Kusamehe Siyo Kusahau

Pata picha mtu anakuja anakukata mkono wako na kukuachia jereha ambalo unaliona maisha yako yote. Katika hali ya kawaida utaweza kumsamehe mtu huyo na kusahau? Ni ngumu kusahau kwa sababu lile jeraha kila ukiliona ,utalikumbuka.Hivyo basi, kusamehe siyo kusahau bali kusamehe ni kupotezea au kupuuzia tu. Mtu anaweza kukusamehe kwa kosa ulilotenda, lakini hawezi kusahau …

Kinachomaliza Fedha Zako

Rafiki, Safari moja huanzisha nyingine. Pale tu unapoanza kufanya matumizi ya vitu mbalimbali, inakuwa inaongezeka. Ni kama ukisema ndiyo moja kwenye matumizi, unakuwa umefungulia mlango wa matumizi. Kinachomaliza fedha zako siyo kitu kingine bali ni matumizi. Na kazi ya fedha ni matumizi. Na siyo kila matumizi unapaswa kufanya.Kuna matumizi mengine unafanya kwa sababu tu ya …

Hii ndiyo Asili Ya Binadamu

Kuna kitu ambacho huwezi kukizuia kwa binadamu. Na kitu hicho ni upendeleo. Upendeleo ni asili ya binadamu. Hata ufanye nini, kuna watu utajikuta tu unawapendelea kwa sababu ni asili ya binadamu. Usishangae kuona watu wakipendelewa, jua anayependelea anafanya hivyo kwa sababu ni asili yake kufanya hivyo. Hata kama kuna upendeleo, ni muhimu sana kuweka utaratibu …

Watu Huwa Hakosi Hili

Watu huwa hawakosi huku kwenye kila jambo. Hivyo ukiwa unafanya mambo yako kwa kutegemea watu, utapata shida. Usifanye kitu kwa kutegemea watu watasemaje. Jua hata ufanye kitu kizuri au kibaya watu hawawezi kukosa maoni. Usihangaike na maoni ya watu. Wewe angalia kile unachofanya kwako ni sahihi? Kama ni sahihi endelea nacho. Kwenye haya maisha lazima …

Maana Halisi Ya Mtu Anayekata Tamaa

Rafiki yangu nikupendaye, Ukiona mtu anakata tamaa, maana yake hataki kile anachotaka. Mtu ambaye anakitaka sana kile anachotaka, hawezi kukata tamaa. Atapambana kwa kila namna kuhakikisha anapata ushindi.Pambana sana mpaka upate kile unachotaka, chochote kile kisikuzuie kupata ushindi, shambulia mpaka upate ushindi. Kama hujapata kile unachotaka, iweje sasa ukate tamaa? Mtu anakata tamaa na kuishia …

Hata Kama Hujisikii Kufanya

Kuna siku unaamka ukiwa na hamasa ya kufanya kile ulichopanga kufanya. Kuna siku unaamka wala hujisikii kufanya kazi na huna hamasa. Ni kawaida kabisa kwa binadamu kupitia hali kama hiyo. Huwezi kuwa vizuri kila siku. Hamasa huwa hazidumu. Wewe kama mtu makini, hautakiwi kuripoti sababu, bali kuripoti matokeo mazuri. Hata kama hujisikii kufanya, wewe fanya …

Bado Hujashindwa

Mara nyingi watu wanaposhindwa kufanya kitu, huwa wanajiona wao ndiyo wameshindwa. Wanaanza hata kujichukia wao wenyewe.Lakini hilo siyo kweli. Kushindwa kwako ni tukio na siyo wewe. Kushindwa mara nyingi ni tukio na siyo mtu. Unapofanya kitu na hakijaenda au hujapata matokeo unayotaka, wala usijione kama wewe ndiyo umeshindwa bali ni tukio ndiyo limeshindwa. Wewe hujashindwa …

Uvumilivu Ukiwa Kwenye Mchakato

Waswahili wanasema, mvumilivu hula mbivu. Au subira ya vuta heri. Haya yote ni sawa, na uvumilivu ni mzuri ukikukuta ukiwa kwenye Mchakato. Uvumilivu unakuja na matokeo fulani. Kama unakitu unafanya basi ni vema ukaendelea kwa sababu unajua mwisho wa siku utavuna. Huwezi kuvuna kama hujapanda. Uvumilivu unalipa pale ukiwa na kitu cha kufanya. Hakikisha unavumilia …

Fuatilia, Usilalamike

Watu wengi pale wanapoona wamepata changamoto ambayo imesababishwa na watu wenye mamlaka ya kitu fulani, huishia tu kulalamika. Usiishie tu kulalamika, bali fuatilia.Matatizo mengi yanashindwa kutatuliwa katika jamii zetu kwa sababu ya watu kushindwa kufuatilia kwa watu mwenye mamlaka husika wa kutatua shida zao. Badala yake wanaishia kulalamika kwa watu wasiokuwa na mamlaka na matokeo …

Usikubali Kushindwa Kirahisi

Kukubali kushindwa kirahisi, siyo sifa nzuri. Sifa nzuri ni kuwa king'ang'anizi na kutokubali kushindwa kirahisi. Unapambana mpaka unapata matokeo unayoyataka.Hata pale unapoona umefikia mwisho, usikubali kukiri udhaifu, pambana kupata matokeo. Hujatumwa kutoa mrejesho wa visingizio, bali matokeo. Matokeo mazuri huwa yanakuja na maandalizi mazuri yenye ufanisi. Kama unataka kupata matokeo mazuri, jiandae na maandalizi mazuri. …

Design a site like this with WordPress.com
Get started