Vunja Laana Zote Ulizobeba Kwenye Eneo Hili

Ni kwenye eneo la kipato na fedha kwa ujumla. Watu wengi wamekuwa na faraja fulani katika eneo la fedha au kipato kwa ujumla. Kwa mfano, kila mmoja wetu ana kiwango chake cha fedha ambacho akishakipata akili yake inatulia na kuridhika lakini asipokipata akili yake inakuwa haiko sawa. Jambo ambalo huwa lishangaza kwenye jamii zetu ni …

Mbinu Ya Kuuza Sana Bidhaa Kwenye Biashara

Ukijua namna ya kuisoma saikolojia ya binadamu na kutumia hisia zake vizuri utakua mtu unayeuza sana. Kama una biashara na una bidhaa ambayo unataka itoke sana kwenye eneo lako la biashara labda duka, ukitaka watu wainunue haraka sana iweke usawa wa macho. Weka bidhaa kwenye usawa wa macho ili kila mtu anapoangalia awe rahisi kuiona. …

Kama Unaitaka Fedha Ije Kwako

Ipende fedha na ifanye kuwa rafiki yako. Kwa vyovyote vile, usiibeze wala usiidharau , wala kujifanya hutaki fedha kwa sababu fedha ni muhimu sana kwenye maisha yetu ya kila siku. Watu wengi hawafanikiwi na fedha inawakimbia kila mara kwa sababu hawaipendi na hawajaifanya kuwa rafiki yao. Fedha huenda kwa mtu ambaye anayeipenda na ambaye anajua …

Usijiwekee Ukomo Kwenye Maisha Yako

Narudia tena, usijiwekee ukomo. Umekuwa ni mtu wa kujiwekea ukomo kwenye kila eneo la maisha yako. Akili yako imekuwa inapokea ukomo ndiyo maana unapata matokeo yale yale kila siku. Maisha hayajakuwekea ukomo, ila wewe ndiyo umejiwekea ukomo. Umejiwekea ukomo kwenye kipato, labda wewe ni mtu wa kipato fulani, akili yako huwa ni kama raba bendi …

Jinsi Ya Kuongeza Kipato Chako Mara Mbili

W. Clement Stone aliwahi kunukuliwa akisema, wewe ni zao la mazingira yako. Hivyo chagua mazingira ambayo yanakutengenezea kuwa kama unavyotaka. Je, watu na vitu vinavyokuzunguka vinakusaidia kuyafikia mafanikio au vinakuzuia? Iko wazi kabisa, ukichukua wastani wa watu watano unaokaa nao muda mrefu utapata kipato chako. Je, unakaa na nani muda mrefu? Angalia wale unaokaa nao …

Maajabu; Unajipenda Lakini Huthamini Kitu Hiki Hapa

Watu wanajipenda kweli lakini wanasahau kitu kimoja ambacho ni maajabu kweli. Siyo mimi peke yangu ninayeshangaa hata aliyekuwa mtawala wa Roma na mwanafalsa ya ustoa mwanafalsa Marcus Aurelius anashangaa iweje watu wanajipenda wao wenyewe lakini utashangaa hawajali maoni yao bali wanajali maoni ya wengine kuliko ya kwao? Unajipenda lakini huthamini maoni yako. Iweje ujipende wewe …

Bila Kutengeneza Faida Biashara Itakufa

Kazi kubwa ya biashara yako ni kutengeneza masoko. Ukishakua na masoko lazima utapata mauzo na faida. Fanyia kazi masoko na jua ni mbinu gani unatumia kupata wateja. Hakikisha katika masoko unakuwa unajua idadi ya wateja wanaofanya manunuzi. Yaani ni wateja wangapi wananunua na akinunua basi mshawishi mteja arudi tena kupata huduma siku nyingine. Mteja anunue …

Kuwa Mtu Wa Namna Hii Kama Unataka Kupiga Hatua Kubwa

Iko kauli moja ambayo nimejifunza hivi karibuni inayosema, ni rahisi kuyavumilia maisha magumu kuliko kupambana kupata maisha bora. Unapata nini kwenye kauli hiyo? Hapo anamaanisha kwamba, ni kazi zaidi kupambana kupata maisha bora kuliko kuvumilia maisha magumu. Hii iko wazi kabisa kwenye maisha, angalia watu wengi wana maisha magumu na hakuna hatua za tofauti wanazochukua …

Fanya Vitu Hivi Viwili Vya Msingi

Kujifunza bila kuchukua hatua ni sawa na kujiburudisha tu. Utafurahia kusoma kitabu kizuri, makala nzuri na kupata mafunzo mbalimbali mazuri lakini maisha yako hayawezi kubadilika kama na wewe mwenyewe hutabadilika na kuingia kwenye vitendo. Fanya vitu hivi viwili vya msingi kila siku; Moja, jifunze kila siku. Kwa kuwa unaendelea kuishi hakikisha unajifunza kila siku na …

Kila Kitu Kinapita

Unapojikuta kwenye mazingira ambayo ni magumu, unapoona mambo hayaendi, jua kabisa hakuna kinachodumu. Kila kitu kinapita. Lakini, ipo tiba moja ya kila kitu kinachotokea au kuendelea kwenye maisha. Tiba hiyo moja ni muda. Kila kitu kinapita, hakuna chochote kinachodumu milele hata wewe mwenyewe. Wewe siyo mti, unao uwezo wa kuondoka popote pale ulipo. Unao uwezo …

Design a site like this with WordPress.com
Get started