Huyu Ndiye Mtu Ambaye Hana Shida na Fedha

Yoyote ambaye hataki maisha mazuri, Hataki kuwa na mali, fedha na kufanya kile anachotaka katika maisha yake huyo hayuko sawa kiakili. Kila mmoja anahitaji maisha mazuri na maisha mazuri yapo kama una fedha. Kama huna fedha huwezi kupata kile anachotaka, huwezi kula kile unachopenda. Ni ushahidi wa wazi kabisa kuwa fedha inafanya maisha yetu kuwa …

Kama Uko Kwenye Maisha Ya Ndoa, Kazi Yoyote Ile Epuka Kabisa Kufanya Kitu Hiki

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna kitu kibaya kama kuingia na kuishi wito ambao siyo wako. Ni mateso sana kufanya kile ambacho hakikusukumi kufanya kila siku. Katika maisha yetu ya mahusiano tunakutanishwa na watu wenye tabia tofauti. Kila mmoja ana tabia zake na watu wakikutana tena wanatengeneza tabia na kisha tabia zinawatengeneza tena. Kuna kitu ambacho watu …

Hili Ndiyo Jawabu La Kuishinda Hofu

Mpendwa rafiki yangu, Mara nyingi pale tunapotaka kufanya au kuanza kitu kipya huwa tunaingiwa na hofu ndani yetu. Hata kitendo tu cha kuzaliwa kwetu kuja duniani tunalia kwa hofu, sijui kama kuna mtu katika yetu alizaliwa akiwa anacheka, kama yupo hongera yake. Jamii yetu imejawa na hofu na kila mtu anapozaliwa anarithishwa ile hofu ndani …

Usimlaumu Mtu Yeyote Kama Hujamfanyia Kitu Hiki

Hakuna kazi ngumu kama ya kumfundisha mtu tabia. Watu wanakuwa na tabia zao sasa ukitaka kubadilisha kwa siku moja lazima utashindwa tu. Unaweza kumfundisha mtu kazi, lakini siyo kumfundisha mtu tabia. Ni rahisi kuwalaumu wengine pale tunapoona hawatufanyii vile tunavyotaka sisi. Muda mwingine tunaweza kuona kuwa labda wanatufanyia tu kwa makusudi kumbe wanakuwa hawajui kitu. …

Hii ndiyo Hamasa Kwa Mtu Aliyekata tamaa Hapa Duniani

Rafiki, Wengi wetu tunapokuwa tunatafuta kile tunachokitaka kwa muda mrefu bila kukipata huwa tunaishia kukata tamaa. Wengine tunajikuta tuna nung'unika na kulalamika na kuona kama Mungu ametusahau vile kumbe siyo kweli. Ziko familia nyingi ambazo zimekuwa katika hali ya sintofahamu huenda ni kwa sababu ya kukosa kile wanachokitaka kwa muda mrefu. Tukumbuke ya kuwa kinachoshindikana …

Kama Unataka Kuuza Sana Katika Biashara Yako Mfanye Mteja Wako Kuwa Hivi

Mpendwa rafiki yangu, Biashara yoyote ni mauzo. Bila mauzo hakuna uhai wa biashara yoyote ile. Na habari njema ni kwamba kila mmoja wetu kuna kitu anauza hivyo basi kila mtu anayetaka kupata mauzo mengi basi anatakiwa kujifunza saikolojia ya mauzo. Unaweza ukawa na bidhaa bora kweli lakini usiwe na mauzo mazuri, ili mteja aje kwako …

Fanya Uamuzi Huu Wa Makusudi Kabisa Katika Maisha Yako

Rafiki, Pema usijapo pema,ukipema si pema tena wasemavyo waswahili. Mama mjazamzito anatakiwa kubeba mimba yake ndani ya miezi tisa chini na zaidi ya hapo inakuwa si salama tena kwake. Unakuwa ni mzigo mkubwa tena kwake. Tuna vifungo vingi ambavyo tumevibeba ndani yetu,vinatufanya tuchoke na kuonekana kuchaka katika maisha yetu. watu wengine hawapendi kuona mtu fulani …

Njia Tatu Pekee Za Kuepuka Kukosolewa

Kama uko hai basi lazima tu utakosolewa, sehemu ambayo haina usumbufu wa aina yoyote ile ni kaburini pale ambako mwili wako utakapowekwa baada ya safari yako kuisha hapa duniani. Kuna watu wanajiona kama wao hawana bahati bali wana visirani kwenye maisha yao hii ni baada ya kuona kuwa kila wanachofanya hawakosi kukosolewa na kukatishwa tamaa. …

Hiki Ndiyo Kipindi Kizuri Cha Kujua Thamani Ya Uhai Wako

Hakuna zawadi kubwa hapa duniani tuliyopewa kama zawadi ya kuishi. Ni upendeleo mkubwa mimi na wewe kuendelea kuishi hapa duniani. Kupitia zawadi ya uhai ndiyo tunaweza kukamilisha ndoto zetu tulizokuwa nazo. Tunaweza kuwa malengo na mipango mizuri lakini bila zawadi ya uhai hatuwezi kitu. Ni zawadi ambayo hatuilipi hivyo tunaalikwa mimi na wewe kushukuru kwa …

Ufahamu Utamaduni Ambao Watu Wengi Hawana

Rafiki, Hakuna aliyezaliwa anajua kila kitu,bali tumezaliwa tukiwa tunajua kulia na kunyonya tu lakini kadiri tunavyokua basi tumejikuta tunajua vingi. Akili zetu ni kama raba bendi kadiri unaivuta ndivyo inavyoongezeka urefu. Uko hivyo ulivyo kadiri ya maarifa uliyoamua kuingiza katika akili yako, kadiri unavyoingiza vitu chanya akili mwako nayo akili yako inaendelea kutanuka hivyo wigo …

Design a site like this with WordPress.com
Get started