Ukizidishiwa Chenchi Utairudisha?

Leo asubuhi, nilikuwa na mkutano na mmoja wa washiriki katika huduma yetu tunayotoa ya CHUO CHA MAUZO ambaye anaishi nchini Uingereza. Katika maongezi yetu, aliniambia kwamba, uaminifu katika nchi anayoishi ni mkubwa sana.Kwa mfano, hivi karibuni alirudishiwa chenchi yake ambayo ilizidi katika huduma aliyolipia na siyo mara moja ni zaidi ya mara moja. Kwa upande …

Hakikisha Vitu Hivi Viwili Vinaendana Kwako

Rafiki, Kinachokufikisha wewe kwenye mafanikio ni ile sifa yako, jinsi ambavyo watu wanakuchukulia. Watu wanakuchukulia vile wanavyotaka wao kwa sababu wewe umewaonesha wewe ukoje.Na hii inatokana na namna unavyofanya mambo yako, Wala siyo kwa jinsi unavyosema unafanya, bali unavyofanya. Rafiki kama unataka kufanikiwa, hakikisha vitu viwili vinaendana kwako navyo ni maneno na matendo. Usiwe mtu …

Weka Kazi Ili Ufanikiwe

Rafiki,Iko wazi kabisa na wewe unajua kwamba, kama unataka kufanikiwa kwenye kitu chochote kile, lazima uweke kazi. Usitegemee kupata matokeo ambayo hutaki kuyafanyia kazi.Ni rahisi kukwepa majukumu yako, lakini ni ngumu kukwepa matokeo yake. Kama unajua unachofanya siyo sahihi kwa nini unaendelea kufanya?Kama unajua siyo kweli kwa nini unasema? Huwa tunakua kabisa nini tunachotakiwa kufanya …

Kama Hakiingizi Fedha Siyo Uwekezaji

Rafiki, Huwa tuna changanya kati ya mali na uwekezaji. Maana rahisi ya uwekezaji ni kile kinachoingiza fedha mfukoni. Kama una uwekezaji na hauingizi fedha huo siyo uwekezaji. Uwekezaji ni kile kinachoingiza fedha na siyo kutoa fedha mfukoni. Kwa mfano, nyumba ya kuishi siyo uwekezaji kwa sababu unatoa hela mfukoni kuihudumia na siyo nyumba kukuletea hela. …

Hakuna Mtu Mwenye Haya Maisha

Rafiki, Unapopitia changamoto kwenye maisha, unaweza kuona kama vile dunia ina kisirani na wewe. Unaweza kuona kama wengine maisha yao ni shwari na hawana kinachowasumbua. Ukweli ni kwamba, kwenye haya maisha kila mtu ana kitu kinachomsumbua, wako ambao wanasumbuliwa na maradhi, wako ambao wanasumbuliwa mwanamke, mwanaume, biashara, kazi, fedha na mengine yanayofanana na hayo.Sina uhakika …

Njia Pekee Ya Kutokurudi Nyuma

Asili yetu sisi binadamu ni kazi. Hata ukiona mikono yetu ilivyokaa ni imekaa kwa ajili ya kazi au kuwajibika. Hata watoto wadogo ukiwaacha sehemu fulani, huwezi kuwakuta wakikaa tu,lazima watawajibika kwa kitu chochote kile. Labda watajenga nyumba kwa mchanga au hata kwa maboxi. Hapa tunajifunza kwamba, uwajibikaji ni asili ya binadamu. Usipowajibika kwenye maisha yako, …

Jifunze Kutokana Na Majanga Yako

Rafiki, Hakuna wakati mzuri wa kujifunza kwenye maisha kama wakati wa majanga. Jua kwamba, majanga kwenye maisha yetu yanamfikia kila mtu na huwezi kuyakwepa. Na njia bora ni kujifunza kupitia majanga hayo ili kuwa bora zaidi. Na namna watu wanavyopokea majanga ni tofauti.Wako ambao wanayapokea na  wanajifunza kupitia majanga yao. Watu ambao wanayapokea  majanga katika …

Aliyejitoa Hana Maelezo

Rafiki, Kwenye haya maisha, maelezo huwa hayahitajiki bali watu wanahitaji matokeo. Haijalishi umepitia au unapitia nini, yule anayetegemea kupata kutoka kwako huwa anataka matokeo na siyo vinginevyo. Haitaji maelekezo yako, anahitaji kile anachotaka. Kama unaweza kutoa maelezo, kwa nini unashindwa kutoa matokeo? Jitahidi sana kwenye maisha yako, usiwe mtu wa maelezo bali kuwa mtu wa …

Jinsi Ya Kujua Kusudi Lako

Rafiki, Kila mtu amekuja duniani kwa kusudi lake, hivyo ni muhimu kujua umekuja duniani kwa kusudi gani. Usikae duniani kihasara, jua umetumwa kuja kukamilisha nini duniani na kamilisha hilo. Haupo hapa duniani kama minyoo, bali acha alama.Swali muhimu la kujua kusudi la maisha yako na kutengeneza maono yako ni kama ifuatavyo; Swali hilo ni KWA …

Siyo Uhalisia

Rafiki, Huwa tunatengeneza hofu kisha hofu inatutengeneza.Tunatengeneza mazingira ya hofu ambayo yanakuwa kama breki kwetu. Hofu ni kitu ambacho hakipo katika uhalisia, hofu ni zao la akili ambalo tunalitengeneza sisi wenyewe. Tunatengeneza picha kwenye akili yetu ambayo kiuhalisia hata hicho kitu hakipo. Usiwe na hofu yoyote kwenye maisha yako, kama kitu kimepangwa kutokea kitatokea tu. …

Design a site like this with WordPress.com
Get started