Kitu Ambacho Kinatukuzwa Sana Katika Zama Hizi

Katika kitabu cha Dedicated kilichoandikwa na mwanajeshi Pete Davis, mwandishi anaelezea ni kwa jinsi gani jamii yetu imeipa uzito mkubwa fedha kuliko vitu na watu. Fedha imekuwa ni kitu ambacho kinatukuzwa sana zama hizi. Mwandishi anasema, kipindi cha nyuma kulikuwa na mpaka ulio wazi kati ya fedha na jamii. Na ilijulikana wazi ni vitu gani …

Usikimbilie Kuvuka Daraja Kabla Hujalifikia

Huwa tunahangaika na mambo ambayo hata kiuhalisia bado hatujayafikia. Ni kama vile tunafikiria kuvuka daraja kabla hata hatujalifikia. Endelea kufanya kile unachofanya na ukifika wakati wa kuvuka daraja utalivuka. Utashindwa kufanya kile ulichopanga kufanya kwa wakati huu kama akili yako inafikiria kuvuka daraja kabla hujalifikia. Kukimbilia kuvuka daraja kabla hujalifikia ni kuhangaika na mambo ambayo …

Mtu Wa Namna Hii Ni Ngumu Kusaidika

Kama umekuwa na nidhamu ndogo, au huna kabisa nidhamu binafsi ya kujisimamia utakua ni mtu ambaye ni ngumu kusaidika. Mtu ambaye anasubiri kusukumwa kufanya wajibu wake, anakuwa anaweka ugumu wa kusaidika. Mtu ambaye hawezi kufanya kitu mpaka akumbushwe au kusukumwa ndiyo anajituma kufanya kazi ni mtu ambaye ni mzigo na anakuwa mgumu kusaidika. Mtu ambaye …

Jua Vitu Hivi Viwili Kama Unataka Kufanikiwa

Kitu kikubwa ambacho nimejifunza katika maisha ni kwamba, kama huna mwelekeo, mwelekeo wowote utakuchukua.Kama hujasimama kwa lolote, utaanguka kwa lolote. Usipokuwa na misingi yoyote ile, ni rahisi kuyumbishwa. Ila mtu ambaye ana mwelekeo anajua kule anakoelekea na anajua kile anachosimamia. Leo nakusihi ujue vitu hivi viwili kwenye maisha yako. Moja, jua kile unachotaka ni nini …

Tunza Siri Za Mtu Huyu

Kama unafanya kazi, biashara au unatoa huduma yoyote ile unatakiwa kuwajali wateja wako. Wateja ni watu muhimu sana kwenye kile unachofanya. Kwa sababu wateja ndiyo wanakuletea fedha kwenye biashara yako. Kwa kuwa wateja ni muhimu unapaswa kutunza siri zao. Mteja anapokuamini na kukuambia mambo yake, tafadhali tunza siri zake. Watu wakikuamini na wewe waaminishe kuwa …

Wekeza Kwa Watu Hawa Muhimu Sana Kwako

Kama ikitokea umekufa leo usiku, mwajiri wako atatangaza nafasi ya kazi mwisho wa mwezi kuziba nafasi yako. Lakini familia yako, wapendwa wako na marafiki zako watakukosa daima.Usiwe bize sana kuishi maisha na kusahau kutengeneza maisha. Hayo ni maneno ya bilionea Elon Musk. Kwa hekima hiyo hapo juu, watu wanakula maisha lakini wanasahau kuwatengenezea watoto wao …

Hiki Ndicho Kinachotokea Pale Mtu Anapoweka Kipaumbele Kwenye Kazi Tu

Jana tulijifunza madhara ya kufanya kazi bila kuwa na mapumziko. Na tuliona ni kwa namna gani mwili wa binadamu unavyohitaji mapumziko. Kwenye maisha lazima uwe na mlinganyo sawa,ukisema unaweka kazi tu mambo mengine yataharibika. Kwa kuweka kipaumbele mbele kikubwa kwenye kazi tu , utayapuuza maeneo mengine ya maisha yako ambayo yanakuwa dhaifu na kuathiri maisha …

Kitu Ambacho Kimepuuzwa Na Watu Wengi Zama Hizi

Katika zama tunazoishi, watu hawapumziki wala hawafanyi kazi. Hapa ninamaanisha kwamba wakati wa kazi mtu anafikiria mapumziko na wakati wa mapumziko mtu anafikiria kazi. Mtu akiwa anakula, uwepo wake hauko kwenye kula bali anafikiria kumaliza aende kufanya kitu kingine. Hii inawafanya hata watu wakila hawaoni ile ladha ya chakula kwa sababu wakati wa kula akili …

Jenga Kitu Hiki Muhimu Kama Una Miliki Biashara

Biashara siyo kununua vitu kwa bei ya jumla na kuviweka kwenye eneo lako la biashara na kuuza kwa reja reja. Kufanikiwa kwenye biashara siyo kazi rahisi kama ingekuwa rahisi basi kila mfanyabiashara angekuwa mbali sana. Wengi tunawaona wanaanza biashara lakini zinakuja kuwashinda. Wewe kama mmiliki wa biashara majukumu yako siyo kuuza na kununua pekee, siyo …

Design a site like this with WordPress.com
Get started