Bila Kitu Hiki Huwezi Kufanya Makubwa Kwenye Maisha Yako

Sababu za sisi kufanikiwa ziko nyingi sana. Na iko sababu moja ambayo inatufanya tuendelee kupata ushindi kamili. Kwenye maisha yako, kama ukikosa UJASIRI huwezi kupata kile unachotaka. Mwanafalsa Aristotle aliwahi kunukuliwa akisema, kamwe huwezi kufanya kitu chochote kwenye hii dunia kama huna ujasiri. Maisha yako yanabadilika au kutokubadilika kwa sababu moja tu ambayo ni ujasiri …

Chanzo Cha Usaliti

Ni asili ya binadamu kusalitiana. Na karibu kila eneo la maisha yetu tayari watu wameshasalitiana. Kama mtu anaweza kujisaliti yeye mwenyewe sembuse wewe? Nini chanzo cha usaliti na usaliti huwa unaanza kwa namna gani? Martin Luther aliwahi kunukuliwa akisema, kila usaliti huwa unaanza na UAMINIFU.Mtu akitaka kukusaliti, ataanza kwanza na GIA ya UAMINIFU. Atajenga uaminifu …

Usipotimiza Wajibu Wako Utakuja Kuulizwa

Kila mtu amepewa kazi yake hapa duniani. Na usipotimiza wajibu wako wa msingi, asili itakuja kukudai na kukuuliza. Lazima utimize kile unachopaswa kufanya. Kwa sababu ni wajibu wako kufanya. Kwa mfano, kwenye familia, kama mzazi humwambii mtoto ukweli, utakuja kuulizwa. Usikubali mtu apate matokeo hasi kwa sababu ya wewe kushindwa kutimiza majukumu yako. Wakati mwingine …

Ngumu Kama Bado Hujaanza

Mara nyingi kabla hatujaanza jambo lolote lile, huwa tunaangalia mwisho. Tutawezaje kufika kule tunakotaka kufika. Kwa mfano, kufanya kitu kwa siku 100 bila kuacha unaweza kuona ni nyingi. Lakini, ukiwa wewe unaangalia siku moja tu, ni rahisi sana kufikia malengo ya kufanya kitu kwa siku mia moja. Usiangalie matokeo, bali angalia pale ulipo sasa. Angalia …

Maisha Mabaya Kuishi

Ni maisha ambayo hayana maana kuishi. Ukiishi maisha ambayo hayana maana kuishi unapoteza maana yako. Maisha yako binafsi yanapaswa kuwa na maana kwako wewe mwenyewe. Kuwa na maana kwa wengine. Kama jamii unayoishi nayo haijivunii kuhusu wewe, unakuwa na maana gani ? Usiwe sehemu ya kero kwa watu wengine. Ishi maisha ambayo yana maana kwa …

Fanya Kwa Sababu

Kwenye maisha yako, fanya kile unachopaswa kufanya. Na unafanya kwa sababu ni sahihi kwako kufanya hivyo. Kwa mfano, unajua kabisa ukiwa barabarani wewe kama ni dereva ni muhimu kuvaa mkanda wakati unaendesha gari lako. Na unavaa mkanda kwa sababu ni salama kwako kufanya hivyo na siyo unafanya kwa sababu ya askari wa barabarani asikukamate. Kufanya …

Usizoee Kitu Chochote Kile

Kila wakati unapaswa kujiona mtu mpya kwenye kile unachofanya. Kamwe usizoee kile unachofanya hata siku moja.Kwa sababu mazoea huwa yanaua kile unachojua. Mazoea yanaharibu kila kitu kwenye maisha yako. Usiwe na mazoea kwenye biashara yako. Usiwe na mazoea kwenye kazi yako. Usiwe na mazoea kwenye Mahusiano yako. Usiwe na mazoea kwenye kile ulichochagua kufanya. Kila …

Ukikosa Sababu Hii Ni Rahisi Kuishia Njiani

Kila kitu kwenye maisha kina hitaji sababu. Watu wanafanya kitu kwa kusukumwa na kitu. Kwa mfano, huwezi kuamka mapema kila siku asubuhi kama huna sababu ya kuamka mapema asubuhi. Mtu anakuambia kisa cha kujitesa roho nini? Tunafanya kwa sababu tunasukumwa na kitu ndani yetu. Kama huna malengo makubwa na ndoto kubwa ni rahisi sana kuishi …

Hawa Ndiyo Wabinafsi Wa Mafanikio

Wote tunajua nafasi ya Mungu kwenye maisha yetu haiwezi kufananishwa na kitu chochote kile. Hata kama mtu hana dini lakini ana amini kuna Mungu. Mwingine ana sali sana lakini hafanikiwi na mwingine hasali na mambo yake yanaenda tu vizuri. Kweli, njia za Mungu hazichunguziki. Tuachane na hayo. Kuna watu kwenye zama hizi wamekuwa wabinafsi sana. …

Nani Anamlipa Nani

Ustaarabu kwenye kazi lazima uwepo. Yule ambaye umempa kazi anapaswa kufuata utaratibu wa kazi kama ulivyo na siyo kuja na utaratibu wake binafsi. Kwenye biashara hakuna mtu ambaye yuko juu ya biashara. Kila mtu anapaswa kufuata utaratibu wa kazi. Kila mtu ambaye anafanya kazi lazima apambanie kombe. Hakuna mtu ambaye atapata matokeo kirahisi. Kila mtu …

Design a site like this with WordPress.com
Get started