Faida Moja Wapo Ya Kuwa Na Mfumo Wa Kuendesha Biashara

Biashara nyingi huwa zinawategemea wamiliki moja kwa moja, yaani wasipokuwepo basi na biashara nayo inakufa. Tunaona biashara nyingi zinakufa kwa sababu ya wamiliki hawakuacha mfumo wa kuendesha biashara hizo. Biashara nyingi zinaendeshwa kama mmiliki wa biashara ndiyo anakuwa fundi, asipokuwepo fundi basi mambo mengine hayawezi kwenda. Watu wakubwa waliofikia mafanikio makubwa, waliweza kuziacha biashara zao …

Vitu Vitatu Vinavyowakwamisha Watu Kutokufanikiwa

Kama kuna mahali hupigi hatua basi ziko sababu ambazo zinakukwamisha wewe. Na ukiweza kuzijua utazitumia kujitathimini na kisha kuwa bora. Na sababu hizo ni ; Moja ni Kutokuchukua hatua kubwa.Watu wengi wanachukua hatua ndogo kwenye maisha yao, hawataki kujitesa, wanataka wapate mafanikio bila kazi. Hata kama mtu anapitia hali ya hatari kwenye maisha yake, wala …

Utakua Na Mtazamo Chanya Kwenye Hili?

Mtu aliyekuepo duniani miaka 100 iliyopita akifufuka leo ataona maisha yamerahisishwa sana. Tukianzia kwenye masomo, kwa mfano somo la hisabati kwa wanafunzi walikuwa hawana majibu ya kuchagua lakini kwa sasa yapo na tena wanatumia na kikokotoa yaani calculator. Unaona ilivyokuwa rahisi, mtu aliyesoma zamani kwa sasa hawezi kufeli kabisa na hata wanaofeli sasa hivi watu …

Kinachotuunganisha

Kipo kitu kimoja ambacho kinatuunganisha sisi sote na kuwa kitu kimoja nacho ni imani. Uko katika mahusiano ya ndoa na huyo uliye naye kwa sababu unamwamini. Kama siyo imani wala usingekuwa naye. Imani ndiyo inatufanya sisi tuweze kuwa kitu kimoja. Umechagua kufanya kile unachofanya sasa kwa sababu una imani na kile ulichochagua. Tunajihusisha na watu …

Falsafa Inayojenga Kila Kitu

Binadamu ni viumbe vya hisia, hivyo pale unapojenga vitu kwa kutumia vitu ambavyo havigusi hisia zao za ndani ni rahisi kufanya kwa muda lakini ni ngumu kufanya kwa muda mrefu. Kipo kitu ambacho kinajenga kwenye kila eneo la maisha yetu, na kitu hicho ni upendo na wala siyo kitu kingine. Siyo kwamba vitu vingine havijengi …

Jisukume kufanya zaidi

Kuna wakati unapanga ratiba ya kufanya kitu, inapofika ule muda wa kufanya, badala ufanye kile ulichopanga kufanya, unaanza kutafuta sababu za kwa nini usifanye. Pale inapotokea hivyo, unajiambia utafanya baadaye, kesho na sababu nyingi nzuri, usikubali, JIKAMATE WEWE MWENYEWE, anza kufanya kile ulichopanga kufanya. Wewe anza tu hata kama hujisikii kufanya lakini baada ya muda …

Tulia

Watu wengi waliovurugwa na maisha huwa wanataka kile ambacho kimewavuruga wao, na wengine pia kiwavuruge.Watu wanakuwa na matatizo yao binafsi, hivyo wanatamani na wengine pia wawe kama wao. Usikubali kununua matatizo ya mtu, na njia nzuri ya kutokununua matatizo ya mtu ni kutokuwa kama wao. Kifupi, tulia, pale ambapo wanakuongelesha kwa jazba, wewe tulia waangalie …

Ukilala Na Mbwa Unaamka Na Kunguni

Kwenye maisha siku zote unapata kile unachotoa. Kuwa makini na utoaji wako, usitegemee kupata matokeo ambayo hujayafanyia kazi. Maisha ni utoaji. Na mafanikio yako kwa ujumla yanatokana na utoaji wako. Ili biashara yako iweze kukua inahitaji wewe utoe muda wako kuisimamia kwa karibu sana. Uwe muuzaji mkuu, meneja mkuu wa biashara yako, na msimamizi wa …

Wakati Mzuri Wa Kununua Mwamvuli

Wakati mzuri wa kuandaa paa lako ni wakati jua linawaka. Hii ina maana kwamba muda mzuri wa kujiandaa na kitu ni kabla ya kile kitu hakijatokea. Unaona wazi jinsi mvua inaponyesha miamvuli inauzwa kwa bei kubwa. Kama hutaki kununua mwambie kwa bei kubwa basi nunua kabla ya mvua.Muda mzuri wa kujiandaa na dharura ni kabla …

Design a site like this with WordPress.com
Get started