Haya Ndiyo Malengo Makubwa Mawili Ya Visingizio

Mara nyingi mtafuta sababu huwa haishiwi sababu. Watu wengi wanaokuwa na visingizio huwa wana malengo yao pia. Hivyo leo kupitia makala yetu ya leo tunakwenda kujifunza malengo makubwa mawili ya watu wenye visingizio. Moja ni kujitetea baada ya kushindwa. Mtu anapokuwa ameshindwa anatafuta sababu nyingi ili kuhalalisha kushindwa kwake.Kwa mfano, kamuulize mwanafunzi yeyote aliyepata daraja …

Ujumbe Muhimu Kwa Waajiriwa Wote

Kama umeajiriwa jambo muhimu ambalo huwezi kulikwepa kwenye maisha yakoni ujasiriamali. Ujasiriamali ni jambo ambalo halikwepi kabisa iwe unataka au hutaki. Hutaweza kuajiriwa milele. Angalia kwa sasa una miaka mingapi halafu umebakisha miaka mingapi kustaafu kwa lazima. Hata kama unaipenda sana ajira yako jua ukifikisha miaka 60 utastaafishwa kwa lazima. Hivyo jiandae mapema kuanza kushughulika …

Usifanye Kikao Na Watu Wakiwa Katika Hali Hizi

Wakiwa katika hali ya uchovu. Watu wakiwa wamechoka hawatakupa umakini wao bali wataigiza tu kama vile wanakusikiliza ili umalize. Kutumia muda wa mtu nje ya ratiba. Kwa mfano, muda wa kutoka wa wafanyakazi halafu unaenda kuomba kuongea na wafanyakazi hao kwa ajili ya kuwasilisha jambo fulani. Hapa hutaweza kuvuna kitu zaidi ya kupoteza muda wako …

Usifanye Kikao Na Watu Wakiwa Katika Hali Hizi

Wakiwa katika hali ya uchovu. Watu wakiwa wamechoka hawatakupa umakini wao bali wataigiza tu kama vile wanakusikiliza ili umalize. Kutumia muda wa mtu nje ya ratiba. Kwa mfano, muda wa kutoka wa wafanyakazi halafu unaenda kuomba kuongea na wafanyakazi hao kwa ajili ya kuwasilisha jambo fulani. Hapa hutaweza kuvuna kitu zaidi ya kupoteza muda wako …

Huyu Hapa Anaona Juhudi Zako

Asili inaona juhudi zako. Na kawaida asili huwa haipendi deni la mtu. Inamlipa mtu kadiri ya thamani anayoitoa. Mungu anaona juhudi zako unazoweka katika kile unachofanya. Hivyo basi, hawezi kukuacha, endelea kumtegemea na kuweka kazi.Weka kazi na sala kwenye kile unachofanya na utafanikiwa ni suala la muda tu. Endelea kuweka bidii kwenye kile unachofanya kwa …

Muda Mzuri wa Kufanya Kazi Za Kutumia Akili

Zipo kazi nyingi zinazohitaji nguvu na akili. Ziko kazi ambazo zinahitaji umakini wako wa hali ya juu sana na hizi ni kazi ambazo hazihitaji usumbufu wa aina yoyote ile. Kwa mfano, kazi kama za kuandika ni kazi ambazo zinahitaji umakini wa hali ya juu. Unahitaji muda ambao hauna usumbufu. Muda mzuri wa kufanya kazi zinazotumia …

Hiki Ndicho Kitakachokutofautisha Na Wengine

Kama huna viwango ulivyojiwekea, jiwekee viwango. Kwa sababu watu wengi wanaishi lakini hawana viwango walivyojiwekea kufikia. Kwenye kila eneo la maisha yako, uwe na viwango ulivyojiwekea kufika na uweke kazi kuvifikia viwango hivyo. Jambo bora ni kuwa na viwango kisha kujitengenezea viwango ambavyo vitakuwa vinakuongoza. Viwango vinakuwa ni kama namba ambazo unatakiwa kuzifikia. Kwani bila …

Je, Ni Mapenzi Ya Mungu Kweli Kufanya Hivi?

Ni swali ambalo kila mtu anapaswa kujiuliza pale anapotaka kuomba au kufanya kitu fulani. Ukiomba chochote kile, jiulize, je haya ni mapenzi ya Mungu kweli? Jibu likiwa siyo acha. Hata kikiwa ni kizuri namna gani. Kwa sababu tunajikuta tunaingia kwenye mitego na kufanya vitu ambavyo si mapenzi ya Mungu bali mapenzi ya binadamu. Tunajua kabisa …

Usidharau Chochote Kile

Kwa sababu kila kitu kipo kwa sababu ya kukusaidia wewe mwenyewe. Kile ambacho unakitegemea kitakusaidia kinaweza kisikusaidie kabisa. Na kile ambacho unahisi hakiwezi kukusaidia ndiyo kinaweza kukusaidia. Heshimu kila kitu kwa sababu kila kitu kina maana yake ndiyo maana kipo. Vizuri au vibaya vyote viko kwa ajili ya kukamilisha ukamilifu wa dunia. Jifunze namna dunia …

Kama Hujui kitu, Usiogope Fanya Hiki Hapa

Kama hujui kitu, hujui kitu cha kufanya wala usiogope. Bali jifunze. Aliwahi kusema mwandishi Ayn Rand. Kama hujui kitu rafiki yangu wala usiogope chukua hatua kujifunza. Hakuna mtu anayejua kila kitu. Kila mtu ana ujinga eneo fulani, ukiona eneo fulani hauko vizuri jifunze kile ambacho hujui. Usijisifie kuwa hujui kitu, bali jisifie kwa kuchukua hatua …

Design a site like this with WordPress.com
Get started