Hii Ndiyo Siri Ya Kushinda Kwenye Chochote Kile Unachotaka

Wengi wanachagua kushindwa kabla hata hawajaanza kufanya. Watu wanakuwa na mawazo mazuri sana lakini cha ajabu hawachukui hatua mpaka wanaibua hofu ndani yao ya kuzalisha matokeo ya kushindwa. Huwezi kushinda kama hauko tayari kujaribu. Na siri ya ushindi kwenye kitu chochote kile ni kujaribu. Wale ambao unaona wana bahati sana huwa ni watu wazuri sana …

Kama Inavumilika, Vumilia

Aliyekuwa mtawala wa Roma na mwanafalsafa wa ustoa mwanafalsafa Marcus Aurelius enzi za uhai wake aliwahi kunukuliwa akisema, kama inavumilika, vumilia ila usilalamike. Kama unapitia magumu ambayo yanavumilika vumilia lakini usilalamike. Kama unaona maisha unayoishi si mazuri chukua hatua na siyo kulalamika. Maajabu yanakuja pale ambapo mtu anaendelea kumilia huku akiwa hachukui hatua sahihi badala …

Vitu Viwili Unavyopaswa Kuwa Navyo Ili Ufanikiwe

Siyo kwamba watu hawajui kile wanachopaswa kufanya, ila watu hawana ujasiri wa kufanya kile wanachopaswa kufanya. Kama kila mtu angekuwa na ujasiri wa kusimamia malengo yake basi tungezidi kuiona dunia inazidi kuwa sehemu salama ya kuishi kwa kila mmoja wetu. Ili ufanikiwe kwenye kitu chochote kile kuwa na vitu hivi viwili. Moja, maamuzi. Kama huendi …

Tafadhali, Usirudie Kusema Kauli Hii Tena

Huwezi kufanikiwa kwa makubwa kama madogo unayadharau. Kama unafanya kazi isiyokulipa vile unavyotaka wewe isiwe tiketi kwako kufanya kwa kiwango cha chini. Kazi yoyote iwe inakulipa au haikulipi unatakiwa kuifanya kwa ubora. Kwa sababu kama utashindwa kufanya kazi ndogo kwa ubora hata ukipata kubwa hutafanya kwa ubora. Binadamu tumekuwa ni watu wa kutengeneza tabia na …

Fanya Mambo Haya Mawili Ili Uweze Kuishi Kwa Amani

Amani ni kitu kidogo tu lakini kikikosekana sehemu yoyote panakuwa ni shida. Ukikosa amani nyumbani, kazini, kwenye biashara, mahusiano nk hali inakuwa mbaya. Tunapokwenda kuabudu kwenye nyumba zetu za ibada tunahubiriwa amani, na wakati tukitaka kuondoka tunaambiwa amani ya Bwana iwe nasi na tuende kwa amani. Kumbe basi, amani ikiwepo kila kitu kitakuwepo. Kama hakuna …

Huyu Ndiye Msemaji Mkuu Wa Maisha Yako

Kwenye taasisi nyingi huwa kuna msemaji mkuu wa taasisi hiyo. Siyo kila mtu ni msemaji maana kuna watu wengine wakisema wanaweza kuharibu kabisa hali ya hewa badala ya kusaidia. Kama kila mtu akiwa ni msemaji mkuu, kutakuwa na fujo nyingi. Mwingine anaweza kujiuliza sasa kama mimi sina msemaji mkuu wa maisha yangu nani atakua ananisemea? …

Design a site like this with WordPress.com
Get started