Hii Ndiyo Huduma Unayopaswa Kumpa Mteja Wako

Kipimo kizuri cha huduma bora kwa mteja ni kujipima kwa sentensi hii"Mara zote nitampa mteja huduma ambayo mimi mwenyewe ningejipa kama ningekuwa mteja huyo" Kuna wakati tunawahudumia wateja wetu lakini hatuwapatii huduma bora. Na watu wengi hawatoi huduma bora ndiyo maana hawafanikiwi. Watu wanaangalia wanapataje fedha kabla hawajaangalia wanasaidiaje kwa kutoa huduma bora. Mafanikio yoyote …

Usikatae Uhalisia

Magonjwa mengi ya akili yanasababishwa na mtu ambaye anakataa ukweli au uhalisia.Usibishane na uhalisia hata siku moja. Pokea uhalisia kama ulivyo na ishi nao. Unapokataa yale ambayo yanakukuta unakuwa unajiandaa kupata magonjwa ya akili. Unakataa kuachwa, unakataa mtu kufa, unakataa kufungwa, na mengine mengi yanayofanana na hayo. Jambo likitokea, lipokee kama kilivyo na jifunze namna …

Kama Ameshindwa Kujihurumia Je, Wewe Utaweza?

Siku zote upendo huwa unaanza na mtu kujipenda kwanza yeye mwenyewe. Kama mtu yeye mwenyewe hajipendi unafikiri wewe ndiyo utaweza kufanya hivyo? Kama mtu hajihurumii yeye mwenyewe, je, wewe utaweza kumhurumia? Kwenye maisha huwezi kumzuia mtu anayetaka kujiua, mtu kama ameamua kujiua atajiua hata ufanye nini. Hii ina maana kwamba, nguvu ya ndani ya mtu …

Usiwe Na Wasiwasi

Akili huwa haifanyi kazi pale hisia zinapokuwa juu na fikra zinapokuwa chini. Fikra zinapokuwa chini, mtu anakuwa anafanya maamuzi ya ajabu na baadaye kuja kujutia. Ndiyo maana, haishauriwi kabisa kufanya maamuzi ukiwa na hisia. Jicheleweshe kufanya maamuzi mpaka pale hisia zinapokuwa chini au zimeisha. Ukiwa na changamoto yoyote ile wala usiwe na wasiwasi, tulia kwani …

Ondoka Kwenye Vikundi Hasi

Ni kawaida yetu sisi binadamu kupenda kuonekana kuwa ndani ya kundi fulani. Tunapokuwa ndani ya kundi huwa tunajisikia vizuri, pale tusipokuwa ndani ya kundi huwa tunaona kama vile tumepotea. Swali muhimu la kujiuliza uko kwenye kundi gani? Kama uko kwenye kundi lolote ambalo halina manufaa kwako, ni kundi hasi badala ya kujadili mambo chanya yanayojenga, …

Changamoto Moja Kwenye Kujifunza

Aliyekuwa baba wa falsafa Mwanafalsafa Socrates aliwahi kunukuliwa akisema hekima pekee ambayo ninayo, ni kwamba sijui kitu. Wakati huo Mwanafalsafa Socrates ndiyo mtu ambaye alikuwa anaonekana anajua sana lakini watu wakimuuliza anasema anachojua ni kwamba hajui kitu. Hii ina maana gani kwetu? Ni kujishusha na kuwa mnyenyekevu na kuwa tayari kutaka kujifunza tena. Sina uhakika …

Huyu Ndiyo Muuzaji

Kila mtu ni muuzaji.Muuzaji ni yule anayemshawishi mwenzake. Kitendo cha wewe kuweza kumshawishi mwenzako kukubaliana na wewe huo ni uuzaji. Siyo lazima anunue bidhaa, ila hata kukubaliana na wewe tu kimawazo ni uuzaji.Uuzaji ni kitendo cha kubadilishana imani. Kifupi, uuzaji ni mbadilishano wa imani, mmoja anamshawishi mtu ili aweze kukubaliana na kile anachokiamini.Ukisema wewe siyo …

Usiangalie Changamoto Unazopitia

Kwenye maisha hakuna eneo ambalo unaweza kwenda na unakuta hakuna changamoto. Au ulishawahi kuona nyumba gani iliyobandika bango mlango lenye ujumbe huu hapae. HAPA HAKUNA MATATIZO.?binafsi sijawahi kuliona hilo bango. Hii ina maana gani kwetu? Ina maana kwamba, hakuna sehemu ambayo ni salama hapa duniani. Kila sehemu ambayo unafikiria ukifanya kazi ndiyo utakutana na bango …

Huwezi Kukimbia Mchakato

Warren Buffett amewahi kusema huwezi kupata mtoto ndani ya mwezi mmoja kwa kuigawa mimba moja kwa wanawake 9. Mimba lazima ichukue miezi 9 kukamilika kuwa mtoto. Ili uweze kufanikiwa kwenye jambo lolote lile, unapaswa kukaa kwenye mchakato wa kile unachotaka. Usikimbilie matokeo kabla hujakaa kwenye mchakato. Kama tulivyooona kutoka kwa Warren Buffett, huwezi kurahisha kazi …

Design a site like this with WordPress.com
Get started