Wewe siyo kiranja wa dunia. Kwamba mambo yako kila siku yataenda kama vile unavyotaka. Unapaswa kuwa na unyenyekevu kwamba, dunia haiwezi kwenda vile unavyotaka wewe hata iweje.Uwe na mamlaka au huna, dunia haijali sana kuhusu hilo. Kuna uhakika fulani huwa tunajipa kwenye maisha yetu. Kwa sababu nina mamlaka juu ya kitu fulani au mtu fulani …
Kabla Ya Kuongea Jiulize Hivi
Rafiki yangu nikupendaye, Mwanafalsafa Plato anasema Werevu huongea kwa sababu wana kitu cha kuongea, ila wapumbavu huongea kwa sababu inabidi waseme kitu. Kama huna kitu cha kuongea, ni vema usiongee kitu. Kaa kimya, utaonekana mtu mwenye hekima. Wakati wowote unapotaka kuongea, jiulize je una kitu cha kuongea au na wewe unataka usikike tu kwamba umeongea? …
Majadiliano Yanatokea Wapi Tena?
Kabla hujapata fedha, unakuwa na mawazo mazuri sana. Unapanga kabisa ukipata fedha, kitu cha kwanza kufanya ni kuwekeza. Chakushangaza ni kwamba, pale tu unapoishika pesa, majadiliano ya ndani yanaanza. Utoe au usitoe.Majadiliano hayo yanatoka wapi? Kama ulishapanga kabla ya kupata fedha, tekeleza haraka na wala usiruhusu majadiliano.Hisia za kutokuwekeza huwa zina nguvu sana. Utaanza kujadiliana …
Kuwa Daraja La Wengine
Mafanikio yetu hapa duniani yanategemea wengine.Tunapaswa kuwa watu wa msaada kwa wengine, kuwasaidia wengine kwenye kile wanachopitia. Mafanikio yetu yanatokana na wengine. Kwa sababu chochote kile ambacho sisi hatuna, tunakipata kutoka kwa wengine. Wewe unaweza kuwa kikwazo kwa mtu mwingine kutokufanikiwa pale unaposhindwa kutimiza wajibu wako vizuri. Wewe unaweza kuwa daraja la wengine kufanikiwa pale …
Jifunze Kuwa Na Hivi Vitu
Mafanikio siyo kupata hiki na kukosa kile, siyo kutumia muda mwingi kwenye kazi na kukosa muda na familia, siyo kuwa bize na kazi na kusahau afya yako. Mafanikio ni kuwa na kila kitu, kuwa na fedha nyingi, kuwa na afya bora, kuna na mahusiano mazuri na wengine, kuwa vizuri kiimani na kuweza kushirikiana na wengine. …
Unaipeleka Wapi Nguvu Yako?
Rafiki yangu nikupendaye, Kila mtu ana nguvu ya kupenda kitu ndani yake. Changamoto ni kwamba nguvu hiyo unaipeleka wapi? Wapo ambao wanapeleka nguvu hiyo kwenye kufanya kazi, wapo wanaoipeleka kwenye kusaka fedha na wapo wanaopeleka nguvu hiyo kwenye ulevi na uteja. Wapo pia wanaopoteza nguvu hiyo kwa kupenda vitu ambavyo havina faida kwao, mfano kufuatilia …
Kama Unataka Kufanikiwa, Penda Kitu Hiki Hapa
Rafiki yangu nikupendaye, Huhitaji kufanya kile ambacho unakipenda ndiyo ufanikiwe, bali unahitaji kupenda kile unachofanya sasa. Watu wengi wamekuwa wakijidanganya kwamba pale walipo sasa hawapapendi na hivyo kutoweka juhudi kubwa, mwishowe wanajikuta wamenasa pale pale, iwe ni kazi au biashara. Siri ni hii rafiki, anza kupenda hapo ulipo sasa, anza kuweka juhudi zako zote kwenye …
Continue reading "Kama Unataka Kufanikiwa, Penda Kitu Hiki Hapa"
Mambo 11 Ya Kujifunza Kuhusu Kazi Kutoka Kwa Albert Hubbard Kwenda Kwa Mwajiriwa na Mwajiri
Albert Hubbard alikuwa ni mwandishi wa insha ya ujumbe kwenda Garcia. Na katika Isha yake hiyo, kuna mambo muhimu sana ya kujifunza kutoka kwake. Kama unamfanyia mtu, mfanyie kazi kweli. Kama anakulipa mshahara unaoweza kukukupatia mkate na siagi, mfanyie kazi. Mwongelee vizuri, fikiria mazuri kuhusu yeye, simama upande wake na tetea taasisi yake. Nadhani kama …
Nia Yako Itakupa Kile Unachotaka
Waswahili wanasema, penye nia pana njia. Ukiamua kuwa vile unavyotaka kuwa unakuwa kwa sababu nia yako ndiyo inaamua wewe uwe nani. Nia yako ya kutaka kitu, itakusukuma kupata hicho kitu. Mtu mwenye nia huwa hashindwi kitu. Je, una nia ya kupata nini? Kama una nia ya kitu fulani, ifanyie kazi nia yako na utaweza kuona …
Hakikisha Unakuwa Navyo Vyote
Rafiki, Uko msemo unaosema kwamba, haijalishi unajua nini, bali unamjua nani. Ni msemo wa kweli kabisa. Sina uhakika kama itakufaa lakini ninakushauri kuwa na vyote. Hakikisha unajua sana, yaani unabobea kwenye kitu fulani.Ubora wako utakukutanisha na koneksheni mbalimbali. Kama ukitegemea kupata dili halafu hujui, siyo muda mrefu utapoteza dili ulilopewa. Watu wanaokujua na kukupa koneksheni …