Haya Ndiyo Yanayokukuta Kadiri Unavyofanikiwa Zaidi

Rafiki, Iko hivi, kadiri unavyofanikiwa ndivyo unavyodanganywa zaidi. Unajua kwa nini ? Kwa sababu watu wanakuambia kile unachotaka kusikia. Kwa mfano, machawa, watakupa kile unachotaka kusikia. Siyo watu wote watakuwa wema kwako, hivyo kadiri unavyofanikiwa, ndivyo unavyodanganywa zaidi hivyo kuwa makini. Mara zote kuwa na machale, ili usiwe mtu wa kudaganywa kila wakati. MUHIMU;Kama bado …

Mitazamo Chanya 10 Ya Kujaribu

Rafiki yangu nikupendaye, Kuna msemo unasema kwamba, haijaisha mpaka iishe. Kama umejaribu na umeshindwa, usichukulie kama ndiyo mwisho. Kwenye maisha yako, usiweke nukta bali weka alama ya koma.Kuwa na mtazamo wa koma kwamba mambo yatakuwa mazuri na siyo kuwa na mtazamo wa nukta kwamba umefikia mwisho mambo hayawezi kubadilika. Leo ondoka na mambo haya 10 …

Kama Hauko Tayari Kufanya Hiki Bado Hujafanikiwa

Rafiki, Kuna wakati watu wanafananisha mafanikio na uvivu. Kuwa tayari kuwajibika hayo ndiyo mafanikio makubwa kwako.Na kutokuwa tayari kuwajibika hayo siyo mafanikio. Mtu ambaye yuko tayari kuwajibika, hiko ndiyo kipimo cha mafanikio. Mafanikio yanataka mchakato, uweke kazi na siyo kusubiri matokeo mezani. Watu wengi ambao hawataki kuwajibika, wanakuwa na dalili za uvivu na hata kwenye …

Chochote Unachokifanya Kwa Namna Hii Utafanikiwa

Rafiki, Kuna kitu kimoja ambacho kinalipa sana duniani.Na kitu hicho siyo kingine bali ni SHAUKU. Chochote kile unachokifanya kwa shauku lazima utapata mafanikio. Hata kama unafanya maombi ya kiroho,ukiomba kwa shauku lazima utafanikiwa. Mchezaji anayecheza mchezo wake kwa shauku anakuwa anacheza vizuri na kuleta matokeo. Shauku inahitajika kwenye kila eneo la maisha yako.Kwa mfano, kwenye …

Kitu Pekee Ambacho Hupaswi Kukipoteza Kwenye Maisha Yako

Kila mmoja wetu ana ndoto. Na huenda tunatafuta ndoto mbalimbali kwenye maisha yetu. Katika hatua za utafutaji utakutana na changamoto nyingi. Changamoto ambazo ZINAWEZA KUKURUDISHA NYUMA kabisa na kuona huna maana. Kile unachotafuta utakipata, endapo tu , utakaa kwenye mchakato bila kukata tamaa. Mafanikio yako utayapata hapo ulipo.Kila mmoja mafanikio yake yapo kwenye kile anachofanya.Mafanikio …

Kuwa Makini Na Hili Kwenye biashara Yako

Wakati mtu unaanza biashara, inakuwa ndogo na unawahudumia wateja vizuri na kufanya kila kitu. Biashara inapokuwa kubwa, changamoto ndiyo huwa zinaanzia hapo. Unajua kwa nini? Kwa sababu, kadiri unavyokua katika biashara, ndivyo changamoto ya huduma mbovu kuongezeka. Natumaini ulishawahi kuwaona watu mwanzoni walikuwa wanahudumia vizuri tu lakini pale walipojipata, wanaanza kuhudumia kwa mazoea. Unapaswa kuwa …

Ukiwa Na Vitu Hivi Viwili, Mafanikio Kwako Ni Lazima

Ukikimbiza sungura wawili, hutampata hata mmoja.Hii ina maana kwamba, ukifokasi na mambo mengi, huwezi kukamilisha hata moja kwa ubora. Ukijua wapi unakwenda, huwezi kupotea njia. Kwenye maisha, ukiwa unajua nini unataka, lazima utakipata. Jua unachotaka, kisha watafute watu ambao wameshafika kule unakotaka kufika au wenye ndoto kama wewe na wanapambana kwenda kule unakotaka kufika. Ukishakuwa …

Anza Na Haya Kwanza

Huwa tunapenda kuhangaika na mambo makubwa wakati mambo madogo yenyewe hatuyafanyi vile inavyotakiwa kufanywa. Kabla hujakimbilia mambo makubwa, angalia yale ya msingi kwanza umeshayafanya? Tunayo mambo mengi ya msingi kabisa hatuyafanyi halafu tunataka mambo makubwa. Anza na mambo ya msingi kwanza UNAYOPASWA kuyafanya ndiyo ukimbilie mambo makubwa. Unakwama kwenye mambo makubwa kwa sababu hata yale …

Watu Wakichoka Huwa Wanafanya Vituko

Ni asili ya binadamu kama hapendi au hataki kitu, hawezi kukuambia wazi. Atakuonesha kila aina ya vituko au vipingamizi vya kuepukana na wewe.Unaweza kuwa na mtu unajua mko pamoja kumbe hapana. Kama mfanyakazi amechoka kufanya kazi na wewe, ataanza kukuonesha drama mbalimbali. Kama uko kwenye mahusiano vile vile mchezo ni ule ule, mtu ataanza kukuonesha …

Design a site like this with WordPress.com
Get started