Unao Uwezo Wa Kusema Hapana Kwa Mambo Haya

Mwanamafanikio, Kwenye maisha unayo nguvu ya kusema hapana kwa vitu ambavyo hujavipenda. Kwa mfano, unaweza kusema hapana usichopenda. Kama kuna watu ambao hupendi kukaa nao kwa namna wanavyofanya mambo yao, Una uwezo wa kusema hapana na ukakaa na wale unaowapenda. Kama kuna kazi unafanya ambayo huipendi na haiendani na uwezo au vipaji vyako, Una uwezo …

Jinsi Ya Kuwa Bora Kwenye Kitu Chochote Kile

Mpendwa rafiki yangu,Huwezi kuwa bora kwenye kitu chochote kile kama wewe mwenyewe siyo bora.Na ili uweze kuwa bora unapaswa kuwa mtu wa kujifunza kila siku kwenye kile unachofanya. Kila wakati unapaswa kujifanyia maboresho kama vile mitandao ya kijamii ilivyo, kila wakati lazima uwe na toleo jipya ili upate vitu vizuri.Usipojiboresha huwezi kupata ushindi kwenye kile …

Ukisikiliza Sababu Za Watu, Hutoboi

Wakati naanza kuandika, nilipokea vipingamizi vingi sana, kutoka kwa marafiki, jamaa, na hata watu wangu wa karibu.Rafiki, chochote utakachoamua kufanya, wako ambao watakupinga hata kama ni kitu kizuri lakini pia wako ambao watakuwa na wewe kwa hali zote.Na huwezi kulizuia hili kwenye maisha kwa sababu ni asili za watu ndivyo ilivyo. Kwa mfano, hata mtu …

Anza Na Wewe Mwenyewe

Pale tu unapoamka jiambie maneno ya ushindi kama vile wewe ni mshindi na umezaliwa kushinda. Yaani jiambie, MIMI NI MSHINDI, NIMEZALIWA KUSHINDA. Mara nyingi watu huwa wanajizuia wao wenyewe kabla hata hawajaanza. Mara nyingi ushindi huwa unaanzia ndani ya mtu kabla haujatoka nje. Usikubali kuanza kushindwa kabla hata hujaanza. Unakubali kushindwa kabla hujaanza ndani yako …

Huwezi Kupokea Simu Isiyoita

Mpendwa rafiki yangu nikupendaye, Kwenye maisha kila kitu kinatokea kwa sababu. Hakuna kitu ambacho kinatokea bila sababu. Hata sheria ya matokeo na visababishi inasema hivyo. Kitu kitatokea mpaka pale kitakaposababishwa. Kwa mfano, jiwe haliwezi kwenda mahali mpaka mtu aje kulisogeza. Katika hali ya kawaida, huwezi kupokea simu ambayo haijaita. Ili uchukue simu na upokee sharti …

Kama Huamini Kile Unachouza Huwezi Kuuza

Mpendwa rafiki yangu nikupendaye, Watu wengi wanashindwa kuuza kwa sababu wao wenyewe siyo mashambani namba moja kwa kile wanachouza.Yaani kama unauza kitu, wewe kama muuzaji ndiyo unapaswa kuwa na imani ya juu kuhusu kile unachouza kiasi cha wateja kutokuwa na shaka juu ya huduma au bidhaa unayouza. Chochote kile unachouza wewe ndiyo unakuwa mnunuaji namba …

Umejipata Au Unajitafuta ?

Mpendwa rafiki yangu nikupendaye, Kama unataka kujipata unatakiwa kufanya mambo mengi kisha kupitia mambo hayo mengi unachagua kitu kimoja ambacho uko vizuri na hapo unakuwa umejipata. Ukishajipata, unapaswa kutulia na kile ambacho umejipata nacho. Siyo umejipata kisha unaendelea kujitafuta na mahangaiko mengine mengi. Watu ambao wana mafanikio makubwa, huwa hawahangaiki na vitu vingi bali unakuta …

Kama Huingizi Fedha Tatizo Linaanzia Hapa

Mwanamafanikio, Utaweza kupata kile unachotaka kwenye maisha yako kama utaweza kuuza zaidi. Kama huoni fedha zikiingia, shida inaanzia kwenye mauzo. Maana yake huuzi. Kama unataka kupata fedha, basi uza zaidi. Kila mtu ni muuzaji, kila mtu anapaswa kuuza. Ukiona huna fedha jiulize, naweza kuuza nini. Jiulize utawezaje kuwasaidia watu ili upate unachotaka kwenye maisha yako? …

Jinsi Ya Kufanya Yale Muhimu Zaidi

Kwa dunia ya sasa, usipokuwa na kipaumbele, kila kitu kwako kitakuwa kipaumbele. Kwa sababu mambo ya kufanya ni mengi hivyo ni muhimu sana kuwa na fokasi kwenye yale ya msingi ili uweze kupata matokeo. Una mambo mengi unayotaka kufanya kuliko muda ulionao wa kuyafanya. Kitu pekee kitakachokuwezesha kufanya yale muhimu ni kuwa na kipaumbele kwenye …

Kama Haileti Jibu Sahihi

Wakati unasoma hesabu, ukitumia njia sahihi lazima ilete jibu sahihi. Njia sahihi siku zote lazima ilete jibu sahihi. Kama njia sahihi haileti jibu sahihi basi kuna mahali utakua unakosea. Usilalamikie njia mbona haileti jibu sahihi kwako wakati kwa wengine inaleta. Kaa chini na jitathimini namna unavyotumia hiyo njia unaitumia kwa namna gani. Kitu chochote sahihi …

Design a site like this with WordPress.com
Get started