Usiwe Na Kinyongo

Kuna watu wanaamini kuwa wakiwasaidia watu wengine watafanikiwa halafu wao watapitwa. Hivyo wanakuwa na kinyongo pale wanapoona mtu mtu mwingine anapotaka kufanikiwa. Usiwe na kinyongo, ukimsaidia mtu na akafanikiwa huo ni ushindi tosha. Roho ya kimasikini ni ile ambayo haitaki kusaidia wengine na wakisaidia wengine wanakuwa na kinyongo. Kuna watu wengine kazi na furaha yao …

Kazi Ya Mbwa

Kama tunavyojua wote kwamba kazi ya mbwa ni kubweka. Ukitembea njiani ukikutana na mbwa akiwa anabweka wala hutomshangaa bali utampuuza tu kwa sababu unajua kazi yake ni kubweka. Kwenye maisha yako ya kila siku utakutana na watu wengi ambao wakibweka, yaani wakiendelea na maisha yao, wengine watakusema kwa namna moja au nyingine maneno yote unayoyasikia …

Kitu Kimoja Kinachomfanya Muuzaji Ajisikie Vizuri

Kwenye mauzo, muuzaji kama hauzi, anakuwa anajisikia vibaya. Siyo tu kujisikia vibaya lakini pia kukata tamaa na kuona kama vile hana bahati au ana kisirani. Lakini muuzaji anajisikia vizuri pale anapokuwa anauza. Kitu ambacho naweza kukuambia ni kwamba, kuuza ni raha. Kuuza raha kwa muuzaji wowote yule, mtu anapokuwa anauza na anaona mauzo anapata hata …

Nyota Njema Huonekana Asubuhi

Waswahili wanasema, nyota njema huonekana asubuhi, ni kweli nyota njema huonekana asubuhi.Lakini, kwenye maisha chochote kinaweza kutokea. Nyota njema inaweza isionekane asubuhi lakini ikaja kuonekana jioni. Kwenye biashara au maisha kwa ujumla muda wowote ule nyota njema huonekana. Inaweza kuwa asubuhi au jioni au wakati wowote.Unaweza ukakaa kwenye biashara siku nzima na usiuze, lakini kabla …

Yumba Lakini Usianguke

Pata picha ukimuangalia mtoto anayejifunza kuendesha baiskeli ya tairi mbili , huwa anaanza kwa kuyumba na kisha ndiyo ananyooka na kwenda na mwendo. Na hata ukishajua kuendesha baiskeli, huwezi kuanza na kunyooka moja kwa moja, lazima utayumba kwanza ndiyo unyooke kwenye mwendo. Hata maisha ndivyo yalivyo, hakuna kitu chochote kinachoanza kikiwa na ukamilifu. Kila kitu …

Una Kitu Gani Cha Kukusukuma?

Binadamu sisi ni watu wa kujali maslahi, tunafanya kitu pale tunapoona kuna maslahi tunayapata. Na kama hakuna kitu ambacho kinatusukuma kwenye jambo lolote lile ni rahisi sana kuishia njiani. Wewe kama mwanamafanikio unapaswa kuwa na kitu ambacho kinakusukuma kuchukua hatua. Huwa tunafanya pale tunapoona kuna kitu kinachotusukuma. Huwezi kuamka asubuhi na mapema kama hakuna kitu …

Njia Ya Kupiga Hatua Kwenye Maisha Yako

Hakuna kitu kibaya kwenye maisha yako kama mazoea. Mazoea ni kufanya kitu bila kuwa na ubunifu wowote ule. Kama unataka ushindwe mapema kwenye kila eneo la maisha yako, basi ingiza mazoea na utapata anguko mara moja. Chochote kile unachofanya, fanya kwa ubunifu na usifanye kwa mazoea. Njia ya kupiga hatua kwenye maisha yako ni kuwa …

Zifahamu Aina Mbili Za Sababu

Kuna aina mbili za sababuMoja, kuna sababu nzuri na mbili sababu ya kweli. Na sababu nyingi wanazokupa watu ni sababu nzuri, sababu za kweli wanazijua wao wenyewe. Ukiona mtu anakupa sababu ya kutokufanya jambo jua hiyo ni sababu nzuri ambayo anataka wewe uisikie lakini yeye mwenyewe ndani yake ana sababu nzuri inayomfanya akupe sababu. Kwa …

Kabla Hujaniangusha Tayari Nilishajiangusha

Huwa tunalalamika fulani kaniangusha, lakini hutakiwi kuruhusu mtu akuangushe bali wewe unapaswa kuishi falsafa ya ustoa. Unaweza ukawa unamdai mtu, anakuahidi kabisa nitakulipa kesho au baadaye na wewe unaamini hilo unamwahidi mtu mwingine kuwa utampatia kiasi fulani cha fedha. Siyo hilo tu, unafanya biashara mteja anakuahidi nitakuja usiwe na wasiwasi au nitanunua na wewe unaliweka …

Design a site like this with WordPress.com
Get started