Usifanye Kwa Sababu Hii Hapa

Kwenye maisha wakati mwingine huwa tunafanya vitu kwa sababu tunaona au kusikia wengine wakifanya. Kwa sababu fulani anachelewa, haimaanishi na wewe uchelewe. Kwa sababu isikuharibie sifa nzuri ulizonazo. Endelea kuwahi kazini. Kwa sababu watu wengi hawasomi vitabu, haimaanishi na wewe usisome vitabu. Soma kwa faida, acha kufuata mkumbo wa watu kila mtu kaja kutengeneza historia …

Jambo Muhimu La Kuzingatia Katika Maisha Ya Wanandoa

Nilipokuwa nasoma kitabu The Prohet kilichoandikwa na Khalil Gibran nilikutana na sentensi moja ambayo nimependa kukushirikisha siku hii ya leo, katika shairi hilo kuna mahali mwandishi anawashauri Wanandoa kuwa imbeni na kucheza pamoja kwa furaha lakini kila mmoja awe na wakati wa peke yake. Ni kweli, maisha ya ndoa yanahitaji muda mwingine uwe na wakati …

Jinsi Ya Kuacha Alama Itakayokumbukwa Na Watu

Iko wazi kabisa siku tunavyokufa hatutaondoka na kitu chochote kile. Ni kweli, iko njia ya kuacha alama kwa watu, huwezi kuondoka na vitu ulivyopokea duniani bali unaweza kuondoka na vitu ulivyotoa duniani. Watu hawatakukumbuka kwa vitu ulivyopokea duniani bali watakukumbuka kwa vitu ulivyotoa duniani. Ukitaka watu wakukumbuke toa zaidi. Huwezi kugusa maisha ya watu wengine …

Kwenye Maisha Yako, Hakikisha Unakuwa Na Kitu Hiki

Hakikisha unakuwa na viwango vya juu. Yaani kwenye kila eneo la maisha yako jiwekee viwango vya juu. Ukishajiwekea viwango vya juu kabisa usikubali chochote chini ya viwango vyako. Kwenye maisha huwa unapata kile unachokubali na siyo kile unachostahili. Jiwekee viwango vya juu kabisa vya ufanyaji na hakikisha unajisukuma kila wakati kuvifikia viwango hivyo. Kwa sababu …

Andaa Mazingira Yako Mwenyewe Wala Usimtegemee Mtu Huyu Hapa

Sisi binadamu kiasili ni wabinafsi. Huwa tunaanza kujifikiria sisi wenyewe kwanza ndiyo tunawafikiria wengine baadaye. Wako baadhi ya wazazi wanayo dhana kwamba wanazaa watoto ili wale watoto waweze kuja kuwasaidia baadaye. Ni mawazo mazuri kweli wako ambao wanafanya hivyo na watoto walio wazaa wanakuja kuwasaidia. Lakini baadhi ya wazazi wanafikia mahali wanajuta na kusema kweli …

Jinsi Ya Kumuona Mungu

Siku moja mama Theresa wa Calcutta alikuwa anamlisha mgonjwa chakula. Mgonjwa yule alipokuwa analishwa chakula alikuwa anamtapikia mama Theresa wa Calcutta. Waandishi wa habari wakamuuliza unawezaje kumlisha chakula mgonjwa anayekutapikia bila manung'uniko?Mama Theresa akawajibu waandishi wa habari, kupitia hiki nachofanya ninamuonda Mungu. Mpendwa rafiki yangu, unaweza kumuona Mungu kupitia kile unachofanya, kama unakifanya kwa moyo …

Design a site like this with WordPress.com
Get started