Ustaarabu Pekee Unaopaswa Kuwa Nao Zama Hizi

Rafiki yangu nikupendaye, Kadiri siku zinavyozidi kwenda, watu wanakuwa na mambo mengi na muda ni mchache wa kukamilisha yote.Kifupi hatuna muda wa kufanya kila kitu, ila tunao muda wa kufanya vitu muhimu tu. Watu wa zama hizi wanapoteza umakini. Kuna wakati tunashindwa kupata kile tunachotaka kwa sababu ya kukosa umakini wa ufuatiliaji. Zama hizi tunakabiliwa …

Huwezi Kukwepa Matokeo Ya Kitu Hiki

Rafiki yangu nikupendaye, Ni rahisi kukwepa majukumu yako lakini ni ngumu kukwepa matokeo yake. Kwa mfano, unaweza kuwa mvivu kwenye majukumu yako ya kazi lakini kamwe huwezi kukwepa matokeo yake. Yote tunayoyapata kwenye maisha ni matokeo ya juhudi ambazo tumeziweka. Maisha huwa yanamwadhibu mtu kulingana na juhudi anazoweka.Ukiweka kazi utapata matokeo mazuri yanayoendana na wewe. …

Tafuta Kitu Kinachokupa Sababu

Rafiki yangu nikupendaye, Sisi binadamu tuna asili ya uvivu ndani yetu.Ili tuende mbele, tunahitaji kusukumwa. Watu wengi wanaofanya makubwa, huwa wana kitu kimoja ambacho kinawasukuma na kuwawajibisha juu ya kitu fulani. Mafanikio ni kuwajishana kwa sababu kwa asili yetu sisi binadamu bila kufanya hivyo ni ngumu watu kufanya. Timu yoyote ya mpira, huwa inakusukumwa na …

Ukitaka Usiahirishe Kitu

Huwa tunapoianza siku yetu huwa tuna nguvu ya kutosha.Ni kama vile unapoamka simu yako inakuwa ni ina chaji fuli. Kama unataka usiahirishe kitu, jambo lako la kwanza na la muhimu, anza nalo pale tu unapoamka. Ni rahisi sana kuahirisha kama ukifanya jambo lako usiku.Kama unataka usiahirishe kitu, basi pale tu unapoamka na kuianza siku yako. …

Mauzo Yanashinda Kila Kitu

Rafiki, Kama kuna kitu ambacho unataka kukifanikisha na bado hujafanya hivyo, basi wewe uza tu. Kwa sababu mauzo yanashinda kila tu nakuambia. Utaweza kupata kile unachotaka kwenye maisha yako, kama utaweza kuuza zaidi. Ni kupitia kuuza, ndiyo fedha inaingia kwenye mifuko yetu. Ukitaka maisha mazuri, utayapata kupitia kuuza.Kuuza ni taaluma moja ambayo ina hela sana. …

Ikatae Kabisa Hii Roho Kwenye Maisha Yako

Rafiki, Huwa tuna sauti moja ndani yetu ambayo inatufanya turudi nyuma. Tunarudi nyuma kwenye kila eneo la maisha yetu. Na leo tunakwenda kuivunja kabisa hiyo roho au sauti ambayo kila siku inakufanya urudi nyuma na kushindwa kukamilisha mambo muhimu. Na kitu ambacho unapaswa kukiua ni sauti yako ya ndani inayokukatisha tamaa. Kila mmoja wetu huwa …

Huyu Pekee Yake Anatosha

Rafiki yangu nikupendaye, Kwenye maisha kuna kupata na kukosa. Huwa kuna wakati tunatamani mambo yetu yaende kama vile tulivyopanga lakini dunia haiko hivyo. Unakuwa na mawazo mazuri ya kitu fulani, unaamua kuwashirikisha watu na wanakuambia ufanye watakuunga mkono. Lakini, wale ambao walikuaambia watakuunga mkono unashangaa wanaenda kinyume na wewe. Pale unapoona hakuna mtu anayekuunga mkono, …

Jinsi Ya Kupunguza Makosa Mwaka 2025

Rafiki yangu nikupendaye, Ufanye mwaka huu uwe bora kwako kwa kutofanya makosa yale yale uliyofanya mwaka jana.Kwa sababu, ujinga ni kufanya mambo yale yale kwa mtindo ule ule huku ukitegemea kupata matokeo ya tofauti. Ili upate matokeo ya tofauti, unapaswa kufanya kitu cha tofauti kabisa kwenye maisha yako. Na siyo kurudia yale yale uliyokuwa unayafanya …

Wale Ambao Hawakuamini Wafanyie Kitu Hiki

Rafiki yangu nikupendaye, Kila mmoja wetu huwa kitu fulani anafanya. Huenda katika eneo ulilopo, watu wanakuamini kwa kile unachofanya au hawakuamini kwa sababu ya uzoefu wako. Huenda una uwezo mzuri sana ndani yako, lakini wale watu ambao wanataka huduma yako, wanashindwa kukuamini kwa sababu ya uzoefu wako. Wafanyabiashara wanapoanza kazi wanapitia changamoto ya kutokuaminika. Wanunuaji …

Kama Bado Unaishi

Waswahili wanasema, usimtukane mamba kabla hujavuka mto. Usicheke matatizo ya wengine kama bado uko hai. Kwa sababu kile ambacho kimetokea kwa wengine, kinaweza kukutokea hata wewe. Hakuna ambaye yuko salama kwenye haya maisha.Mara zote ishi kwa tahadhari ili kukabiliana na kila hali. Kama bado unaishi, wasaidie wale ambao wanapitia changamoto fulani kwenye maisha yao. Mwimbaji …

Design a site like this with WordPress.com
Get started