Unapofanya Kazi, Jifanyie Wewe: Jinsi ya Kujijenga Kwenye Ajira na Kujiandaa kwa Uhuru Wako wa Baadaye

Usijidanganye kwamba unamfanyia mtu kazi. Mtazamo ambao umekuwa unawapoteza waajiriwa wengi ni kuona kwamba wanamfanyia mtu mwingine kazi. Ni kweli kwamba kazi kubwa unayofanya anayefaidi matunda yake ni mtu mwingine, lakini ile kazi unajifanyia wewe mwenyewe.Hivi unafikiri unapokaa kwenye kazi moja kwa miaka kumi, ni nani anayenufaika au kuumia? Ni wewe.Kama utaitumia miaka hiyo kumi …

Kamwe Usiseme Huwezi—Sema Nitajifunza

Rafiki, Kwenye maisha ya kazi—iwe umeajiriwa, umejiajiri, au unafanya biashara—kuna maneno ambayo hayapaswi kabisa kutoka kinywani mwako. Mojawapo ya maneno hayo ni: “Hili siyo jukumu langu,” au “Siwezi kufanya.” Maneno haya huonyesha ukosefu wa uwajibikaji, moyo wa kujitoa, na huweza kuharibu fursa zako za kuaminiwa na kupandishwa daraja. Umeajiriwa?Pale unapopewa jukumu, hata kama linaonekana halihusiani …

Ipende Kazi Yako: Mbegu ya Mafanikio na Utimilifu

Kazi ndiyo rafiki na mpenzi wa kweli.Ipende KaziKazi yoyote unayoifanya, ipende. Ipende kwa moyo wote. Hata kama si kazi ya ndoto zako, hata kama ni ya muda tu au inalipa kidogo sana – bado inastahili mapenzi yako. Kupenda kazi ni maamuzi binafsi, si matokeo ya mazingira. Wengine wanaweza kukuona hufai, wakose kuthamini mchango wako, au …

“Anza Kwanza Kichwani: Siri ya Kufanikisha Malengo Yako ya Kifedha”

Rafiki, Watu wengi huweka malengo ya fedha kila mwaka—kuongeza kipato, kuanzisha biashara, kuwekeza zaidi, au hata kuondoka kwenye madeni. Lakini miaka inapita, na malengo hayo yanabaki kwenye makaratasi au kwenye ndoto za usiku. Kwa nini? Sababu kubwa siyo kwamba hawana maarifa au fursa, bali kwa sababu hawajayafikia malengo hayo kiakili kwanza. Ukweli ni huu: malengo …

Vunja Laana Ya Kipato Ulizorithi

Kuna jambo la kushangaza – na la kusikitisha – linalotokea kwa watu wengi linapokuja suala la fedha: laana ya kipato cha kurithi. Ndiyo, laana.Laana isiyoonekana kwa macho, lakini inayofunga ndoto za wengi kimya kimya.Ni ile hali ya ndani – isiyosemwa wazi – ya kuamini kwamba haupaswi kuwa na pesa nyingi zaidi ya wazazi wako. Watu …

Ongeza Wigo Wako wa Faraja Kwenye Fedha ili Ufanikiwe Zaidi Kwenye Mauzo

Kila mtu ana kiwango fulani cha fedha ambacho akili yake inakitambua kama "salama" au "cha kutosha". Hiki ndicho kiwango cha faraja ya kifedha—pale unapofikia, akili yako inatulia, moyo unaridhika, na hamasa ya kutafuta zaidi hupungua. Kwa mfano, kama umezoea kupata milioni moja kwa mwezi, mara nyingi utajikuta ukijenga maisha yako kuendana na kiwango hicho. Hicho …

Sababu Kuu Inayowatofautisha Wajasiriamali Wenye Mafanikio na Wanaoshindwa: Ujuzi wa Kuuza

Rafiki, Katika ulimwengu wa biashara, kuna sababu nyingi zinazotajwa kuwa chanzo cha mafanikio au kushindwa kwa mjasiriamali. Wengine husema ni mtaji, wengine mazingira au mitandao ya watu. Lakini kuna kitu kimoja ambacho mara nyingi hupuuzwa, lakini ndicho msingi wa kila mafanikio makubwa katika ujasiriamali — uwezo wa kuuza. Kitu kimoja kinachowatofautisha wajasiriamali wenye mafanikio na …

Biashara Ni Kama Mtoto Mdogo: Umuhimu wa Ufuatiliaji Katika Kila Eneo la Maisha

Rafiki, “Biashara ni kama mtoto mdogo – ikiachwa bila uangalizi, huweza kufa kabla ya kukua.” Katika safari ya maisha na mafanikio, kuna jambo moja ambalo hufanya tofauti kubwa kati ya wanaofanikiwa na wanaokwama: ufuatiliaji.Bila ufuatiliaji, hata mipango mizuri inaweza kupotea. Bila ufuatiliaji, matarajio hubaki kuwa ndoto. Na bila ufuatiliaji, biashara au maisha ya mtu huweza …

Jinsi ya Kujenga Ujasiri wa Kufanikisha Ndoto Zako

Ujasiri hauzaliwi nao mtu—unajengwa. Ni kama misuli: unavyoutumia zaidi, ndivyo unavyokuwa imara zaidi. Hapa kuna hatua tano zinazoweza kukusaidia kuujenga na kuutunza ujasiri wa kweli wa mafanikio: Anza kwa Kushinda Vita Ndani ya Akili Yako Mafanikio yanaanzia ndani ya kichwa chako kabla hayajawa halisi nje. Waza vizuri, sema vizuri, na jiamini hata kama hakuna mwingine …

Vikwazo Vikuu Viwili vya Mauzo kwa Muuzaji

Katika ulimwengu wa mauzo, mafanikio hayaamuliwi tu na ubora wa bidhaa au huduma, bali pia na hali ya kisaikolojia ya muuzaji mwenyewe. Wauzaji wengi hushindwa kufikia viwango vya juu si kwa sababu ya ukosefu wa maarifa au fursa, bali kwa sababu ya vikwazo vya ndani vinavyowazuia kuchukua hatua. Miongoni mwa vikwazo hivyo, viwili vinaonekana kuwa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started