Hiki Ndicho Unachokosa Pale Ambapo Huchukui Hatua

Kama kila mtu angechukua hatua ya kile anachotaka basi leo hii kila mtu angeweza kutimiza ndoto zake. Lakini mambo ndiyo yako tofauti tena, watu hawako tayari kuchukua hatua hata kama ni kitu muhimu kwao. Ni nani hajui kama akichukua hatua atakua atakuwa mbali sana?Hebu fikiria ni mambo mangapi umeyaahirisha kufanya ndani ya mwaka huu? Vipi …

Kitu Chochote Kilichokosa Maandalizi Kinakuwa Hivi

Hakuna mafanikio bila maandalizi, hatua unazochukua kila siku ndiyo zinazokupelekea kwenye maandalizi ya kufikia mafanikio unayotaka. Hivi ni kitu gani ambacho kinaweza kufanyika bila maandalizi? Sasa kitu ambacho kimekosa maandalizi kinakuwa hakina ufanisi mkubwa. Na maandalizi bila ya kuwa na ufanisi hapo panakuwa hakuna maandalizi. Kumbe basi, sifa moja nzuri ya maandalizi ni ufanisi. Maandalizi …

Kila Mzazi Awe Makini Na Hili

Dunia ya sasa watu wako huru kufanya kile wanachojisikia kufanya bila kuwa na hofu yoyote ile. Matukio ya ajabu yanazidi kushamiri kila siku. Ulimwengu huu ambao wazazi wanakua bize sana na majukumu ya kutafuta fedha, watu wengine wanatumia mwanya huo kuwarubuni watoto wadogo. Vitendo vya ukatili kwa watoto wadogo vinakuwa kwa kasi, watoto ambao hawana …

Jiepushe Na Vitu Hivi Vitatu Kwenye Maisha Yako

Dunia inajiendesha kwa misingi yake ya asili hivyo tukiweza kuishi kadiri ya misingi ya asili tutakuwa na maisha bora sana. Shabaha yangu leo ni kukujulisha vitu vitatu ambavyo unapaswa kuviepuka kwenye maisha yako.Na tukiweza kuviepuka tutaifanya dunia kuwa sehemu salama kuishi kwa kila mmoja wetu. Na vitu hivyo ni kama ifuatavyo; Uzembe, tunaweza kupunguza uzembe …

Hakuna Mtu Anayekupotezea Muda

Huwa tunalalamika kuwa kuna watu huwa wanatupotezea muda lakini siyo kweli hakuna anayekupotezea muda isipokuwa wewe mwenyewe. Unajipotezea muda wewe mwenyewe, mpaka mtu akupotezee muda basi tayari wewe umekubali akupotezee muda. Ili kuepukana na kulalamika juu ya hili, unatakiwa kuwa na njia mbadala ya kutumia muda wako vizuri. Kwa mfano, umewekeana miadi na mtu kuwa …

Huyu Ndiye Jiniazi Wa Kutawala Akili Za Watu

Rafiki, Mchezo mzima wa binadamu uko kwenye akili ndiyo maana huyu jiniazi ambaye tunakwenda kumjua leo ameweza kufanikiwa hilo kwa asilimia mia moja. Biashara zote hasi ambazo wewe unazijua zinawatawaliwa na bingwa wa kutawala akili za watu kwenye karne ya 21. Jiniazi ambaye anatawala akili za watu siyo mwingine bali ni shetani. Kazi kubwa ya …

Tafuta Mtu Anayeendana Na Kasi Yako

Katika maisha kila mmoja huwa anaishi falsafa yake na kufanya kile anachokiamini na kuona kwake ni sahihi. Ni kweli hatuwezi kuwa sawa kimtazamo lakini tunaweza kutafuta watu ambao wanaendana na kasi yetu ya maisha. Ukifanya kazi na mtu ambaye hawezi kwenda na kasi yako basi utakua unapoteza muda. Tunatakiwa kuambatana na watu ambao wana kasi …

Jinsi Ya Kumaliza Siku Yako Kwa Ushindi Mkubwa

Ni kawaida kwa kila mwanamafanikio kuanza siku yake kwa ushindi na kuimaliza kwa ushindi. Ila wako watu ambao hawajui jinsi ya kumaliza siku zao kwa ushindi. Leo ninakwenda kukufundisha namna ya kumaliza siku yako kwa ushindi. Aliyekuwa mwandishi, mwanasiasa na mwanajeshi katika nchi ya uingereza aliwahi kusema namna ya kumaliza siku yako kwa ushindi na …

Sifa Moja Muhimu Ambayo Kila Mwajiriwa Na Mfanyabiashara Anapaswa Kuwa Nayo

Kiasili kila mtu ni mfanyabiashara hata kama umeajiriwa basi jua hata kuajiriwa ni mfumo wa biashara ambao wewe unakua unauza ujuzi na muda wako. Kila mfanyabiashara na aliyeajiriwa unapaswa kuwa na sifa moja muhimu ambayo ni kuwahi eneo la kazi.Iwe umejiajiri au umeajiriwa unatakiwa kuwahi eneo la kazi mapema. Kuna faida moja kubwa sana ya …

Falsafa Ya Kazi Na Sala

Natumaini maneno haya kazi na sala siyo mara yako ya kwanza kuyasikia, umeshayasikia sana watu mbalimbali wakisema na kuwekea msisitizo. Maana rahisi ya kazi na sala ni kama vile kusema imani na matendo. Imani bila matendo imekufa, kama una imani ya kuwa na kitu fulani basi vizuri sana. Lakini imani uliyonayo unatakiwa kuiweka katika kazi.Usikeshe …

Design a site like this with WordPress.com
Get started