Hii Ndiyo Sehemu Pekee Ambayo Upendo Huwa Unapenda Kukaa

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna falsafa kubwa duniani kama upendo, ukiweza kuishi kwa upendo utaweza kushika amri zote. Karibu dini zote duniani zinashikilia falsafa ya upendo. Katika upendo tunapata kila kitu, upendo ndiyo asili ya dunia na tunapokwenda kinyume na upendo huwa tunapata shida. Kila mtu anajua ni kwa jinsi gani upendo ulivyokuwa na nguvu, kama …

Mbinu Bora Itakayokusaidia Kutoka Hapo Ulipo

Vita vikubwa ambavyo tunapaswa kuvitangaza ni vita dhidi ya miili yetu, hakuna upinzani mkubwa tunaopata katika maisha yetu kama upinzani wa miili yetu. Tusipokuwa makini na miili yetu basi tutaishia mahali pabaya sana. Miili yetu inapenda rah asana, inataka kile inachotaka bila sababu yoyote ile. Tukianza kuisikiliza miili yetu hakika hatutoweza kutoboa, hatutoweza kutoka hapa …

Jinsi Ya Kuwa Na Hekima Kwa Njia Rahisi

  Watu wengi wanaweza kujiuliza je nina wezaje kuwa na hekima? Hili ndiyo swali ambalo linaulizwa na watu wengi. Iko njia rahisi ya kuweza kuwa na hekima katika maisha yetu nayo ni kutumia akili. Kwa kuwa sisi ni binadamu tulioumbwa kwa jinsi ya ajabu tumepewa akili kubwa ya kuweza kujua zuri na baya. Kwa kutumia …

Huna Haja Ya Kuelezea Falsafa Yako

Mpendwa rafiki, Hatutakiwi kuyaanika maisha yetu hadharani, kila mtu ajue vile tulivyo. Unapoanika mambo yako na watu wakishakujua inakuwa si salama kwako tena. Huna haja ya kuelezea falsafa yako kwamba wewe ni mwanafalsafa wa ustoa au la. Unapochagua kuwa mwanafalsafa hutakiwi kuelezea na kusema kuwa wewe ni mwanafalsafa bali unatakiwa; Unatakiwa kuishi misingi ya kifalsafa, …

Hii Ndiyo Mbinu Bora Ya Kuvuta Upendo Kwenye Maisha Yako

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna kitu chenye nguvu duniani kama upendo, tunasikia hadithi mbalimbali za upendo kwenye maisha yetu. Lakini hebu tujiulize ni wangapi tunaishi ule upendo unaokusudiwa? Wengi wanaishi upendo wa mdomoni kuliko wa vitendo. Natumaini umeshawahi kuona au hata umeshawahi kufanya kisasi kinachokwenda kinyume na upendo. Kwa mfano, mlienda sehemu x baada ya kufika …

Huyu Ndiye Mtatuzi Wa Ndoa Nyingi Kwenye Zama Hizi

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna sehemu ambayo tunaweza kusema kuwa haina tatizo, yaani ni salama. Hata ukipita katika nyumba zetu, hakuna nyumba iliyoweka bango mlangoni kuwa HAPA HAKUNA TATIZO. Kila sehemu ina shida zake, japo shida zetu zimetofautiana. Kama hutaki shida kwenye eneo lolote la maisha yako, basi jua kabisa sehemu ambayo haina changamoto ya maisha …

Vitu Vitatu Vyenye Uraibu Au Uteja Mkubwa Duniani

Mpendwa rafiki yangu, Kila mtu huwa ana kitu anachopenda hapa duniani, kila mtu ana ulevi wake. Kwa lugha nyingine tunaweza kusema ulevi ni kama uraibu au uteja juu kitu fulani. Huwa tunatengeneza tabia na kisha tabia zinatutengeneza. Tabia ambazo huwa tunazianzisha zinatulea uteja katika maisha yetu. Hebu leo tuende tukajifunze vitu vitatu vyenye uraibu, ulevi …

Usijisumbue Na Mambo Haya

Rafiki, Siyo kila kitu unapaswa kuhangaika nacho, mambo mengine siyo hata ya kujisumbua kabisa. Unatakiwa kuyaacha mambo yatokee kama yalivyopangwa. Hutakiwi kuogopa na kujipa msongo wa mawazo kwa mambo yanayoendelea kutokea kwa sababu ni mambo ambayo huwezi hata kuyazuia. Hutakiwi kujisumbua na mambo ambayo yako nje ya uwezo wako. Bali unatakiwa kujisumbua na mambo ambayo …

Hii Ndiyo Faida Ya Kuwa Mwanafunzi Wa Maisha

  Ili ufanikiwe katika zama hizi hutakiwi kuboboea katika kitu kimoja. Bali unatakiwa kuwa mbobezi wa mambo mbalimbali. Kuchagua kubobea katika kitu kimoja zama hizi ni kama kuchagua kuwa na chanzo kimoja cha mapato ambayo ni hatari zaidi. Hutakiwi kujifungia katika eneo moja, bali kuwa na uwanja mpana, jifunze mambo kwa upana wake na siyo …

Haya Ndiyo Mambo Matatu Ambayo Hupaswi Kuwaambia Watu Wa Nje

Mpendwa rafiki yangu, Siyo kila kitu unapaswa kumwambia mtu, siyo lazima kila mtu ajue undani wa maisha yako. Pale watu wanapokuwa wanakuja undani wako ni rahisi kufanya kile wanachotaka kadiri ya taarifa ulizo nazo. Mambo matatu ambayo ni siri yako tu na hupaswi kuwaambia watu ni kama yafuatavyo; Kipato chako; usiwaambie watu juu ya kipato …

Design a site like this with WordPress.com
Get started