Watu Wote Wanaofanya Wanatumia Mbinu Hii Hapa

Kwenye maisha kuna vitu ambavyo havina mjadala na kuna vitu ambavyo vina mjadala ili vifanyike. Kwenda kujisaidia, kula, kulala, kupiga mswaki ni vitu ambavyo haviitaji mjadala ikishafika wakati wake unafanya tu, hujiulizi nikajisaidie au nisiende. Lakini sasa, INAPOKUJA kwenye vitu vya maana ambavyo vinatupa fedha kama kazi, biashara au hata kusoma vitabu na kujifunza kuwa …

Njia Bora Ya Kuwahamasisha Watu

Kama unataka kuwahamasisha watu wafanye kile unachotaka unapaswa kutumia mbinu hii. Kwanza unapaswa kujua kiasili sisi binadamu ni wabinafsi, tunaanza kujali maslahi yetu ndiyo kisha wanafuata wengine. Tunaanza kuona tunapata nini kisha ndiyo tunafanya. Ili uweze kufanikiwa, unapaswa kucheza na akili za watu, unapaswa kujali kwanza maslahi yao kisha unatumia hayo hayo maslahi yao kuweza …

Tambua Mchango Wa Bahati Kwenye Mafanikio Yako

Mafanikio huwa yanadanganya sana na ndiyo maana wengi huanguka vibaya baada ya kufanikiwa.Hiyo inatokana na kiburi ambacho watu wanakipata wanapofanikiwa, kwa kuona ni kwa ujanja wao. Ni mpaka pale wanaporudia tena walichofanya na wanashindwa vibaya. Lakini kwa kiburi walichopata, wanaendelea kurudia tena na wanazidi kushindwa. Kuna mchango mkubwa wa bahati kwenye mafanikio yoyote ambayo mtu …

Njia Nzuri Ya Kuepuka Mabishano Na Watu

Kwenye maisha utakutana na watu ambao wanaamini tofauti na unavyoamini wewe. Unaweza kuona wewe upo sahihi zaidi yao na hata kubishana nao, lakini hilo halitakusaidia. Maana watu wakishaamini kitu, hata uwape ushahidi gani, bado hawatabadili imani zao kirahisi. Hivyo basi, ili kuweza kuelewana na watu hawa na kushirikiana nao, jiweke kwenye upande wao. Chagua kutetea …

Kama Biashara Ina Watu Hawa Itakua

Biashara huwa haishindwi kwa sababu ya bidhaa au huduma inayotoa bali huwa inashindwa kwa sababu ya watu ambao inao.. Kama biashara ina watu sahihi itakua. Lakini kama haina watu sahihi itakufa. Chagua watu sahihi wa kufanya nao kazi. Biashara inajengwa na watu walio ndani ya biashara hiyo, kama watu ni sahihi itaendeshwa vizuri na kama …

Kitu Ambacho Watu Wanapenda Kuambiwa

Rafiki yangu nikupendaye, Kama unafanya kampeni ya kugombania nafasi ya kitu fulani labda unataka ubunge, udiwani au uraisi, halafu unasimama mbele ya kadamnasi na kuwaambia, nyie hamjafanikiwa kwenye maisha yenu kwa sababu hizi tatu,Moja, uzembe,Mbili, uvivu na tatu,Ujinga. Unafikiri mtu ambaye anataka nafasi atapata? Watu ukiwaambia ukweli wala hawakupi kura yako lakini ukiwadanganya watakupa kura …

Raisi Amepita Na Gari La Kifahari

Ukimuona raisi amepita na gari la kifahari wala hutaumia wala kuona wivu, utachukulia tu ni hadhi yake au ana stahili kufanya hivyo kwa sababu ya nafasi yake. Lakini, ikitokea mtu ambaye mmesoma naye au mnayefahamiana amepita na gari la kifahari utashangaa ghafla wivu unaanza kukuungia. Wivu ni hali ya kujiona wewe unastahili zaidi kupata kuliko …

Sababu Namba Moja Ya Kukosa Ushawishi

Unahitaji ushawishi ili uweze kukubalika na kukubaliana na watu wengine juu ya jambo fulani.Ushawishi ndiyo unawashawishi watu wengine wakubaliane na sisi. Watu wengi wanapoteza ushawishi ni kwa sababu hawajiheshimu na kujiamini. Jiheshimu na watu watakuamini. Kwa kitendo cha kutokujiamini, watu WANASHINDWA kusimamia kile wanachotaka. Wanajikuta wakitaka kuwaridhisha wengine na hapo wanapoteza ushawishi. Ukishajikuta uko upande …

Waambie Watu Kitu Hiki

Kuna wakati unaweza kujiona kama vile dunia ina kisirani na wewe lakini ukija kuchunguza utakuja kugundua kwamba tatizo siyo dunia bali tatizo ni sisi wenyewe kwa kushindwa kukaa kwenye mchakato wa kile tunachotaka. Watu wengi wana bidhaa, wana kitu ambacho wanakiuza lakini watu hawajui kama wanauza. Wanalalamika hawauzi siyo kwamba wateja hakuna tatizo biashara haijulikani. …

Kauli Ya Uchumi Mgumu

Kauli ya uchumi mgumu haitokuja kuisha kamwe. Ndiyo wimbo ambao watu wanapenda kuimba. Watu kusema uchumi ni mgumu wala haijaanza leo, hata kama uchumi ni mzuri watu watasema uchumi mgumu. Ile ya wateja kusema hali mbaya ni kawaida kuisikia kila mara, hata mteja awe na hela, kauli pendwa kwake ni uchumi mgumu. Mtu akitaka kukutoroka …

Design a site like this with WordPress.com
Get started