Hiki Ndicho Kitu Ambacho Watu Wengi Wanakitoa Kwa Wengine

Mara nyingi watu huwa wanauza kile walichonacho kwa lugha rahisi tunaweza kusema watu wanajaribu kutoa kile ambacho tayari kipo ndani yao. Usiumie na wale wanaokufanyia mabaya badala yake waonee huruma. Kwa sababu watu wanatoa kile ambacho kipo ndani yao. Kwa mfano, ukiona mtu anakupa upendo jua upendo ndiyo upo ndani yake. Ukiona anakuuzia chuki jua …

Sentensi Mbili Zitakazobadili Maisha Yako

Leo tunahitimisha juma la 46 katika mwaka 2021. Zimebakia siku 48 tu kumaliza mwaka 2021. Najua ndani ya juma hili umekutana na mengi na umejifunza mengi pia. Hivyo basi, nami napenda kukushirikisha sentensi mbili tu zitakazobadili maisha yako. Ukichanganya na yale uliyojifunza na haya unayokwenda kujifunza sasa unakwenda kuwa na mwisho mzuri kabisa wa juma …

Karibu Kwenye Semina Ya Kuanza Mwaka 2022 Kiushindi, Huwezi Kuhamasisha Kama Hujahamasika

Iko wazi kabisa huwezi kuhamasisha wengine kama wewe hujahamasika. Ili uweze kuwasaidia wengine lazima na wewe uwe na kitu cha kutoa. Ili uweze kutoa kwa wengine lazima uwe na kitu cha kutoa. Wakati nasoma kitabu cha mwandishi Robin Sharma kinachoitwa the everyday Hero nikakutana na sehemu ambayo Robin Sharma anasema hakuna cheo anapenda kujipa kama …

Njia Mbili Unazoweza Kuzitumia Kama Huoni Mchango Wako Kwenye Tatizo Lolote Ambalo Upo

Ni kawaida na tabia ya binadamu kupenda kujipendelea. Pale wewe unapofanya kosa ni rahisi kujipa sababu nzuri kwanini umefanya kosa hilo. Kwa sababu sisi binadamu ni wagumu kukubali kwamba na sisi tumechangia kutokea kwa matatizo ambayo tunayo. Matatizo mengine huwa yanatokea huenda labda ulikuwa umechoka au ulipitiwa au hukuwa na taarifa za kutosha. Lakini, inapotokea …

Jinsi Ya Kuepuka Utapia Mlo Wa Akili

Kitu chochote ambacho hakina afya imara huwa kinakufa. Mwili wa binadamu ukikosa virutubisho sahihi kwenye mwili wake ni rahisi kupata magonjwa mbalimbali. Juzi nilipokea simu kutoka kwa mmoja wa wasomaji wa kazi zangu, katika mazungumzo yetu, nilimuuliza kitu, je, tokea umalize shule ulishawahi kusoma kitabu? Akajibu hapana. Naamini bado kuna watu wengi tu tokea wamalize …

Sababu Mbili Zinazopelekea Kuwa Tofauti Kwenye Mazungumzo

Siku zote katika mazungumzo kubishana ni njia mbovu sana ya kufikia maamuzi. Kila mtu anakazana kusimamia kile anachoamini. Ni muhimu sana uelewe kwamba kwenye mazungumzo kila mmoja anaweza kuwa na mtazamo tofauti. Leo nimekuandalia sababu mbili zinazopelekea watu kuwa tofauti kwenye mazungumzo. Na mara nyingi mitazamo yetu inakuwa tofauti kwa sababu kuu mbili; Moja, tumepitia …

Shugulika Na Vitu Hivi Viwili Utaiona Fedha

Mara nyingi watu huwa wanajisahau sana. Wanakuwa bize sana kuongeza kipato lakini cha ajabu mwisho wa siku hawaioni hela. Kitu kikubwa ambacho unatakiwa kufanya kwenye eneo la fedha, ni kuongeza kipato na kudhibiti matumizi. Yaani ni kitu ambacho kinatakiwa kwenda sambamba. Ni kawaida kabisa, mtu akiwa hana fedha nyingi atatumia kile alichonacho kwa umakini lakini …

Design a site like this with WordPress.com
Get started