Hiki Ndiyo Kitu Cha Kuepuka Pale Unapojenga Timu

Pale tunapojenga kitu tunatumia nguvu nyingi, fedha nyingi na muda hivyo ukiangalia ni rasilimali nyingi. Lakini pale unapotaka kubomoa kitu ni dakika tu. Kwa mfano, kujenga jina ni kazi, unatumia kila aina za rasilimali lakini kuvunja jina hachukui sekunde. Vivyo hivyo katika kujenga timu, tunapojenga timu tunatumia nguvu nyingi. Na timu ninazozungumzia hapa ni timu …

Huu Ndiyo Ushauri Wa Mwanafalsafa Epictetus Kwa Wale Wote Wanaotaka Kupiga Hatua

Hakuna kitu ambacho unaweza kufanya na kumfurahisha kila mtu. Kila binadamu ana maoni yake kwenye kila kitu. Haitokuja kutokea hata siku moja utaweza kumfurahisha kila mtu. Ila mtu pekee ambaye unaweza kumfurahisha hapa duniani ni wewe mwenyewe. Katika suala la mafanikio, kila mtu ana njia zake. Kila mtu ana hadithi zake hivyo hadithi zetu katika …

Jinsi Ya Kutumia Utani Ili Kukuzuia Usipate Hasira Na Kutumia Nafasi Yako Vibaya

Binadamu sisi  ni viumbe wa hisia, hivyo vitu kama hasira ni kitu cha kawaida sana. Na wako ambao wanatumia nafasi zao vibaya kwa sababu ya kuwa na chuki na mtu fulani sasa ikitokea mtu huyo ni kiongozi anatumia nguvu yake ya uongozi kumuumiza yule wa chini yake. Katika falsafa ya ustoa tunaalikwa kujiandaa na lolote …

Unaweza, Ni Suala La Kuamua Tu

Katika hii dunia kila mtu anaweza kuwa vile anataka kama mtu huyo akiamua kufanya kile anachotaka. Watu wengi wanaweza ila hawafanyi kwa sababu hawajaamua. Unajua kuamua ndiyo hatua ya kwanza ya kufikia mafanikio yako.Usipoamua hakuna kizuri kitakachokuja kwako. Binadamu wanafanya vizuri sana pale wanapoamua wao wenyewe kufanya. Binadamu hafanyi vizuri kama akilazimishwa kufanya ila akiamua …

Hii Ndiyo Hatua Ya Kuchukua Pale Fedha Inapokuwa Ngumu Kwako

Iko hivi rafiki yangu, fedha Inapokuwa nyingi kwenye mzunguko inakuwa rahisi kupatikana. Lakini pia na thamani yake inakuwa ndogo, mtu unaweza kuwa na fedha nyingi lakini haina thamani kubwa na tumaini hili umeshawahi kukutana nalo, unakuwa na fedha nyingi lakini inakuwa haina thamani.Unaweza ukawa na fedha nyingi lakini vitu vikawa ghali sana licha ya wewe …

Ifahamu Sababu Kuu Moja Kwanini Watu Wanaahirisha Mambo

Sisi binadamu tuna asili ya uvivu. Hivyo pale tunapohisi kutokufanya kitu  tunatafuta sababu ya kuacha, tunaacha kufanya na tunatii miili yetu vile inavyotaka na hapa ndiyo maana wengi wanapotea. Tunatakiwa tuwe tunaitawala miili yetu na siyo sisi kutawaliwa na miili yetu. Sababu kuu moja ambayo inatufanya tuahirishe mambo yetu ni moja ambayo ni kwamba tunaahirisha …

Hiki Ndicho Unachokosa Pale Ambapo Huchukui Hatua

Kama kila mtu angechukua hatua ya kile anachotaka basi leo hii kila mtu angeweza kutimiza ndoto zake. Lakini mambo ndiyo yako tofauti tena, watu hawako tayari kuchukua hatua hata kama ni kitu muhimu kwao. Ni nani hajui kama akichukua hatua atakua atakuwa mbali sana?Hebu fikiria ni mambo mangapi umeyaahirisha kufanya ndani ya mwaka huu? Vipi …

Kitu Chochote Kilichokosa Maandalizi Kinakuwa Hivi

Hakuna mafanikio bila maandalizi, hatua unazochukua kila siku ndiyo zinazokupelekea kwenye maandalizi ya kufikia mafanikio unayotaka. Hivi ni kitu gani ambacho kinaweza kufanyika bila maandalizi? Sasa kitu ambacho kimekosa maandalizi kinakuwa hakina ufanisi mkubwa. Na maandalizi bila ya kuwa na ufanisi hapo panakuwa hakuna maandalizi. Kumbe basi, sifa moja nzuri ya maandalizi ni ufanisi. Maandalizi …

Kila Mzazi Awe Makini Na Hili

Dunia ya sasa watu wako huru kufanya kile wanachojisikia kufanya bila kuwa na hofu yoyote ile. Matukio ya ajabu yanazidi kushamiri kila siku. Ulimwengu huu ambao wazazi wanakua bize sana na majukumu ya kutafuta fedha, watu wengine wanatumia mwanya huo kuwarubuni watoto wadogo. Vitendo vya ukatili kwa watoto wadogo vinakuwa kwa kasi, watoto ambao hawana …

Jiepushe Na Vitu Hivi Vitatu Kwenye Maisha Yako

Dunia inajiendesha kwa misingi yake ya asili hivyo tukiweza kuishi kadiri ya misingi ya asili tutakuwa na maisha bora sana. Shabaha yangu leo ni kukujulisha vitu vitatu ambavyo unapaswa kuviepuka kwenye maisha yako.Na tukiweza kuviepuka tutaifanya dunia kuwa sehemu salama kuishi kwa kila mmoja wetu. Na vitu hivyo ni kama ifuatavyo; Uzembe, tunaweza kupunguza uzembe …

Design a site like this with WordPress.com
Get started