Hivi Ndivyo Vitabu Vyangu Ambavyo Mpaka Sasa Vipo Sokoni

Karibu sana rafiki ujipatie nakala ya kitabu chako na uweze kujifunza. Mpaka sasa vitabu ambavyo viko sokoni na bei yake ni kama vifuatavyo; Funga na Utajiri na Kuupa Umasikini Talaka Bei ya kitabu hiki ni 5000/=Ongea Lugha Yako, Sauti Yako Ya Ndani Ndiyo Mafanikio Yako Ya Kweli.Bei ni elfu 5Kwanini Msamaha, Ni wakati wa kupata …

Kuwa Makini Na Mtu Huyu Anayeanika Mambo Yako Hadharani

Iko hivi rafiki yangu,Kama unataka watu wasijue mambo yako binafsi usiwaambie. Anayeanika mambo yako hadharani ni wewe mwenyewe. Usimlaumu mtu mwingine, kama ni mambo yako binafsi sasa watu wa nje wamejuaje? Kumbuka, ukiwaambia watu mambo yako ambayo hupendi wayajue jua watayajua tu. Unapokuta watu wanajua mambo yako mengi ya ndani basi ujue wewe ndiyo tatizo. …

Haijalishi Una Roho Nzuri Kiasi Gani

Leo tuambiane tu ukweli bila kuweka unafiki. Kuwa na roho nzuri bila kuwa na fedha roho yako nzuri itakuwa haina msaada kwa mtu ambaye ana shida ya fedha kwako. Haijalishi una roho nzuri kiasi gani kama huna fedha roho yako nzuri haitakuwa na msaada kwa wengine. Kwa mfano, watu wakiwa na njaa hawatashiba roho nzuri …

Hiki Ndicho Kitakachotokea Pale Usipojisumbua

Asili itakuadhibu pale usipojisumbua kwa mambo yako mwenyewe. Jua unachopaswa kufanya na kifanye vizuri sana. Jisumbue wewe mwenyewe kabla wengine hawajakusumbua. Ni bora kujisumbua wewe mwenyewe kuliko kusumbuliwa na dunia. Dunia inawapenda watu ambao wanajitambua na kujua nini wanatakiwa kufanya kwenye maisha yao. Ukijituma na kujisukuma kwenye mambo yako hakuna atakayekusumbua. Ila ukisubiria kukumbushwa majukumu …

Hii Ndiyo Faida Ya Kujua Kanuni Ya Mchezo Wako

Hakikisha unajua vizuri kanuni za mchezo unaotaka kucheza. Bila kujua kanuni za mchezo unaotaka kucheza lazima utakua umeshindwa kabla hata ya kuanza kwa mchezo. Ukishajua kanuni za mchezo unaocheza, cheza vizuri sana kuliko mtu yeyote kwenye mchezo huo. Mchezo wako unaweza kuwa ni kazi unayofanya au kile unachopenda kufanya. Fanya kile unachopenda vizuri kuliko mtu …

Kama Unajua Hiki Lazima Utafanikiwa

Kama unajua kile unachotaka kwenye maisha yako lazima utafanikiwa. Kama unaamka na hujui unakwenda kufanya nini ni ngumu kufanikiwa. Mtu anayejua kile anachotaka hawezi kuamka asubuhi na hajui nini anatakiwa kufanya. Wachezaji wakubwa wa mpira wa miguu au kikapu au mchezo wowote ule huwa wanalipwa kiasi kikubwa cha fedha kuliko wengine kwa sababu ya thamani …

Huu Ni Wajibu Wako Wa Msingi

Kuna vitu vingine hata ukifanya vizuri sana huhitaji kupongezwa kwa sababu ni wajibu wako kufanya hivyo. Uaminifu ni wajibu wako.Kwa mfano, mtu yeyote aliyepo kwenye ndoa suala la kuwa mwaminifu katika ndoa au kutoka nje ya ndoa ni wajibu wako. Kwa sababu kuoa au kuolewa msingi wake mkubwa ni uaminifu. Kama usipokuwa mwaminifu kwenye ndoa …

Usisahau Kufanya Kitu Hiki Ukipata Mshahara Wako

Msingi mkuu wa fedha ni kutoa thamani. Hivyo basi, ukitaka upate fedha zaidi toa thamani kubwa zaidi. Fedha unayopata kwenye mshahara wako ni mbegu. Hata siku moja sijawahi kumuona mkulima anayekula mbegu hata awe na njaa vipi. Hivyo basi, usisahau kuwekeza sehemu ya fedha unayopata kutoka kwenye kipato au mshahara wako katika uwekezaji. Na uwekezaji …

Jinsi Ulivyo Mbinafsi Na Mchoyo

Utaweza kukataa wewe siyo mbinafsi wala mchoyo lakini sio kweli. Leo ninakwenda kukuonesha kwa namna gani ulivyokuwa mchoyo na mbinafsi. Ili kujua kama wewe ni mbinafsi na mchoyo hebu angalia malengo yako uliyokuwa nayo kwenye maisha yako. Ukiwa na malengo ya kununua gari na kujenga nyumba inayokutosha wewe na familia yako tu wewe ni mchoyo. …

Design a site like this with WordPress.com
Get started