngumu kuswaga paka wakaenda katika mstari mmoja. Kuwaongoza binadamu ni kama vile paka, kila mtu atakwenda njia yake anayojua yeye, lakini kondoo ni rahisi sana kuwaongoza kwani wanafuata mstari mmoja tu. Katika maisha tunatakiwa tusiwe kama kondoo, …

Jinsi Ya Kufanya Mambo Yasiyowezekana

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna jambo au neno gumu lisilowekana hapa duniani. Kama limeshindikana kwako basi kwa mwingine linawezekana. Hakuna mtu ambaye anapewa jambo ambalo hawezi kulikabili. Yale yote unayokutana nayo jua yako ndani ya uwezo ndiyo maana umepewa. Unaweza kusema wewe huwezi lakini watu wengine wanaweza, kama kitu hujui chukua kama changamoto ya kujifunza ili …

Jinsi Ya Kumfundisha Mtoto Kwenye Uwezekano Wa Mambo

Mpendwa rafiki yangu, Wazazi wengi hawawafundishi  watoto wenye uwezekano wa mambo chanya. Utamaduni huu una waathiri sana watoto kutokuwa na uwezo wa kufikiri mambo katika fikra chanya. Kuna umuhimu mkubwa sana kila mzazi au mlezi kuwafundisha watoto katika uwezekano, watu wengi wanawafundisha watoto mitazamo hasi iliyoshindwa badala ya kuwafundisha mitazamo chanya. Kama wewe ni mzazi …

Hii Ndiyo Anuani Mpya Ya Mtandao Wa Kessy Deo

Habari rafiki, Leo kumekuwa kuna mabadiliko ya makubwa ya mtandao wetu wa kessy deo. Blog tayari imehamishwa kutoka kwenye mtaalamu.net/kessydeo kwenda kwenye http:kessydeo.home.blog. Makala zote zimehamishiwa kule hivyo kuanzia sasa hakuna tena mtaalamu na tutatumia link hii hapa kupata makala au kuingia moja kwa moja. Https://kessydeo.home.blog  Hakuna kitu kilichoharibika rafiki yangu, makala zitaendelea kuwepo kila …

Hiki Ndicho Kitakachotokea Pale Unatakaposhindwa Kumjali Mteja Wako?

Kama umeajiriwa basi unaauza muda na ujuzi wako hivyo kila mtu ana kitu cha kuuza. Na katika kuuza ni lazima pawepo na mteja bila mteja huwezi kuuza. Kila mtu anaishi hapa duniani kwa kuuza kitu fulani. Hakuna mtu ambaye ni hai hana anachouza, haijalishi umeajiriwa au umejiajiri. Kadiri ya Don Peppers, bila mteja huna biashara, …

Haya Ndiyo Mawazo Bora Duniani  Yatakayokusaidia Kuwa Na Mafanikio Makubwa

Uko hivyo ulivyo leo kutokana na maamuzi uliyofanya hapo awali. Kila mtu anapokea kadiri ya yeye alivyoamua kwenye maisha yake. Huwezi kupewa kitu ambacho wewe hujaamua kuwa nacho. Angalia maisha yako ya livyo utaona kuwa vitu vingi ulivyonavyo vinatokana na maamuzi uliyofanya. Huwezi kuwa vile unavyotaka kama hujaamua kufanya maamuzi ya vile unavyotaka. Sisi ndiyo …

Jambo Muhimu Ambalo Watu Wengi  Huwa Wanalisahau Katika Msamaha

Mpendwa rafiki yangu, Kwa kuwa sisi binadamu hatujakamilika, basi ndiyo maana hata kukawekwa msamaha. Mwasisi wa msamaha ni Mungu mwenyewe. Hivi kama ingekuwa hakuna msamaha je dunia ingekuwaje? Tungekuwa ni watu wa kulipizana visasi? Ingekuwa ni sheria ya jino kwa jino je tungeweza kuishi kweli? Kila siku ya maisha yetu huwezi ukamiliza siku bila kukosa …

Usiogope Kujaribu, Jaribu Halafu Iachie Sehemu Hii Ifanye Kazi Yake

Watu wengi wanaogopa kujaribu sana, na hili linawafanya watu wengi kuendelea kubaki pale walipo. Kama hujaribu kitu utawezaje sasa kuwa na maisha bora? Utakuwa kila siku ni mtu yuyule kama hutoamua kuchukua hatua za kujaribu. Kujaribu siyo kushindwa unapojaribu kitu ndiyo unajifunza. Wako ambao wanataka kuanzisha biashara lakini wanaogopa kuna kitu kinawazuia kuanza nacho ni …

Njia Mbili Za Uhakika Za Kupata Fedha Unazotaka

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna mtu ambaye hajui umuhimu wa fedha, fedha ni muhimu sana katika maisha yetu na hilo halina ubishi. Fedha ni jawabu la mambo yote. Fedha ni mbadilishano wa thamani, au tunaweza kusema fedha ni zao la thamani. Kwahiyo, ili uweze kupata fedha zaidi unahitaji kufanya haya yafuatayo; Kama unataka upate fedha, unatakiwa …

Ushauri Wa Mwanafalsafa Epictetus Kwa Mtu Yeyote Anayetaka Kufanikiwa

Heri ya mwezi agasti rafiki yangu, Natumaini hujambo na unaendelea vizuri. Niendelee kukutakia kila la heri katika mwezi huu wa nane tunaoanza nao leo. Unaweza kufanya kitu chochote leo na kubadilisha maisha yako. Zaidi ya miaka elfu mbili mafundisho ya wanafalsafa bado yako hai na yanaendelea kutumika katika jamii yetu. Licha  ya wanafalsafa hawa kuishi …

Design a site like this with WordPress.com
Get started