Leo ni Maandalizi ya Kesho

Rafiki yangu mpendwa,Kila unachofanya leo kina mchango mkubwa katika maisha yako ya kesho. Mazoea, maamuzi, na juhudi zako za leo zitaamua namna kesho yako itakavyokuwa. Ikiwa unafanya mambo yako kwa uzembe au bila mpango, basi tarajia kesho yenye matokeo yasiyoridhisha. Lakini ikiwa leo unajituma, unajifunza, na kujiboresha, basi unajitengenezea kesho yenye mafanikio. Matokeo mazuri ya …

Jinsi ya Kuwa Bora

Rafiki yangu mpendwa, Katika dunia ya leo, kila mtu ana maoni. Watu wanajiona wataalamu wa kila kitu, na mara nyingi wako huru kutoa mawazo yao, hata kama si lazima wawe na ujuzi wa kina katika mada wanayozungumzia. Hakuna anayetaka kuonekana yuko nyuma. Kila mtu anataka kuonekana yuko mbele, anajua kila kitu, na ana mchango katika …

Mazingira Yanashinda Mara Zote

Rafiki yangu mpendwa, Ili uweze kushinda vishawishi vya aina yoyote, epuka mazingira yanayokuvuta kwenye mazoea mabaya. Mazingira yana nguvu kubwa kuliko hata utashi wako (willpower). Kama hutaki kuwa mtumwa wa mitandao ya kijamii, epuka kuwa na simu janja au futa apps zinazokula muda wako. Tafiti zinaonyesha kuwa kwa sasa, TikTok ndiyo mtandao unaoongoza kwa kunasa …

Hakuna Kinachopotea

Rafiki yangu nikupendaye, Chochote kile ambacho unajifunza sasa hivi, jua unafanya uwekezaji na utakuja kukusaidia baadaye. Ni kama vile unavyokula, virutubisho vinabaki ndani yako. Na unaposoma, unawekeza. Vile unavyojifunza sasa unaweza kuviona siyo muhimu lakini siku ukiwa una changamoto fulani unajikuta unavitumia bila hata wewe mwenyewe kujua. Asikuambie mtu maarifa hayana maana, mwache aendelee kujaribu …

Huwezi Kukimbia Maumivu

Rafiki yangu mpendwa, Katika safari ya maisha, kuna kitu kimoja ambacho kila mtu anakutana nacho ambacho ni maumivu. Haijalishi unajaribu kwa kiasi gani, huwezi kuyakimbia kabisa. Ni aidha ukubali kuyakabili sasa au ukubali athari zake baadaye. Huwezi kujikimbia wewe mwenyewe. Kukimbia maumivu yako ni sawa na kujikimbia wewe mwenyewe kitu ambacho hakiwezekani. Kuna aina mbalimbali …

Umuhimu wa Kujua Namba Zako

Rafiki yangu nikupendaye, Kila kitu kilichokuzunguka ni hesabu. Kila kilichokuzunguka ni namba. Kwa kifupi, maisha ni mchezo wa namba. Hatuwezi kukwepa namba kwenye kila eneo la maisha yetu. Kuku analalia kwa siku kwa wiki tatu, na mama mjamzito anabeba mimba kwa miezi tisa. Hii inatuonesha kwamba maisha yetu ni mchezo wa namba. Hatuwezi kukwepa namba …

Ijue Biashara Yako Kwa Kina

Rafiki yangu nikupendaye, Dunia inaenda kwa kasi, watu wanaofanya kile unachofanya wewe ni wengi. Utafanyaje ili uweze kujitofautisha na wengine? Ili uweze kujitofautisha na wengine unapaswa kuijua biashara kwa kina. Jua kile unachofanya vizuri sana kuliko mtu mwingine yeyote yule. Kuwa na uwezo wa kuilezea biashara yako kwa sekunde 30 na mtu akaelewa unafanya nini. …

Njia Nzuri Ya Kujitofautisha Na Wengine

Rafiki yangu nikupendaye, Ili upige hatua kwenye maisha yako, unapaswa kufanya kitu kimoja ambacho wengine hawakifanyi. Kitu ambacho ukikifanya, utapata matokeo mazuri. Utapata matokeo mazuri kwenye kila eneo la maisha yako. Ni kitu ambacho watu wengi hawako tayari kukifanya licha ya kuwa wanajua kile wanachofanya. Miaka nenda rudi, kama umekuwa huendi mbele, basi unarudi nyuma. …

Adui Mkubwa Anayekuzuia Usifanikiwe

Rafiki yangu nikupendaye, Ili tuweze kufanya, lazima tutake kweli kufanya, lazima tuwe tayari kuweka kila kinachopaswa kuwekwa kwenye mchakato wa kile tunachotaka ndiyo uweze kupata matokeo makubwa na ya tofauti. Adui mkubwa ambaye atakuzuia usiweze kufanya kama ambavyo unapaswa kufanya ni uvivu na kuridhika na matokeo madogo ambayo mtu anakuwa amepata. Ili uweze kupata zaidi …

Kitu Muhimu Kwenye Kila Uwekezaji

Vitu viwili vya kuwekeza vizuri ili kufanikiwa kwenye biashara, ambavyo ni fedha na muda. Lakini pia kuna kitu cha tatu muhimu sana kinachohitajika ili uwekezaji wa vitu hivyo viwili uwe na tija. Kitu hicho ni UVUMILIVU. Uwekezaji ni sawa na kupanda, huwezi kupanda mbegu leo na kesho ukaanza kuvuna. Unahitaji muda wa kupalilia mbegu hizo …

Design a site like this with WordPress.com
Get started